Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 11:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Basi watu wote wakaenda Gilgali, kisha wakamfanya Sauli kuwa mfalme mbele za Yehova katika Gilgali. Ndipo wakatoa huko dhabihu za ushirika mbele za Yehova,+ na Sauli na watu wote wa Israeli wakaendelea kushangilia huko kwa hali ya juu sana.+

  • 1 Samweli 13:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ndipo Samweli akamwambia Sauli: “Umetenda kipumbavu.+ Hukuishika amri+ ya Yehova Mungu wako ambayo alikuamuru,+ kwa sababu, kama ungeishika, Yehova angeufanya ufalme wako juu ya Israeli kuwa imara mpaka wakati usio na kipimo.

  • 1 Samweli 15:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Lakini Samweli akamwambia Sauli: “Sitarudi pamoja nawe, kwa kuwa umelikataa neno la Yehova, naye Yehova amekukataa wewe usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli.”+

  • 1 Samweli 16:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Na ikatukia kwamba wakati roho ya Mungu ilipokuja juu ya Sauli, Daudi alichukua kinubi na kukipiga kwa mkono wake; ndipo Sauli akapata faraja na mambo yakamwendea vema, na ile roho mbaya ikaondoka juu yake.+

  • 1 Samweli 28:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Mwishowe Sauli akawaambia watumishi wake: “Nitafutieni mwanamke ambaye ni stadi wa kuwasiliana na pepo,+ nami nitaenda kwake nitafute shauri kutoka kwake.” Ndipo watumishi wake wakamwambia: “Tazama! Kuna mwanamke katika En-dori ambaye ni stadi wa kuwasiliana na pepo.”+

  • 1 Samweli 31:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake: “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije na kunichoma na kunitendea vibaya.” Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+

  • 2 Samweli 1:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Sauli na Yonathani,+ watu wenye kupendwa na wenye kupendeza wakati wa maisha yao,

      Nao hawakutenganishwa katika kifo chao.+

      Walikuwa wepesi kuliko tai,+

      Walikuwa wenye nguvu kuliko simba.+

  • Matendo 13:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Lakini tangu hapo na kuendelea wakadai mfalme,+ na Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mwanamume wa kabila la Benyamini,+ kwa miaka 40.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki