Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itapanga Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa kipindi cha mkusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho kama inavyohitajika ili kuruhusu kuhudhuria “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya na pitio la dakika 30 la mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma litakalofuata. Pitio hilo la siku baada ya siku la mkusanyiko wa wilaya lapaswa kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wanaostahili ambao wataweza kukazia hoja zenye kutokeza. Pitio lililotayarishwa vizuri litasaidia kutaniko kukumbuka hoja za msingi kwa ajili ya utumizi wa kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na yaliyoonwa yatakayosimuliwa yapasa kuwa mafupi na yenye kugonga kichwa cha msumari.
Juma Linaloanza Oktoba 2
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Msifu Yehova Sikuzote.” Maswali na majibu. Kazia utumizi wa Maandiko yaliyoonyeshwa na yaliyonukuliwa.
Dak. 20: “Toa Magazeti Katika Kila Pindi.” Zungumzia mambo makuu, kisha upitie makala ambazo huenda zitatumiwa katika kutoa matoleo ya karibuni zaidi. Uwe na maonyesho mawili au matatu.
Wimbo 153 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 9
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: “‘Wasifaji Wenye Shangwe’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995.” Maswali na majibu ya mafungu 1-15.
Dak. 20: “Je, Tunakesha—Tukiepuka Vikengeusha-Fikira?” Maswali na majibu. Kadiri wakati unavyoruhusu, toa maelezo ya ziada yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1992, kurasa 20-22.
Wimbo 128 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Elekeza uangalifu kwenye kijitabu Good News for All Nations, ambacho hutoa utoaji wa mlango kwa mlango katika lugha tofauti-tofauti 59. Tia moyo utumizi wa kijitabu hiki ikiwa watu wenye kunena lugha ya kigeni wanapatikana katika eneo.
Dak. 20: “‘Wasifaji Wenye Shangwe’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995.” Maswali na majibu ya mafungu 16-26. Pitia “Vikumbusha vya Mkusanyiko wa Wilaya.” Wakati ukiruhusu, pitia habari zifaazo kutoka “Urahisishaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995,” ambayo ilipatikana katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1995.
Dak. 15: “Ziara za Kurudia Zenye Kusudi.” Zungumzia malengo yetu katika kufanya ziara za kurudia. Panga kuwe na wahubiri wenye uwezo wafanye wonyesho wa toaji mbili tofauti. Panga mhubiri aeleze jinsi kazi hii hugharimiwa.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Twahitaji Kutaniko.” Maswali na majibu.
Dak. 20: Elekeza Upendezi Kwenye Tengenezo. Mwangalizi wa utumishi aongoza mazungumzo na wahubiri wawili au watatu, akitumia broshua Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote. Eleza kwa nini ni jambo lenye mafaa kuwajulisha wenye kupendezwa jinsi tengenezo linavyofanya kazi, jinsi utendaji mbalimbali hupangwa, na jinsi wanavyoweza kujihusisha. Pitia mambo makuu kutoka kurasa 14 na 15 kwenye makala “Mikutano ya Kuhimizana Ili Kupenda na Kufanya Kazi Nzuri.” Kikundi chafanya wonyesho kifupi jinsi habari hii iwezavyo kutiwa katika mazungumzo kwenye ziara ya kurudia au funzo la Biblia ili kusaidia mtu anayependezwa athamini uhitaji wa kuhudhuria.
Wimbo 126 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Huku sikukuu za kilimwengu na vipindi vya likizo vikikaribia katika Desemba, tia wote moyo wafikirie kujiandikisha wakiwa mapainia wasaidizi.
Dak. 15: Je, Umejaribu Watu Unaorejezewa? Hotuba. Wahubiri fulani wameweza kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia kwa njia hii: Baada ya kujifunza na mtu anayependezwa kwa muda fulani, wao huuliza mtu huyo ikiwa anajua yeyote kati ya marafiki wake, watu wa ukoo, au washiriki wa karibu ambao wanaweza kupendezwa na funzo la Biblia. Mara nyingi majina kadhaa hutolewa. Uliza ikiwa unaweza kutumia jina lake wakati utakapowasiliana na watu hawa. Unapowasiliana nao unaweza kusema hivi: “Fulani amefurahia sana kujifunza Biblia hivi kwamba alifikiri wewe pia ungependa kunufaika kutokana na programu yetu ya funzo la Biblia bila malipo.” Hili laweza kuandaa orodha yenye manufaa ya ziara za kurudia ambazo zaweza kuendelea na kuwa mafunzo ya Biblia yenye matokeo. Tia ndani ono moja au mawili kutoka kwa wahubiri ambao walipata watu wenye kupendezwa au kuanzisha mafunzo mapya kwa njia hii.
Dak. 20: Kutoa New World Translation Pamoja na Kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Wakati wa Novemba. Pitia habari kuu za New World Translation katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 248-251. Soma “Fasili,” ukieleza kwa nini ilitokezwa. Jibu maswali haya: Tafsiri hii ilitegemea nini? Ni nani waliokuwa watafsiri? Je, kweli ni tafsiri iliyofanywa na wanachuo? Kwa nini jina Yehova limetumiwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo? Kisha eleza kwa nini twaweza kuwa wenye shukrani kuwa na tafsiri hii. (Ona kitabu “Kila Andiko,” ukurasa 331, mafungu 22 na 23.) Panga mhubiri mwenye uwezo afanye wonyesho wa utoaji mfupi akitumia maelezo ya utangulizi ya sura ya 14 katika kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? ukurasa 184. Kumbusha wote wachukue nakala za kutumia katika utumishi juma hili.
Wimbo 138 na sala ya kumalizia.