2 Petro
Barua ya Pili ya Petro
1 Simoni Petro, mtumwa+ na mtume+ wa Yesu Kristo, kwa wale ambao wamepata imani, yenye pendeleo lililo sawa na letu,+ kupitia uadilifu+ wa Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo:+
2 Na mwongezewe fadhili zisizostahiliwa na amani+ kwa ujuzi sahihi+ juu ya Mungu na juu ya Yesu Bwana wetu, 3 kwa maana nguvu zake za kimungu zimetupa sisi bila malipo mambo yote yanayohusu uzima+ na ujitoaji-kimungu,+ kupitia ujuzi sahihi juu ya yeye ambaye alituita+ kupitia utukufu+ na wema wa adili. 4 Kupitia mambo haya ametupa sisi bila malipo ahadi zenye thamani na zilizo bora sana,+ ili kupitia hizi ninyi muwe washiriki katika asili+ ya kimungu,+ mkiwa mmeponyoka kutoka katika uharibifu ulio katika ulimwengu+ kutokana na uchu.
5 Ndiyo, kwa sababu hii, mkiitikia kwa kuchanga kwenu jitihada yote yenye bidii,+ ongezeni kwenye imani yenu wema wa adili,+ kwenye wema wenu wa adili ujuzi,+ 6 kwenye ujuzi wenu kujizuia, kwenye kujizuia+ kwenu uvumilivu, kwenye uvumilivu wenu ujitoaji-kimungu,+ 7 kwenye ujitoaji-kimungu wenu upendo wa kindugu, kwenye upendo wenu wa kindugu upendo.+ 8 Kwa maana mambo hayo yakikaa ndani yenu na kufurika, yatawazuia kuwa ama wasiotenda au wasiozaa matunda+ kuhusiana na ujuzi sahihi juu ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Kwa maana ikiwa mambo hayo hayapo ndani ya yeyote, yeye ni kipofu, akifunga macho yake yasione nuru,+ naye amesahau+ kutakaswa+ kwake kutoka katika dhambi zake za zamani za kale. 10 Kwa sababu hiyo, akina ndugu, fanyeni hata zaidi yote mnayoweza ili kufanya mwito+ na kuchaguliwa+ kwenu kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe; kwa maana mkiendelea kufanya mambo hayo hamtashindwa hata kidogo.+ 11 Kwa kweli, hivyo ndivyo mtakavyowezeshwa kwa wingi kuingia+ katika ufalme wa milele+ wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.+
12 Kwa sababu hiyo sikuzote nitakuwa na mwelekeo wa kuwakumbusha+ ninyi kuhusu mambo haya, ijapokuwa mnayajua hayo na mmewekwa imara katika kweli+ iliyo ndani yenu.+ 13 Lakini ninaona hili kuwa sawa, maadamu ningali katika maskani hii,+ kuwaamsha ninyi kwa kuwakumbusha,+ 14 nikijua ninavyojua kwamba kuondolewa kwa maskani yangu kutakuwa hivi karibuni,+ kama vile pia Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha.+ 15 Kwa hiyo nitafanya yote ninayoweza pia kila wakati ili, baada ya kuondoka kwangu,+ ninyi mweze kuyataja mambo haya kwa ajili yenu wenyewe.
16 Sivyo, haikuwa kwa kufuata hadithi za uwongo zilizotungwa+ kwa ufundi kwamba tuliwafahamisha ninyi juu ya nguvu na kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo,+ lakini ilikuwa kwa sisi kuwa mashahidi wa kujionea fahari yake.+ 17 Kwa maana alipokea kutoka kwa Mungu Baba heshima na utukufu,+ wakati maneno ya namna hii yalipotolewa kwake kwa utukufu wenye fahari: “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ambaye mimi mwenyewe nimemkubali.”+ 18 Ndiyo, maneno hayo tuliyasikia+ yakitoka mbinguni tulipokuwa tungali pamoja naye katika ule mlima mtakatifu.+
19 Kwa hiyo tuna neno la kinabii+ likiwa limefanywa hakika zaidi;+ nanyi mnafanya vema kulikazia uangalifu kama vile taa+ inayoangaza mahali penye giza, mpaka siku ipambazuke na nyota ya mchana+ ichomoze, katika mioyo yenu. 20 Kwa maana mnajua hili kwanza, kwamba hakuna unabii wa Andiko unaotokana na fasiri yoyote ya kibinafsi.+ 21 Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu,+ bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu+ kama walivyoongozwa na roho takatifu.+