Waefeso
6 Enyi watoto, watiini wazazi+ wenu katika muungano+ na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu:+ 2 “Mheshimu baba yako na mama yako”;+ ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi:+ 3 “Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.”+ 4 Nanyi, akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu,+ bali endeleeni kuwalea+ katika nidhamu+ na mwongozo wa akilini+ wa Yehova.
5 Enyi watumwa, watiini wale ambao ni mabwana wenu katika maana ya kimwili,+ kwa kuogopa na kutetemeka+ katika unyoofu wa mioyo yenu, kama vile kwa Kristo, 6 si kwa njia ya utumishi wa macho kama wanavyofanya wale wanaowapendeza wanadamu,+ bali kama watumwa wa Kristo, mkiyafanya mapenzi ya Mungu kwa nafsi yote.+ 7 Iweni watumwa mkiwa na maelekeo mema, kama kwa Yehova,+ wala si kwa wanadamu, 8 kwa maana mnajua kwamba wema wowote ambao huenda kila mmoja akafanya, Yehova atamlipa+ huo, hata kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.+ 9 Pia, enyi mabwana, endeleeni kuwatendea wao mambo hayohayo, na mwache kutisha,+ kwa maana mnajua kwamba Bwana wao na wenu+ pia yuko mbinguni, naye hana ubaguzi+ wowote.
10 Mwishowe, endeleeni kujipatia nguvu+ katika Bwana na katika uwezo+ wa nguvu zake. 11 Vaeni mavazi kamili ya silaha+ kutoka kwa Mungu ili mweze kusimama imara kupinga hila+ za Ibilisi; 12 kwa sababu tuna kushindana mweleka,+ si juu ya damu na mwili, bali juu ya serikali,+ juu ya mamlaka,+ juu ya watawala wa ulimwengu+ wa giza hili, juu ya majeshi ya roho waovu+ katika mahali pa kimbingu. 13 Kwa sababu hiyo chukueni mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu,+ ili mweze kupinga katika ile siku ya uovu, baada ya ninyi kufanya mambo yote kwa ukamili, mweze kusimama imara.+
14 Kwa hiyo, simameni imara, viuno vyenu+ vikiwa vimefungwa kwa ile kweli,+ na mkiwa mmevaa bamba la kifuani la uadilifu,+ 15 na mkiwa mmevaa miguuni+ mwenu viatu vya habari njema ya amani.+ 16 Zaidi ya mambo yote, ichukueni ngao kubwa ya imani,+ ambayo kwa kuitumia mtaweza kuizima mishale yote inayowaka moto ya yule mwovu.+ 17 Pia, ipokeeni kofia ya chuma+ ya wokovu, na upanga+ wa roho,+ yaani, neno la Mungu,+ 18 huku kwa kila namna ya sala+ na dua mkiendeleza sala kila wakati katika roho.+ Na kwa kusudi hilo endeleeni kukaa macho daima na kuomba dua kwa ajili ya watakatifu wote, 19 pia kwa ajili yangu, ili nipewe uwezo wa kusema+ kwa kufungua kinywa changu, kwa uhuru wa kusema+ ili kujulisha siri takatifu ya habari njema,+ 20 ambayo kwa ajili yake ninatenda kama balozi+ aliyefungwa minyororo; ili niweze kusema kuhusiana nayo kwa ujasiri kama ninavyopaswa kusema.+
21 Basi ili ninyi mjue pia juu ya mambo yangu, kuhusu jinsi ninavyoendelea, Tikiko,+ ndugu mpendwa na mhudumu mwaminifu katika Bwana, atawajulisha ninyi kila jambo.+ 22 Ninamtuma kwenu kwa kusudi hilo, ili myajue mambo yetu na ili aifariji mioyo yenu.+
23 Akina ndugu na wawe na amani na upendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 24 Fadhili zisizostahiliwa+ na ziwe pamoja na wale wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.