1 Wakorintho
13 Nikisema kwa lugha+ za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chombo cha shaba nyeupe kinachovuma au toazi+ linalolia. 2 Na ikiwa nina zawadi ya kutoa unabii+ nami nazijua siri takatifu+ zote na ujuzi+ wote, na ikiwa nina imani yote kuweza kuhamisha milima,+ lakini sina upendo, mimi si kitu.+ 3 Nami nikitoa mali zangu zote ili kuwalisha wengine,+ nami nikiutoa mwili wangu,+ ili nijisifu, lakini sina upendo,+ sipati faida hata kidogo.
4 Upendo+ ni wenye ustahimilivu+ na wenye fadhili.+ Upendo hauna wivu,+ haujigambi,+ haujivuni,+ 5 haujiendeshi bila adabu,+ hautafuti faida zake wenyewe,+ hauchokozeki.+ Hauweki hesabu ya ubaya.+ 6 Haushangilii juu ya ukosefu wa uadilifu,+ bali hushangilia pamoja na kweli.+ 7 Huhimili mambo yote,+ huamini mambo yote,+ hutumaini mambo yote,+ huvumilia mambo yote.+
8 Upendo haushindwi kamwe.+ Lakini kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitakoma; kama kuna ujuzi, utaondolewa mbali.+ 9 Kwa maana tuna ujuzi wa sehemu+ tu nasi tunatoa unabii kwa sehemu+ tu; 10 lakini wakati kile kilicho kamili kitakapofika,+ kile kilicho kwa sehemu tu kitaondolewa mbali. 11 Nilipokuwa mtoto, nilikuwa nikisema kama mtoto, nikifikiri kama mtoto, nikiwaza kama mtoto; lakini kwa kuwa sasa nimekuwa mtu mzima,+ nimeziondolea mbali tabia za mtoto. 12 Kwa maana wakati wa sasa tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi kupitia kioo cha chuma,+ lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso.+ Wakati wa sasa najua kwa sehemu tu, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi kama vile ninavyojulikana kwa usahihi.+ 13 Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.+