Waefeso
4 Kwa hiyo, mimi, niliye mfungwa+ katika Bwana, nawasihi ninyi mtembee kwa kuustahili+ mwito mlioitiwa,+ 2 mkiwa na unyenyekevu kamili wa akili+ na upole, mkiwa na ustahimilivu,+ mkivumiliana katika upendo,+ 3 mkijitahidi sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.+ 4 Kuna mwili mmoja,+ na roho moja,+ kama vile mlivyoitwa katika tumaini+ moja mliloitiwa; 5 Bwana mmoja,+ imani moja,+ ubatizo mmoja;+ 6 Mungu mmoja+ na Baba wa watu wote, aliye juu ya wote na kupitia wote na katika wote.
7 Basi kila mmoja wetu alipewa fadhili zisizostahiliwa+ kulingana na jinsi Kristo alivyoipima hiyo zawadi ya bure.+ 8 Kwa hiyo anasema: “Alipopanda juu alichukua mateka; alitoa zawadi katika wanadamu.”+ 9 Basi neno “alipopanda,”+ linamaanisha nini isipokuwa kwamba alishuka pia katika maeneo ya chini zaidi, yaani, dunia?+ 10 Yule aliyeshuka ndiye pia aliyepanda+ juu zaidi ya mbingu+ zote, ili avijaze+ vitu vyote.
11 Naye alitoa wengine kuwa mitume,+ wengine kuwa manabii,+ wengine kuwa waeneza-injili,+ wengine kuwa wachungaji na walimu,+ 12 kwa kusudi la kuwarekebisha+ upya watakatifu, kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo,+ 13 mpaka sisi sote tuufikie umoja katika imani na katika ujuzi sahihi wa Mwana wa Mungu, kufikia kuwa mtu aliyekomaa,+ kufikia kipimo cha kimo ambacho ni cha ujazo wa Kristo;+ 14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukirushwa huku na huku+ kama kwa mawimbi na kuchukuliwa huku na huku na kila upepo wa fundisho+ kupitia udanganyifu+ wa watu, kwa njia ya ujanja katika kutunga kosa. 15 Lakini tukisema kweli,+ na tukue kwa upendo+ katika mambo yote ndani yake yeye aliye kichwa,+ Kristo. 16 Kutoka katika yeye mwili wote,+ kwa kuunganishwa pamoja kwa upatano na kufanywa ushirikiane kupitia kila kiungo ambacho hutoa kile kinachohitajiwa, kulingana na utendaji wa kila kiungo kimoja-kimoja katika kipimo kinachofaa, hutokeza ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.+
17 Kwa hiyo, nasema hili na kulitolea ushahidi katika Bwana, kwamba msiendelee tena kutembea kama vile mataifa+ wanavyotembea pia katika ubatili wa akili+ zao, 18 huku wakiwa katika giza kiakili,+ na kutenganishwa mbali+ na uzima ambao ni wa Mungu, kwa sababu ya kule kutojua+ ambako kumo ndani yao, kwa sababu ya ugumu+ wa mioyo yao. 19 Wakiisha kuishiwa na ufahamu wote wa maadili,+ walijitoa wenyewe ili kuwa na mwenendo mpotovu+ na kufanya ukosefu wa usafi+ wa kila namna kwa pupa.+
20 Lakini ninyi hamkujifunza Kristo kuwa hivyo,+ 21 mradi tu mlimsikia yeye na mlifundishwa kupitia yeye,+ kama vile kweli+ ilivyo katika Yesu, 22 kwamba mnapaswa kuuondolea mbali utu wa zamani+ unaolingana na mwenendo wenu wa kwanza na ambao unaharibiwa+ kulingana na tamaa zake za udanganyifu;+ 23 bali kwamba mnapaswa kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili yenu,+ 24 na mnapaswa kuvaa+ utu mpya+ ulioumbwa+ kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli+ na ushikamanifu.
25 Kwa hiyo, sasa kwa kuwa mmeuondolea mbali uwongo,+ semeni kweli kila mmoja wenu na jirani yake,+ kwa sababu sisi ni viungo vya mtu na mwenzake.+ 26 Iweni na ghadhabu, lakini msitende dhambi;+ jua lisitue mkiwa katika hali ya kuchokozeka,+ 27 wala msimpe Ibilisi nafasi.+ 28 Mwizi asiibe tena,+ bali afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema,+ ili awe na kitu cha kumgawia mtu aliye na uhitaji.+ 29 Neno lililooza na lisitoke kinywani mwenu,+ bali neno lolote ambalo ni jema kwa ajili ya kujenga kulingana na uhitaji, ili liwape wasikiaji lile linalofaa.+ 30 Pia, msiwe mkiihuzunisha roho takatifu+ ya Mungu, ambayo kupitia hiyo mmetiwa muhuri+ kwa ajili ya siku ya kuachiliwa huru kupitia fidia.+
31 Uchungu wote wenye uovu+ na hasira na ghadhabu na kupiga kelele na matukano+ na viondolewe mbali kutoka kwenu pamoja na ubaya wote.+ 32 Bali iweni wenye fadhili+ ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo,+ mkisameheana kwa hiari kama vile Mungu pia kupitia Kristo alivyowasamehe ninyi kwa hiari.+