Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 kur. 3-6
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vichapo Vinavyopendekezwa
  • Jinsi ya Kutayarisha
  • Fikiria Mahitaji ya Mwanafunzi
  • Tumia Neno la Mungu Kufundisha
  • Kupiga Mstari Chini ya Majibu na Kuandika Pambizoni
  • Pitio la Kabla na Baada ya Kutayarisha
  • Jenga Imani Thabiti
  • Usikengeushwe
  • Uwe Mwenye Utambuzi
  • Usitoe Maoni Yako
  • Kueleza Sababu za Kutoa Sala
  • Mambo Unayoweza Kutaja Katika Sala
  • Mikutano ya Kutaniko
  • Tumia Video ili Kujenga Uthamini
  • Watie Moyo Watoe Ushahidi
  • Wazoeze Kuwaeleza Wengine Kuhusu Imani Yao
  • Kutayarisha Pamoja
  • Kuhubiri Pamoja
  • Kujitayarisha Kufanya Ziara za Kurudia
  • Kufanya Ziara za Kurudia kwa Bidii
  • Kuanzisha Funzo la Biblia
  • Kuwazoeza Wanafunzi Wawe Walimu
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 9/05 kur. 3-6

Tunza

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Nyongeza hii ina mambo makuu ya mfululizo wa makala za Huduma Yetu ya Ufalme kuhusu jinsi ya kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo. Wote wanatiwa moyo watunze nyongeza hii na kuirejelea wanapoongoza mafunzo ya Biblia. Zaidi ya hayo, ndugu wanaweza kukazia mambo mbalimbali ya nyongeza hii wanapoongoza mikutano ya utumishi wa shambani, nao waangalizi wa utumishi wanaweza kuitumia wanapotayarisha hotuba ambazo wanatoa wanapotembelea vikundi vya funzo la kitabu.

Seh. ya 1: Funzo la Biblia Ni Nini?

Ikiwa unazungumza na mtu kwa ukawaida kuhusu Biblia kwa kutumia Biblia au kichapo fulani kinachopendekezwa, basi unaongoza funzo la Biblia, hata kama mazungumzo hayo ni ya muda mfupi. Funzo linaweza kuripotiwa baada ya kuanzishwa na kuongozwa mara mbili, na ikiwa kuna sababu ya kuamini kwamba funzo hilo litaendelea.—km 7/04 uku. 1.

Vichapo Vinavyopendekezwa

◼ Mungu Anataka Tufanye Nini?

◼ Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele

◼ Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli

◼ Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Broshua hii inaweza kutumiwa kujifunza pamoja na watu wasio na elimu au wale wasiojua kusoma vizuri.

Seh. ya 2: Kujitayarisha Kuongoza Funzo

Tunahitaji kuzungumzia habari kwa njia inayogusa moyo wa mwanafunzi. Ili kufanya hivyo, inatubidi kujitayarisha vizuri na kufikiria mahitaji ya mwanafunzi.—km 8/04 uku. 1.

Jinsi ya Kutayarisha

◼ Chunguza kichwa cha sura au somo, vichwa vidogo, na picha.

◼ Tafuta majibu ya maswali yaliyochapishwa, na upige mstari chini ya maneno muhimu tu.

◼ Chagua maandiko yasiyonukuliwa ambayo mtasoma wakati wa funzo. Andika mambo machache pambizoni mwa kichapo cha funzo.

◼ Tayarisha pitio fupi la mambo makuu.

Fikiria Mahitaji ya Mwanafunzi

◼ Sali kumhusu mwanafunzi na mahitaji yake.

◼ Fikiria mapema mambo ambayo huenda mwanafunzi akaona ni vigumu kuelewa au kukubali.

◼ Fikiria maswali haya: Anahitaji kuelewa nini au kufanya mabadiliko gani ili asonge mbele kiroho? Ninawezaje kuufikia moyo wake?

◼ Inapohitajika, fikiria mfano, au tayarisha maelezo au maswali kadhaa ili kumsaidia mwanafunzi kupata maana ya jambo au andiko fulani.

Seh. ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo

Kusudi letu la kuongoza mafunzo ya Biblia ni ‘kufanya wanafunzi’ kwa kuwasaidia watu waelewe na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu, kisha wayatumie maishani mwao. (Mt. 28:19, 20; 1 The. 2:13) Kwa hiyo, tunapaswa kukazia Maandiko tunapoongoza funzo.—km 11/04 uku. 4.

