Wimbo wa Sulemani
4 “Tazama! Wewe ni mrembo,+ ewe msichana mwenzi wangu. Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni kama ya njiwa,+ nyuma ya ushungi wako.+ Nywele zako ni kama kundi la mbuzi+ ambao wameruka chini kutoka eneo lenye milima la Gileadi.+ 2 Meno yako ni kama kundi la kondoo-jike waliokatwa manyoya hivi karibuni+ ambao wamepanda kutoka kuoshwa, wote wanazaa mapacha, wala hakuna yeyote kati yao amepoteza watoto wake. 3 Midomo yako ni kama tu uzi mwekundu, na maneno yako yanakubalika.+ Kama kipande cha komamanga ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya ushungi wako.+ 4 Shingo yako+ ni kama mnara+ wa Daudi, uliojengwa kwa mistari ya mawe, ambao juu yake hutungikwa ngao elfu, ngao zote za mviringo+ za wanaume wenye nguvu. 5 Maziwa yako mawili+ ni kama watoto wadogo wawili, mapacha ya swala-jike, ambao wanalisha katikati ya mayungiyungi.”+
6 “Mpaka mchana uvume upepo mtulivu+ na vivuli viwe vimekimbia, nitakwenda zangu kwenye mlima wa manemane na kwenye kilima cha ubani.”+
7 “Wewe ni mrembo kabisa,+ ewe msichana mwenzi wangu, wala hamna kasoro ndani yako.+ 8 Na uje pamoja nami kutoka Lebanoni, ewe bibi-arusi,+ uje pamoja nami kutoka Lebanoni.+ Ushuke kutoka kilele cha Milima ya Anti-Lebanoni, kutoka kilele cha Seniri,+ naam, Hermoni,+ kutoka katika matundu ya simba, kutoka katika milima ya chui. 9 Umefanya moyo wangu upige, ewe dada yangu,+ bibi-arusi wangu,+ umefanya moyo wangu upige kwa moja la macho yako,+ kwa kidani kimoja cha mkufu wako. 10 Jinsi yalivyo mazuri maonyesho yako ya mapenzi,+ ewe dada yangu, bibi-arusi wangu! Jinsi maonyesho yako ya mapenzi yalivyo bora kuliko divai na harufu nzuri ya mafuta yako kuliko namna zote za manukato!+ 11 Midomo yako inadondosha asali ya sega,+ ewe bibi-arusi wangu. Asali+ na maziwa viko chini ya ulimi wako, na harufu nzuri ya mavazi yako ni kama harufu nzuri+ ya Lebanoni. 12 Dada yangu,+ bibi-arusi wangu, ni bustani iliyowekewa boma, bubujiko lililofungwa kwa kutiwa muhuri. 13 Ngozi yako ni paradiso ya makomamanga, yenye matunda bora kabisa,+ mimea ya hina pamoja na mimea ya nardo;+ 14 nardo+ na zafarani,+ kane+ na mdalasini,+ pamoja na namna zote za miti ya ubani, manemane na udi,+ pamoja na manukato yote yaliyo bora zaidi;+ 15 na bubujiko la bustani, kisima cha maji safi,+ na vijito vinavyotiririka kutoka Lebanoni.+ 16 Amka, ewe upepo wa kaskazini, ingia, ewe upepo wa kusini.+ Vuma juu ya bustani yangu.+ Manukato yake na yatiririke.”
“Mpenzi wangu na aje katika bustani yake, ale matunda yake yaliyo bora kabisa.”