Mhubiri
4 Nami nikarudi nipate kuona matendo yote ya uonevu+ yanayofanywa chini ya jua, na, tazama! machozi ya wale wanaokandamizwa,+ lakini hawakuwa na mtu wa kuwafariji;+ nao wakandamizaji walikuwa na nguvu, hivi kwamba hawakuwa na mtu wa kuwafariji. 2 Nami nikawapongeza wafu ambao tayari walikuwa wamekufa badala ya wale wanaoishi waliokuwa wangali hai.+ 3 Kwa hiyo aliye afadhali kuliko hao wawili ni yule ambaye hajakuwapo bado,+ ambaye bado hajaona kazi yenye msiba inayofanywa chini ya jua.+
4 Nami nimeona kazi yote ngumu na ustadi wote katika kazi,+ ya kwamba maana yake ni mashindano kati ya mtu na mwenzake;+ hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.
5 Mjinga anakunja mikono+ yake na kula nyama yake mwenyewe.+
6 Konzi moja ya pumziko ni afadhali kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kufuatilia upepo.+
7 Mimi mwenyewe nikarudi nipate kuona ubatili ulio chini ya jua: 8 Kuna mtu mmoja, wala hakuna wa pili;+ naye hana mwana wala ndugu,+ lakini kazi yake ngumu haina mwisho. Pia, macho yake mwenyewe hayatosheki na utajiri:+ “Nami ninamfanyia nani kazi yote hii ngumu na kuinyima nafsi yangu mambo mazuri?”+ Hilo pia ni ubatili, nalo ni shughuli yenye msiba.+
9 Wawili ni afadhali kuliko mmoja,+ kwa maana wana thawabu nzuri kwa ajili ya kazi yao ngumu.+ 10 Kwa maana mmoja wao akianguka, yule mwingine anaweza kumwinua mwenzake.+ Lakini itakuwaje kwa yule aliye peke yake akianguka wakati ambapo hakuna mwingine wa kumwinua?+
11 Tena, wawili wakilala pamoja, watapata joto; lakini aliye peke yake anawezaje kupata joto?+ 12 Na mtu akiweza kumshinda nguvu mmoja aliye peke yake, wawili wakiwa pamoja wataweza kusimama dhidi yake.+ Nayo kamba yenye nyuzi tatu haiwezi kukatika upesi.
13 Mtoto mwenye uhitaji lakini mwenye hekima+ ni afadhali kuliko mfalme mzee lakini mjinga,+ ambaye haoni tena haja ya kukubali onyo.+ 14 Kwa maana ametoka gerezani akawe mfalme,+ ingawa katika ufalme wa huyu alizaliwa akiwa maskini.+ 15 Nimeona wote walio hai wanaotembea chini ya jua, jinsi inavyokuwa kwa mtoto wa pili, anayesimama mahali pa yule mwingine.+ 16 Hakuna mwisho wa watu wote, wote ambao aliwatangulia;+ wala watu baadaye hawatamshangilia,+ kwa maana hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+