Ezekieli
9 Naye akaita masikioni mwangu kwa sauti kubwa, na kusema: “Waleteni karibu wale wanaolikazia jiji fikira, kila mmoja wao akiwa na silaha yake mkononi mwake ili kuleta uharibifu!”
2 Na, tazama! kulikuwa na wanaume sita wakija kutoka upande wa lango la juu+ linaloelekea kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha yake ya kuponda mkononi mwake; na kulikuwa na mwanamume mmoja kati yao aliyevaa kitani,+ akiwa na kidau cha wino kiunoni, nao wakaingia ndani na kusimama kando ya madhabahu ya shaba.+
3 Nao utukufu wa Mungu wa Israeli,+ uliondolewa juu ya makerubi+ ambao ulikuwa juu yao kwenye mlango wa nyumba hiyo,+ naye akaanza kumwita yule mwanamume aliyevaa kitani,+ ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni. 4 Na Yehova akamwambia: “Pita katikati ya jiji, katikati ya Yerusalemu, nawe lazima utie alama kwenye mapaji ya uso ya watu wanaougua na kulia+ kwa sababu ya machukizo yote yanayofanywa katikati yake.”+
5 Naye akawaambia hawa wengine masikioni mwangu: “Piteni katikati ya jiji nyuma yake na kupiga. Jicho lenu lisisikitike, wala msiwe na huruma yoyote.+ 6 Mzee, kijana na bikira na mtoto mdogo na wanawake+ mtawaua kabisa—mtawaharibu. Lakini mtu yeyote ambaye ana ile alama msimkaribie,+ nanyi mnapaswa kuanzia patakatifu pangu.”+ Kwa hiyo wakaanza na wale wanaume wazee waliokuwa mbele ya nyumba.+ 7 Naye akazidi kuwaambia: “Itieni nyumba unajisi na kuzijaza nyua kwa wale waliouawa.+ Nendeni!” nao wakaenda na kupiga jijini.
8 Na ikawa kwamba, walipokuwa wakipiga nami nikiwa nimeachwa, nikaanguka kifudifudi,+ nikapaaza kilio, na kusema: “Ole+ wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, unawaharibu mabaki wote wa Israeli huku ukimwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”+
9 Kwa hiyo akaniambia: “Kosa la nyumba ya Israeli na Yuda+ ni kubwa, kubwa sana,+ na nchi imejaa umwagaji wa damu+ nalo jiji limejaa upotovu;+ kwa maana wamesema, ‘Yehova ameiacha nchi hii,+ na Yehova haoni.’+ 10 Na mimi pia, jicho langu halitasikitika,+ wala sitaonyesha huruma.+ Hakika nitaileta njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”+
11 Na, tazama! yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni, akaleta neno, na kusema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”+