Tumia Neno la Mungu Kufundisha

◼ Mwonyeshe mwanafunzi jinsi ya kutafuta maandiko hususa katika Biblia yake.

◼ Fungueni na mzungumzie maandiko ya Biblia yanayoonyesha msingi wa imani yetu.

◼ Tumia maswali. Badala ya kufananua maandiko ya Biblia, mwache ayafafanue.

◼ Rahisisha habari. Usijaribu kueleza kila jambo katika andiko. Eleza tu kile kinachohitajika ili mwanafunzi aelewe habari inayozungumziwa.

◼ Onyesha jinsi ya kutumia maandiko. Msaidie mwanafunzi kuona jinsi maandiko ya Biblia yanavyomhusu yeye binafsi.

Seh. ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kutayarisha

Mwanafunzi anayetayarisha somo kabla ya funzo, anayepiga mstari chini ya majibu, na anayefikiria jinsi ya kutoa majibu hayo kwa maneno yake mwenyewe, hufanya maendeleo ya kiroho haraka. Kwa hiyo, baada ya kuanzisha funzo na kuliongoza kwa muda, tayarisha somo fulani pamoja na mwanafunzi ili kumwonyesha jinsi ya kujitayarisha. Mara nyingi inafaa kutayarisha somo au sura nzima pamoja na mwanafunzi.—km 12/04 uku. 1.

Kupiga Mstari Chini ya Majibu na Kuandika Pambizoni

◼ Eleza jinsi ya kupata majibu ya moja kwa moja kwa maswali yaliyochapishwa.

◼ Mwonyeshe mwanafunzi kichapo chako cha funzo ambacho umepiga mstari chini ya maneno au vifungu muhimu pekee.

◼ Msaidie mwanafunzi kutambua kwamba kila andiko lililotajwa bila kunukuliwa linaunga mkono jambo fulani katika fungu, na mwonyeshe jinsi ya kuandika maelezo mafupi kuhusu maandiko pambizoni mwa kichapo cha funzo.

Pitio la Kabla na Baada ya Kutayarisha

◼ Mwonyeshe mwanafunzi jinsi ya kuchunguza kichwa cha sura au somo, vichwa vidogo, na picha kabla hajaanza kutayarisha kwa undani.

◼ Mtie mwanafunzi moyo apitie mambo makuu baada ya kutayarisha somo.

Seh. ya 5: Kuamua Kiasi cha Habari Mtakachozungumzia

Kiasi cha habari mnachoweza kuzungumzia kitategemea uwezo na hali ya mwalimu na mwanafunzi.—km 1/05 uku. 1.

Jenga Imani Thabiti

◼ Kumsaidia mwanafunzi kuelewa vizuri Neno la Mungu ni muhimu kuliko kupitia haraka-haraka habari nyingi mnapojifunza.

◼ Tumia muda wowote ule unaohitajika ili kumsaidia mwanafunzi kuelewa na kukubali yale anayojifunza.

◼ Tumia wakati wa kutosha kuzungumzia maandiko muhimu ambayo ni msingi wa mambo mnayojifunza.

Usikengeushwe

◼ Ikiwa mwanafunzi anapenda sana kuongea juu ya mambo yake, huenda ukahitaji kupanga mzungumzie mambo hayo baada ya funzo.

◼ Usiongee kupita kiasi wakati wa funzo. Usizungumzie sana mambo ya ziada na mambo yaliyoonwa hivi kwamba mwanafunzi anakosa kuelewa kwa usahihi mafundisho ya msingi ya Biblia.

Seh. ya 6: Mwanafunzi Anapouliza Swali

Baada ya kuanzisha funzo la Biblia na kuliongoza kwa muda, kwa kawaida ni afadhali mzungumzie mafundisho ya Biblia kwa utaratibu badala ya kuzungumzia mambo mengi tofauti-tofauti. Jambo hilo humsaidia mwanafunzi kuelewa mafundisho ya msingi kwa usahihi na kufanya maendeleo ya kiroho.—km 2/05 uku. 6.

Uwe Mwenye Utambuzi

◼ Kwa kawaida maswali yanayohusu habari mnayojifunza yanaweza kujibiwa mara moja.

