2 Wakorintho
5 Kwa maana tunajua kwamba nyumba yetu ya kidunia,+ hema+ hili, ikivunjwa,+ tutapata jengo kutoka kwa Mungu, nyumba isiyojengwa kwa mikono,+ ya milele+ mbinguni. 2 Kwa maana tunaugua+ kwelikweli katika nyumba hii ya kukaa, tukitamani kwa bidii kuvaa ile yetu kutoka mbinguni,+ 3 ili kwamba, tukiisha kuivaa kwelikweli, hatutapatikana tukiwa uchi.+ 4 Kwa kweli, sisi tulio katika hema hili tunaugua, tukilemewa; kwa sababu tunataka, si kulivua, bali kuvaa lile lingine,+ ili uhai ukimeze kile kinachoweza kufa.+ 5 Basi yeye aliyetutokeza kwa ajili ya jambo hili ni Mungu,+ aliyetupa sisi rehani+ ya kitakachokuja, yaani, roho.+
6 Kwa hiyo sikuzote sisi tuna uhodari mwingi na tunajua kwamba, tukiwa tungali na makao yetu katika mwili, hatupo mahali alipo Bwana,+ 7 kwa maana tunatembea kwa imani, si kwa kuona.+ 8 Lakini sisi tuna uhodari mwingi na tunapendezwa vema tusiwepo katika mwili na badala yake tufanye makao yetu pamoja na Bwana.+ 9 Kwa hiyo pia tunaifanya iwe shabaha yetu kwamba, kama tuna makao yetu pamoja naye au tukiwa hatupo pamoja naye,+ tuweze kukubalika kwake.+ 10 Kwa maana sisi sote lazima tufunuliwe mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo,+ ili kila mmoja apate thawabu yake kwa ajili ya mambo yaliyofanywa kupitia mwili, kulingana na mambo ambayo ametenda, kama ni mema au ni maovu.+
11 Kwa hiyo, kwa kuwa tunajua kumwogopa+ Bwana, tunaendelea kuwashawishi+ watu, lakini sisi tumefunuliwa kwa Mungu. Hata hivyo, natumaini kwamba tumefunuliwa pia kwa dhamiri+ zenu. 12 Hatujipendekezi+ wenyewe tena kwenu, bali tunawapa ninyi kichocheo cha kujisifu kuhusiana na sisi,+ ili mpate kuwa na jibu la kuwapa wale ambao hujisifu juu ya sura ya nje+ lakini si juu ya moyo.+ 13 Kwa maana ikiwa tulikuwa tumerukwa na akili+ yetu, ilikuwa ni kwa ajili ya Mungu; ikiwa tuna utimamu wa akili,+ ni kwa ajili yenu. 14 Kwa maana upendo alio nao Kristo hutulazimisha, kwa sababu hili ndilo tumehukumu, kwamba mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote;+ kwa hiyo, basi, wote walikuwa wamekufa; 15 naye alikufa kwa ajili ya wote ili wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe,+ bali kwa ajili ya yeye+ aliyekufa kwa ajili yao na kufufuliwa.+
16 Kwa hiyo tangu sasa na kuendelea sisi hatumjui mtu yeyote kulingana na mwili.+ Hata kama tumemjua Kristo kulingana na mwili,+ hakika sasa hatumjui hivyo tena.+ 17 Basi ikiwa yeyote yuko katika muungano na Kristo, yeye ni kiumbe kipya;+ mambo ya zamani yalipitilia mbali,+ tazama! mambo mapya yamekuja kuwako.+ 18 Lakini mambo yote yametoka kwa Mungu, aliyetupatanisha+ sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo na kutupa sisi huduma+ ya upatanisho, 19 yaani, kwamba Mungu kupitia Kristo+ alikuwa akiupatanisha ulimwengu+ kwake mwenyewe,+ bila kuwahesabia makosa+ yao, naye alitukabidhi sisi lile neno+ la upatanisho.+
20 Kwa hiyo sisi+ ni mabalozi+ walio badala ya Kristo,+ kana kwamba Mungu alikuwa akisihi kupitia sisi.+ Kama walio badala ya Kristo tunaomba:+ “Mpatanishwe pamoja na Mungu.” 21 Yeye ambaye hakujua dhambi+ alimfanya kuwa dhambi+ kwa ajili yetu, ili sisi tuwe uadilifu wa Mungu+ kupitia yeye.