Wagalatia
6 Akina ndugu, hata mtu akijikwaa katika kosa+ fulani kabla ya yeye kulijua, ninyi mlio na sifa za kustahili kiroho+ jaribuni kumrekebisha upya mtu huyo katika roho ya upole,+ huku kila mmoja wenu akiendelea kujiangalia,+ ili wewe pia usije ukajaribiwa.+ 2 Endeleeni kubebeana mizigo mizito,+ na hivyo kuitimiza sheria ya Kristo.+ 3 Kwa maana yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu,+ anaidanganya akili yake mwenyewe. 4 Lakini kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini,+ kisha atakuwa na sababu ya kufurahi kwa habari yake mwenyewe peke yake, na si kwa kujilinganisha+ na mtu yule mwingine. 5 Kwa maana kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.+
6 Zaidi ya hayo, mtu yeyote anayefundishwa neno kwa mdomo+ na ashiriki+ katika mambo yote mema pamoja na yule anayetoa fundisho hilo la mdomo.+
7 Msipotoshwe:+ Mungu si wa kudhihakiwa.+ Kwa maana lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia;+ 8 kwa sababu yeye anayepanda kwa mwili wake atavuna uharibifu kutokana na mwili wake,+ lakini yeye anayepanda kwa roho+ atavuna uzima wa milele kutokana na roho.+ 9 Kwa hiyo na tusife moyo katika kufanya yaliyo mema,+ kwa maana katika majira yanayofaa tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.+ 10 Kwa kweli, basi, tukiwa na wakati unaofaa kwa ajili ya hilo,+ tuwatendee wote mema, na hasa wale ambao katika imani ni jamaa zetu.+
11 Oneni kwamba nimewaandikia ninyi kwa herufi kubwa kwa mkono wangu mwenyewe.+
12 Wale wote wanaotaka kuwa na sura ya kupendeza katika mwili ndio wanaojaribu kuwalazimisha ninyi mtahiriwe,+ ili tu wasiteswe kwa ajili ya mti wa mateso wa Kristo,+ Yesu. 13 Kwa maana hata wale wanaotahiriwa wenyewe hawaishiki Sheria,+ lakini wanataka ninyi mtahiriwe ili wawe na sababu ya kujisifu katika mwili wenu. 14 Mimi nisijisifu kamwe, isipokuwa katika mti wa mateso+ wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia yeye ulimwengu umetundikwa mtini+ kwangu na mimi kwa ulimwengu. 15 Kwa maana tohara si kitu wala kutotahiriwa,+ bali kiumbe kipya+ ndicho kitu. 16 Na wale wote watakaotembea kwa utaratibu kwa kanuni hii ya mwenendo, juu yao kuwe na amani na rehema, ndiyo, juu ya Israeli wa Mungu.+
17 Kwa hiyo mtu yeyote asiwe akinitaabisha, kwa maana ninachukua mwilini mwangu alama+ za mtumwa wa Yesu.+
18 Akina ndugu, fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo ziwe pamoja na roho+ ambayo mnaonyesha. Amina.