Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Kumbuka: Usisahau jinsi ambavyo umemchokoza Yehova Mungu wako nyikani.+ Tangu siku uliyotoka katika nchi ya Misri mpaka mlipofika mahali hapa ninyi mmekuwa wenye tabia ya kumwasi Yehova.+

  • 2 Wafalme 17:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 na wana wa Israeli wakatafuta mambo ambayo hayakuwa sawa kumwelekea Yehova Mungu wao,+ wakaendelea kujijengea mahali pa juu+ katika majiji yao yote, kuanzia mnara+ wa walinzi mpaka jiji lenye ngome;

  • Nehemia 9:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “Nao wenyewe, mababu zetu, wakatenda kwa kimbelembele+ na kufanya shingo zao kuwa ngumu,+ wala hawakusikiliza amri zako.

  • Zaburi 106:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Tumetenda dhambi kama mababu zetu;+

      Tumefanya kosa; tumetenda kwa uovu.+

  • Yeremia 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Nami mwishowe nikawaleta ninyi katika nchi yenye mashamba ya matunda, ili mle matunda yake na vitu vyake vyema.+ Lakini mkaingia na kuitia unajisi nchi yangu; nanyi mkaufanya urithi wangu kuwa chukizo.+

  • Yeremia 3:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Tunalala katika aibu+ yetu, na fedheha yetu inaendelea kutufunika;+ kwa maana tumemtendea dhambi+ Yehova Mungu wetu, sisi na baba zetu tangu ujana wetu na kuendelea mpaka leo hii,+ nasi hatukuitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”+

  • Ezekieli 16:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “ ‘Nami nikaja nikipita kando yako nikakuona, na, tazama! wakati wako ulikuwa wakati wa maonyesho ya upendo.+ Kwa hiyo nikatandaza upindo wa nguo yangu juu yako+ na kuufunika utupu wako na kukutolea ahadi yenye kiapo na kuingia katika agano pamoja nawe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘na kwa hiyo ukawa wangu.+

  • Ezekieli 20:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Nami nikawaleta katika nchi+ ambayo nilikuwa nimeuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa wao.+ Walipoona kila kilima kilichoinuka+ na kila mti wenye matawi mengi, ndipo wakaanza kutoa dhabihu+ zao huko na kutolea huko matoleo yao yenye kuudhi, na kutolea huko harufu zao za kutuliza+ na kumimina huko matoleo yao ya kinywaji.+

  • Matendo 7:51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 “Ninyi watu wenye shingo ngumu na wasiotahiriwa katika mioyo+ na masikio, sikuzote mnaipinga roho takatifu; kama mababu zenu walivyofanya, ndivyo ninyi mnavyofanya.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki