Ayubu
33 “Hata hivyo, sasa, Ee Ayubu, tafadhali sikia maneno yangu,
Nawe tega sikio kwa maneno yangu yote.
2 Tafadhali, tazama! Lazima nifungue kinywa changu;
Ulimi wangu pamoja na kaakaa+ langu lazima viseme.
5 Ukiweza, nijibu,
Yapange maneno mbele yangu; usimame mahali pako.
7 Tazama! Hofu yoyote kutoka kwangu haitakutisha,
Wala mkazo+ kutoka kwangu hautakuwa mzito juu yako.
8 Ila tu umesema masikioni mwangu,
Nami nikaendelea kusikia sauti ya maneno yako,
Mimi ni safi, wala sina kosa.+
12 Tazama! Katika hayo hukuwa upande wa haki,+ ninakujibu;
Kwa maana Mungu anamzidi mwanadamu anayeweza kufa.+
15 Katika ndoto,+ maono+ ya usiku,
Wakati usingizi mzito unapowashika wanadamu,
Wakati wa kusinzia kitandani.+
16 Ndipo anapofungua sikio la wanadamu,+
Naye hutia muhuri wake kwa kuwasihi wao,
17 Ili kumgeuza mwanadamu kutoka katika tendo lake,+
Na ili afunike kiburi+ kutoka kwa mwanamume.
19 Naye kwa kweli hukaripiwa kwa maumivu kitandani mwake,
Na kugombana kwa mifupa yake huendelea mfululizo.
21 Nyama yake hukonda ikaacha kuonekana,
Na mifupa yake ambayo haikuonekana hakika hutokeza.
23 Ikiwa kuna mjumbe kwa ajili yake,
Msemaji, mmoja kati ya elfu,
Ili kumwambia mwanadamu unyoofu wake,
24 Ndipo anapompa kibali na kusema,
‘Mwachilie ili asishuke chini kuingia shimoni!+
Nimepata fidia!+
26 Yeye atamsihi Mungu ili amfurahie,
Naye ataona uso wake kwa kupaaza sauti kwa shangwe,+
Na Yeye ataurudisha uadilifu Wake kwa mwanadamu anayeweza kufa.
27 Yeye atawaimbia wanadamu na kusema,
‘Nimetenda dhambi;+ na nimepotosha lililo nyoofu,
Nalo hakika halikuwa jambo linalofaa kwangu.
29 Tazama! Mungu hufanya mambo hayo yote,
Mara mbili, mara tatu, kuhusiana na mwanamume,
30 Ili kuigeuza nafsi yake isiingie shimoni,+
Ili atiwe nuru kwa nuru ya wale walio hai.+
31 Kaza uangalifu, Ee Ayubu! Nisikilize mimi!
Nyamaza kimya, nami nitaendelea kusema.
32 Ikiwa kuna maneno yoyote ya kusema, nijibu;
Sema, kwa maana nimependezwa na uadilifu wako.