◼ Maswali ambayo hayahusu habari mnayojifunza au yanayohitaji kufanyiwa utafiti yanaweza kujibiwa wakati mwingine. Inafaa kuandika maswali kama hayo.

◼ Ikiwa mwanafunzi ana tatizo la kukubali fundisho fulani, tumia kichapo kingine kinachozungumzia habari hiyo kinaganaga.

◼ Ikiwa mwanafunzi hasadikishwi, liache jambo hilo hadi wakati mwingine na uendelee na funzo.

Usitoe Maoni Yako

◼ Ikiwa hujui jibu la swali fulani, usijaribu kutoa maoni.

◼ Mfundishe hatua kwa hatua jinsi ya kufanya utafiti.

Seh. ya 7: Kutoa Sala Wakati wa Funzo

Baraka za Yehova ni muhimu ili mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. Kwa hiyo inafaa kuanza na kumalizia funzo kwa sala.—km 3/05 uku. 4.

Kueleza Sababu za Kutoa Sala

◼ Unapoanzisha funzo pamoja na wanadini, mara nyingi unaweza kutoa sala hata unapojifunza nao kwa mara ya kwanza.

◼ Lakini tunapowafundisha wanafunzi wengine, tunahitaji kutumia busara ili tutambue wakati unaofaa wa kuanza funzo kwa sala.

◼ Unaweza kutumia Zaburi 25:4, 5 na 1 Yohana 5:14 kuonyesha sababu za kutoa sala.

◼ Andiko la Yohana 15:16 linaweza kutumiwa kuonyesha kwamba tunapaswa kutoa sala kwa Yehova kupitia Yesu Kristo.

Mambo Unayoweza Kutaja Katika Sala

◼ Inafaa kumsifu Yehova kwa sababu yeye ndiye Chanzo cha yale mnayojifunza.

◼ Taja mambo yanayoonyesha kwamba unamjali sana mwanafunzi.

◼ Mshukuru Yehova kwa tengenezo ambalo anatumia.

◼ Mwombe Yehova abariki jitihada za mwanafunzi za kuishi kupatana yale anayojifunza.

Seh. ya 8: Kuwaelekeza Wanafunzi Kwenye Tengenezo

Tunapowafunza wanafunzi wa Biblia, lengo letu si kuwafundisha mambo ya msingi tu, bali pia kuwasaidia wawe sehemu ya kutaniko la Kikristo. Tumia dakika chache kila juma wakati wa funzo kuwaeleza jambo fulani kuhusu tengenezo la Yehova.—km 4/05 uku. 8.

Mikutano ya Kutaniko

◼ Waeleze wanafunzi kuhusu mkutano mmoja-mmoja. Waalike wahudhurie mikutano mara unapoanza kujifunza nao.

◼ Waeleze mambo makuu yaliyozungumziwa kwenye mikutano.

◼ Wasaidie kuthamini Ukumbusho, makusanyiko, na ziara ya mwangalizi wa mzunguko.

◼ Tumia picha katika vichapo vyetu kuwasaidia waelewe mambo yanayofanywa katika pindi hizo.

◼ Watie moyo wasome broshua Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?

Tumia Video ili Kujenga Uthamini

◼ Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name

◼ Our Whole Association of Brothers

◼ United by Divine Teaching

◼ To the Ends of the Earth

Seh. ya 9: Kuwazoeza Wanafunzi Kutoa Ushahidi Isivyo Rasmi

Wanafunzi wa Biblia wanapoanza kuamini yale ambayo wanajifunza, wao husukumwa kusema kuyahusu.—km 5/05 uku. 1.

Watie Moyo Watoe Ushahidi

◼ Je, wana marafiki au watu wa familia ambao wanaweza kuwaalika kwenye funzo?

◼ Je, kuna yeyote kati ya wafanyakazi wenzao, wanafunzi wenzao, au watu wengine wanaofahamiana nao ambaye anapendezwa?

Wazoeze Kuwaeleza Wengine Kuhusu Imani Yao

◼ Mnapozungumzia habari fulani katika funzo mwulize mwanafunzi hivi: “Wewe ungetumiaje Biblia kuwaeleza watu wa familia yenu kweli hii?”

