Zekaria
“Neno la Yehova linashindana na nchi ya Hadraki, nalo linapumzika Damasko;+ kwa maana Yehova ameweka jicho juu ya mtu wa udongo+ na juu ya makabila yote ya Israeli. 2 Na Hamathi+ litapakana naye pia; Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana ana hekima sana.+ 3 Tiro nalo likajijengea boma, na kukusanya fedha kama mavumbi na dhahabu kama matope ya barabarani.+ 4 Tazama! Yehova mwenyewe atamfukuza, naye hakika atalipiga na kuliangusha baharini jeshi lake;+ naye mwenyewe atateketezwa motoni.+ 5 Ashkeloni litaona na kuogopa; Gaza nalo pia litakuwa na maumivu makali sana; Ekroni+ pia, kwa sababu tumaini lake analotazamia+ litaona aibu. Na mfalme ataangamizwa kutoka Gaza, nalo Ashkeloni halitakaliwa na watu.+ 6 Na mwana-haramu+ ataketi huko Ashdodi,+ nami nitakikatilia mbali kiburi cha Mfilisti.+ 7 Nami nitaviondoa vitu vyake vyenye madoa ya damu kinywani mwake na kuyaondoa machukizo yake kutoka katikati ya meno+ yake, naye mwenyewe atabaki kwa ajili ya Mungu wetu; naye atakuwa kama shehe+ katika Yuda,+ na Ekroni kama Myebusi.+ 8 Nami nitapiga kambi kama mlinzi wa mbele kwa ajili ya nyumba yangu,+ ili kusiwe na mtu yeyote anayepita kati wala anayerudi; wala msimamizi wa kazi+ hatapita tena kwao, kwa maana sasa nimeyaona kwa macho yangu.+
9 “Shangilia sana, Ee binti Sayuni.+ Piga kelele za ushindi,+ Ee binti Yerusalemu. Tazama! mfalme+ wako anakuja kwako.+ Yeye ni mwadilifu, ndiyo, ameokolewa;+ ni mnyenyekevu,+ naye amepanda juu ya punda, juu ya mnyama mkomavu, mwana wa punda-jike.+ 10 Nami nitalikatilia mbali gari la vita kutoka katika Efraimu na farasi kutoka katika Yerusalemu.+ Na upinde wa mapigano+ utakatiliwa mbali. Naye atasema amani kwa mataifa;+ na utawala wake utakuwa kutoka bahari mpaka bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.+
11 “Nawe pia, Ee mwanamke, nitawatoa wafungwa+ wako kutoka katika shimo ambalo halina maji kwa kutumia damu ya agano+ lako.
12 “Rudini katika ngome,+ enyi wafungwa wa lile tumaini.+
“Pia, leo ninakuambia, ‘Nitakulipa fungu lililo mara mbili,+ Ee mwanamke. 13 Kwa maana nitamkanyaga Yuda kama upinde wangu. Nami nitamtia Efraimu katika upinde, nami nitawaamsha wana wako, Ee Sayuni, kupigana na wana wako,+ Ee Ugiriki,+ nami nitakufanya kama upanga wa mwanamume mwenye nguvu.’+ 14 Na Yehova mwenyewe ataonekana juu yao,+ na mshale wake utaenda kama umeme.+ Naye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atapiga baragumu,+ ataenda pamoja na dhoruba za upepo wa kusini.+ 15 Yehova wa majeshi mwenyewe atawalinda wao, nao watakula+ na kuyatiisha mawe ya kombeo. Nao watakunywa+—wafanye kelele—kana kwamba kuna divai; nao watajazwa kama bakuli, kama pembe za madhabahu.+
16 “Na Yehova Mungu wao atawaokoa+ katika siku hiyo kama kundi la watu wake;+ kwa maana watakuwa kama mawe ya taji yanayong’aa juu ya nchi yake.+ 17 Kwa maana lo! jinsi ulivyo mkuu wema wake,+ na jinsi ulivyo mkuu uzuri wake!+ Nafaka ndiyo itakayowasitawisha vijana, na divai mpya nayo itawasitawisha mabikira.”+