1 Yohana
5 Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa kutokana na Mungu,+ na kila mtu ambaye humpenda yule ambaye alisababisha kuzaliwa humpenda yeye ambaye amezaliwa kutokana na huyo.+ 2 Kwa hili sisi tunajua kwamba tunawapenda+ watoto wa Mungu,+ wakati tunapompenda Mungu na kutenda amri zake.+ 3 Kwa maana kumpenda+ Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake;+ na bado amri zake si mzigo mzito,+ 4 kwa sababu kila kitu ambacho kimezaliwa+ kutokana na Mungu huushinda ulimwengu.+ Na huu ndio ushindi+ ambao umeushinda+ ulimwengu, imani+ yetu.
5 Ni nani ambaye huushinda+ ulimwengu+ isipokuwa yeye aliye na imani+ kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu?+ 6 Huyu ndiye aliyekuja kwa njia ya maji na damu, Yesu Kristo; si kwa maji+ tu, bali kwa maji na kwa damu.+ Na roho+ ndiyo inayotoa ushahidi, kwa sababu roho ndiyo kweli. 7 Kwa maana kuna vitatu vinavyotoa ushahidi, 8 roho+ na maji+ na damu,+ na hivyo vitatu vinakubaliana.+
9 Tukipokea ushahidi ambao wanadamu hutoa,+ ushahidi ambao Mungu hutoa ni mkuu zaidi, kwa sababu huu ndio ushahidi ambao Mungu hutoa, jambo la kwamba ametoa ushahidi+ kumhusu Mwana wake. 10 Mtu anayemwamini Mwana wa Mungu, ushahidi+ umetolewa kwa habari yake. Mtu asiye na imani katika Mungu amemfanya yeye kuwa mwongo,+ kwa sababu hakuwa na imani katika ushahidi uliotolewa,+ ambao Mungu akiwa shahidi+ ametoa kumhusu Mwana wake. 11 Na huu ndio ushahidi ambao umetolewa, kwamba Mungu alitupa sisi uzima wa milele,+ na uzima huu umo ndani ya Mwana+ wake. 12 Yeye ambaye ana Mwana ana uzima huu; yeye ambaye hana Mwana wa Mungu hana uzima huu.+
13 Ninawaandikia mambo haya ili mjue kwamba ninyi mnao uzima wa milele,+ ninyi ambao mmekuwa na imani katika jina la Mwana wa Mungu.+ 14 Na huu ndio uhakika ambao tunao kwake,+ kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.+ 15 Zaidi ya hayo, tukijua kwamba yeye hutusikia kwa habari ya jambo lolote tunaloomba,+ tunajua tutapata mambo yaliyoombwa kwa kuwa tumeyaomba kwake.+
16 Yeyote akimwona ndugu yake anafanya dhambi, dhambi ambayo haileti kifo,+ yeye ataomba, naye atampa huyo uzima,+ ndiyo, kwa wale ambao hawafanyi dhambi inayoleta kifo.+ Kuna dhambi ambayo huleta kifo. Ni kuhusu dhambi hiyo kwamba simwambii aombe.+ 17 Ukosefu wote wa uadilifu ni dhambi;+ na bado kuna dhambi ambayo haileti kifo.
18 Tunajua kwamba kila mtu ambaye amezaliwa kutokana na Mungu+ hana mazoea ya kufanya dhambi, lakini yeye hulindwa na Yule+ ambaye amezaliwa kutokana na Mungu, na yule mwovu hamshiki imara.+ 19 Tunajua tunatokana na Mungu,+ lakini ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.+ 20 Lakini tunajua kwamba Mwana wa Mungu amekuja,+ naye ametupa sisi uwezo wa akili+ ili tupate kumjua yule wa kweli.+ Na sisi tumo katika muungano+ na yule wa kweli, kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyo ndiye Mungu wa kweli+ na uzima wa milele.+ 21 Watoto wadogo, jilindeni na sanamu.+