1 Mambo ya Nyakati
Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
5 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri na Magogu+ na Madai+ na Yavani+ na Tubali na Mesheki+ na Tirasi.+
6 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi+ na Rifathi+ na Togarma.+
7 Na wana wa Yavani walikuwa Elisha+ na Tarshishi,+ Kitimu+ na Rodanimu.+
8 Wana wa Hamu walikuwa Kushi+ na Misraimu,+ Putu+ na Kanaani.+
9 Na wana wa Kushi walikuwa Seba+ na Havila na Sabta+ na Raama+ na Sabteka.+
Na wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.+
10 Na Kushi akamzaa Nimrodi.+ Ni yeye wa kwanza kuwa mwanamume mwenye nguvu duniani.+
11 Misraimu naye akamzaa Ludimu+ na Anamimu na Lehabimu na Naftuhimu+ 12 na Pathrusimu+ na Kasluhimu+ (ambao Wafilisti+ walitokana nao) na Kaftorimu.+
13 Kanaani naye akamzaa Sidoni+ mzaliwa wake wa kwanza na Hethi+ 14 na Myebusi+ na Mwamori+ na Mgirgashi+ 15 na Mhivi+ na Mwarkia na Msini+ 16 na Mwarvadi+ na Msemari+ na Mhamathi.+
17 Wana wa Shemu+ walikuwa Elamu+ na Asihuru+ na Arpakshadi+ na Ludi+ na Aramu,
Na Usi na Huli na Getheri na Mashi.+
18 Arpakshadi naye akamzaa Shela,+ na Shela akamzaa Eberi.+
19 Na Eberi alizaa wana wawili. Jina la mmoja lilikuwa ni Pelegi,+ kwa sababu katika siku zake dunia ilikuwa imegawanyika; na jina la ndugu yake lilikuwa ni Yoktani.
20 Yoktani naye akazaa Almodadi na Shelefu na Hazarmavethi na Yera+ 21 na Hadoramu na Uzali na Dikla+ 22 na Obali na Abimaeli na Sheba+ 23 na Ofiri+ na Havila+ na Yobabu;+ hao wote ndio waliokuwa wana wa Yoktani.
28 Wana wa Abrahamu walikuwa Isaka+ na Ishmaeli.+
29 Hizi ndizo asili za familia zao: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayothi+ na Kedari+ na Adbeeli na Mibsamu,+ 30 Mishma na Duma,+ Masa, Hadadi+ na Tema, 31 Yeturi, Nafishi na Kedema.+ Hao ndio waliokuwa wana wa Ishmaeli.
32 Nao wana wa Ketura,+ suria wa Abrahamu,+ aliwazaa Zimrani na Yokshani na Medani+ na Midiani+ na Ishbaki+ na Shua.+
Na wana wa Yokshani walikuwa Sheba na Dedani.+
33 Na wana wa Midiani walikuwa Efa+ na Eferi na Hanoki na Abida na Eldaa.+
Wote hao walikuwa wana wa Ketura.
34 Naye Abrahamu akamzaa Isaka.+ Wana wa Isaka walikuwa Esau+ na Israeli.+
35 Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli+ na Yeushi na Yalamu na Kora.+
36 Wana wa Elifazi walikuwa Temani+ na Omari, Sefo na Gatamu, Kenasi+ na Timna+ na Amaleki.+
37 Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shamma na Miza.+
38 Na wana wa Seiri+ walikuwa Lotani na Shobali na Sibeoni na Ana+ na Dishoni na Ezeri na Dishani.+
39 Na wana wa Lotani walikuwa Hori na Homamu. Na dada ya Lotani alikuwa Timna.+
40 Wana wa Shobali walikuwa Alvani na Manahathi na Ebali, Shefo na Onamu.+
Na wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana.+
41 Wana wa Ana walikuwa Dishoni.+
Na wana wa Dishoni walikuwa Hemdani na Eshbani na Ithrani na Kerani.+
42 Wana wa Ezeri+ walikuwa Bilhani na Zaavani na Akani.+
Wana wa Dishani walikuwa Usi na Arani.+
43 Na hawa ndio wafalme waliotawala katika nchi ya Edomu+ kabla ya mfalme+ yeyote kuwatawala wana wa Israeli: Bela mwana wa Beori, ambaye jina la jiji lake lilikuwa Dinhaba.+ 44 Mwishowe Bela akafa, na Yobabu mwana wa Zera+ kutoka Bosra+ akaanza kutawala mahali pake. 45 Mwishowe Yobabu akafa, na Hushamu+ kutoka katika nchi ya Watemani+ akaanza kutawala mahali pake. 46 Mwishowe Hushamu akafa, na Hadadi+ mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani+ katika uwanda wa Moabu, akaanza kutawala mahali pake. Na jina la jiji lake lilikuwa Avithi.+ 47 Mwishowe Hadadi akafa, na Samla kutoka Masreka+ akaanza kutawala mahali pake. 48 Mwishowe Samla akafa, na Shauli kutoka Rehobothi+ kando ya ule Mto akaanza kutawala mahali pake. 49 Mwishowe Shauli akafa, na Baal-hanani mwana wa Akbori+ akaanza kutawala mahali pake. 50 Mwishowe Baal-hanani akafa, na Hadadi akaanza kutawala mahali pake; na jina la jiji lake lilikuwa Pau, nalo jina la mke wake lilikuwa Mehetabeli, binti ya Matredi, binti ya Mezahabu.+ 51 Mwishowe Hadadi akafa.
Nao mashehe wa Edomu wakawa ni shehe Timna, shehe Alva, shehe Yethethi,+ 52 shehe Oholibama, shehe Ela, shehe Pinoni,+ 53 shehe Kenasi, shehe Temani, shehe Mibsari,+ 54 shehe Magdieli, shehe Iramu.+ Hao ndio waliokuwa mashehe+ wa Edomu.