Isaya
64 Laiti ungezipasua mbingu, ushuke chini,+ ili milima itetemeke kwa sababu yako,+ 2 kama wakati moto unapowasha vichaka, na moto kuyachemsha maji, ili kuwajulisha adui zako jina lako,+ ili mataifa yafadhaike kwa sababu yako!+ 3 Ulipofanya mambo yenye kuogopesha+ ambayo hatungeweza kuyatumaini, ulishuka chini. Milima ilitetemeka kwa sababu yako.+ 4 Na kutoka zamani za kale hakuna aliyesikia,+ wala hakuna aliyetega sikio, wala hakuna jicho lililomwona Mungu, isipokuwa wewe,+ unayetenda kwa ajili ya mtu anayeendelea kumtarajia huyo.+ 5 Umekutana na yule anayefurahi na kutenda uadilifu,+ wale wanaoendelea kukukumbuka katika njia zako mwenyewe.+
Tazama! Wewe ulikuwa na ghadhabu,+ huku sisi tukiendelea kutenda dhambi+—katika hizo muda mrefu, na je, sisi tuokolewe?+ 6 Nasi tunakuwa kama mtu asiye safi, sisi sote, na matendo yetu yote ya uadilifu ni kama vazi la vipindi vya hedhi;+ nasi tutafifia kama majani,+ sisi sote, na makosa yetu yatatuchukua kama upepo.+ 7 Na hakuna yeyote anayeliitia jina lako,+ hakuna yeyote anayeamka ili akushike; kwa maana umeuficha uso wako kutoka kwetu,+ nawe unatuyeyusha+ kwa nguvu za kosa letu.
8 Na sasa, Ee Yehova, wewe ni Baba yetu.+ Sisi ni udongo,+ nawe ni Mfinyanzi+ wetu; nasi sote ni kazi ya mkono wako.+ 9 Usiwe na ghadhabu kupindukia,+ Ee Yehova, wala usilikumbuke milele kosa letu.+ Tazama, sasa, tafadhali: sisi sote ni watu wako.+ 10 Majiji yako matakatifu+ yamekuwa nyika. Sayuni+ umekuwa nyika tupu, Yerusalemu limekuwa mahame yenye ukiwa.+ 11 Nyumba yetu ya utakatifu na uzuri,+ ambayo ndani yake mababu zetu walikusifu wewe,+ imekuwa kitu cha kuteketezwa motoni;+ na kila kimoja cha vitu vyetu vyenye kutamanika+ kimeharibika. 12 Mbele ya mambo hayo yote, je, utaendelea kujizuia,+ Ee Yehova? Je, utanyamaza na kutuacha tuteseke kupindukia?+