◼ Msaidie mwanafunzi kuelewa umuhimu wa kuonyesha heshima na fadhili anapoongea na wengine kumhusu Mungu na makusudi yake.

◼ Wanafunzi wanaweza kutumia broshua Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? kuwasaidia marafiki wao na watu wa familia yao kuelewa imani yetu na utendaji wetu unaotegemea Biblia.

Seh. ya 10: Kuwazoeza Wanafunzi Katika Huduma ya Nyumba kwa Nyumba

Wazee wanapoamua kwamba mwanafunzi wa Biblia anastahili kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa, mwanafunzi huyo anaweza kuanza kuhubiri pamoja na kutaniko.—km 6/05 uku. 1.

Kutayarisha Pamoja

◼ Mwonyeshe mwanafunzi mahali ambapo anaweza kupata mapendekezo kuhusu mambo ya kusema katika utumishi.

◼ Msaidie kuchagua habari rahisi inayofaa eneo lenu.

◼ Mtie moyo atumie Biblia katika huduma.

◼ Fanyeni mazoezi pamoja. Mwonyeshe jinsi anavyoweza kushughulikia kwa busara maoni ya kawaida ya watu katika eneo lenu.

Kuhubiri Pamoja

◼ Mwache mwanafunzi aone jinsi unavyotumia habari ambayo mlitayarisha pamoja.

◼ Zingatia utu na uwezo wa mwanafunzi. Nyakati nyingine, huenda ikafaa mwanafunzi ashughulikie sehemu tu ya habari mliyotayarisha.

◼ Msaidie mhubiri mpya awe na ratiba ili ashiriki kwa ukawaida katika huduma.

Seh. ya 11: Kuwasaidia Wanafunzi Kufanya Ziara za Kurudia

Mpango wa kufanya ziara ya kurudia hufanywa wakati wa ziara ya kwanza. Mtie mwanafunzi moyo awajali sana wale anaowahubiria. Mzoeze hatua kwa hatua kuwatia moyo wanaopendezwa wajieleze, asikilize maelezo yao, na atambue mambo yanayowahangaisha.—km 7/05 uku. 1.

Kujitayarisha Kufanya Ziara za Kurudia

◼ Pitia habari kuhusu ziara ya kwanza, na umsaidie mwanafunzi kuchagua habari itakayomvutia mwenye nyumba.

◼ Tayarisheni mambo ya kusema yanayotegemea andiko moja la Biblia pamoja na fungu moja katika kichapo kimoja.

◼ Tayarisheni swali mnaloweza kutokeza baada ya mazungumzo.

Kufanya Ziara za Kurudia kwa Bidii

◼ Mtie mwanafunzi moyo awarudie bila kukawia wote wanaopendezwa.

◼ Msaidie mwanafunzi kuona uhitaji wa kurudi tena na tena ili kuwapata watu ambao hawapatikani nyumbani kwa urahisi.

◼ Mwonyeshe mhubiri mpya jinsi ya kupanga ziara za kurudia, na umsaidie kuelewa umuhimu wa kurudi kama alivyoahidi.

Seh. ya 12: Kuwasaidia Wanafunzi Kuanzisha na Kuongoza Mafunzo ya Biblia

Ni muhimu kuiga kielelezo cha Yesu kwa kuwa mfano mzuri katika huduma. Mwanafunzi anapoona mfano wako mzuri katika huduma, atatambua kwamba lengo la kufanya ziara za kurudia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia.—km 8/05 uku. 1.

Kuanzisha Funzo la Biblia

◼ Mweleze mwanafunzi kwamba kwa kawaida si lazima kueleza kwa undani jinsi funzo linavyoongozwa.

◼ Mara nyingi ni afadhali kuonyesha jinsi funzo linavyofanywa kwa kujifunza fungu moja au mawili katika kichapo cha funzo pamoja na mwenye nyumba.

◼ Pitieni pendekezo moja kuhusu jinsi ya kuanzisha mafunzo ya Biblia na mlifanyie mazoezi.—km 8/05 uku. 8; km 1/02 uku. 6.

Kuwazoeza Wanafunzi Wawe Walimu

◼ Watie wanafunzi moyo wajiunge na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

◼ Panga ili wahubiri wapya waandamane nawe kwenye mafunzo mengine ya Biblia ambayo wanaweza kushiriki kidogo kufundisha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki