Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 9:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Na nyumba hii itakuwa marundo ya mabomoko.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ naye atapiga mluzi na kusema, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+

  • 2 Wafalme 25:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Naye akaiteketeza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme+ na nyumba zote za Yerusalemu;+ na nyumba ya kila mtu mkuu akaiteketeza kwa moto.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 7:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na nyumba hii iliyokuwa marundo ya mabomoko,+ kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ na kwa hakika aseme, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Naye akaiteketeza nyumba ya Mungu wa kweli+ na kuubomoa ukuta+ wa Yerusalemu; na minara yake yote ya makao wakaiteketeza kwa moto na pia vyombo vyake vyote vyenye kutamanika,+ ili kufanya uharibifu.+

  • Zaburi 74:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Wao, hata uzao wao, wamesema pamoja moyoni mwao:

      “Mahali pote pa kukutania pa Mungu katika nchi lazima pateketezwe.”+

  • Zaburi 79:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 79 Ee Mungu, mataifa yameingia katika urithi wako;+

      Wamelitia unajisi hekalu lako takatifu;+

      Wamefanya Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+

  • Yeremia 26:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Mika+ wa Moreshethi+ alikuwa akitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda+ naye akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Sayuni utalimwa kama shamba,+ na Yerusalemu litakuwa marundo ya mabomoko,+ na mlima wa ile Nyumba utakuwa kama mahali pa juu pa msitu.”’+

  • Maombolezo 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Yehova ameitupilia mbali madhabahu yake.+ Patakatifu pake amepakataa kwa dharau.+

      Ametia katika mkono wa adui kuta za minara ya makao yake.+

      Wamepaaza sauti zao ndani ya nyumba ya Yehova, kama katika siku ya sherehe.+

  • Ezekieli 24:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 ‘Iambie nyumba ya Israeli: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, mimi ninapatia unajisi patakatifu pangu,+ fahari ya nguvu zenu,+ kitu chenye kutamanika machoni penu+ na kitu ambacho nafsi yenu hukihurumia, nao wana wenu na binti zenu ambao mmewaacha nyuma—wataanguka kwa upanga.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki