Nehemia
11 Basi wakuu+ wa watu walikuwa na makao yao katika Yerusalemu;+ lakini wale watu wengine walipiga kura+ kuleta ndani mtu mmoja kati ya watu kumi ili waishi Yerusalemu lile jiji takatifu,+ na wale watu wengine, sehemu tisa, waishi katika yale majiji mengine. 2 Na zaidi ya hayo, watu wakawabariki+ watu wote waliojitolea+ kukaa Yerusalemu.
3 Na hawa ndio vichwa vya wilaya ya utawala+ ambao walikaa Yerusalemu;+ lakini katika majiji ya Yuda walikaa Israeli,+ makuhani+ na Walawi,+ na Wanethini+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ kila mmoja katika urithi wake, katika majiji yao.+
4 Pia, sehemu ya wana wa Yuda na sehemu ya wana wa Benyamini walikaa Yerusalemu.+ Kati ya wana wa Yuda kulikuwa na Athaya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi;+ 5 na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mshela. 6 Wana wote wa Perezi waliokuwa wakikaa Yerusalemu walikuwa 468, wanaume wenye uwezo.
7 Na hawa ndio waliokuwa wana wa Benyamini:+ Salu mwana wa Meshulamu+ mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Ithieli mwana wa Yeshaya; 8 na baada yake Gabai na Salai, wanaume 928; 9 na Yoeli mwana wa Zikri, mwangalizi juu yao, na Yuda mwana wa Hasenua juu ya jiji akiwa mwangalizi wa pili.
10 Wa makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu,+ Yakini,+ 11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu+ mwana wa Sadoki+ mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli; 12 na ndugu zao waliokuwa wakifanya kazi ya ile nyumba,+ watu 822; na Adaya mwana wa Yerohamu+ mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya,+ 13 na ndugu zake, vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ watu 242, na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemothi mwana wa Imeri, 14 na ndugu zao, mashujaa,+ wanaume wenye nguvu 128, na kulikuwa na mwangalizi+ juu yao, Zabdieli mwana wa wakuu.
15 Na wa Walawi:+ Shemaya mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia+ mwana wa Buni, 16 na Shabethai+ na Yozabadi,+ wa vichwa vya Walawi, juu ya kazi za nje za nyumba ya Mungu wa kweli; 17 na Matania+ mwenyewe, mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa nyimbo za sifa,+ ndiye aliyesifu katika sala,+ na Bakbukia alikuwa wa pili wa ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali+ mwana wa Yeduthuni.+ 18 Walawi wote katika jiji takatifu+ walikuwa 284.
19 Na watunza-malango+ walikuwa Akubu, Talmoni+ na ndugu zao waliokuwa wakilinda malangoni,+ 172.
20 Na wale wengine wa Israeli, wa makuhani na wa Walawi, walikuwa katika majiji mengine yote ya Yuda, kila mmoja katika fungu lake mwenyewe la urithi.+ 21 Na Wanethini+ walikuwa wakikaa katika Ofeli;+ na Siha na Gishpa walikuwa juu ya Wanethini.
22 Na mwangalizi+ wa Walawi katika Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika+ wa wana wa Asafu,+ waimbaji,+ kuhusiana na kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli. 23 Kwa maana mfalme alikuwa ametoa amri kwa ajili yao,+ na kulikuwa na mpango kamili kwa ajili ya waimbaji kulingana na mahitaji ya kila siku.+ 24 Na Pethahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa kando ya mfalme kuhusiana na kila jambo la watu.
25 Na kuhusu makao+ katika mashamba yao, kulikuwa na sehemu ya wana wa Yuda waliokaa katika Kiriath-arba+ na miji yake ya kandokando na katika Diboni na miji yake ya kandokando na katika Yekabzeeli+ na makao yake, 26 na katika Yeshua na katika Molada+ na katika Beth-peleti+ 27 na katika Hasar-shuali+ na katika Beer-sheba+ na miji yake ya kandokando 28 na katika Siklagi+ na katika Mekona na miji yake ya kandokando 29 na katika En-rimoni+ na katika Sora+ na katika Yarmuthi,+ 30 Zanoa,+ Adulamu+ na makao yake, Lakishi+ na mashamba yake, Azeka+ na miji yake ya kandokando. Nao wakapiga kambi kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.+
31 Na wana wa Benyamini walikuwa kutoka Geba,+ Mikmashi+ na Aiya+ na Betheli+ na miji yake ya kandokando, 32 Anathothi,+ Nobu,+ Ananiya, 33 Hasori, Rama,+ Gitaimu,+ 34 Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35 Lodi+ na Ono,+ bonde la mafundi. 36 Na kati ya Walawi kulikuwa na migawanyo ya Yuda iliyokaa Benyamini.