Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 2
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mambo ya Walawi—Yaliyomo

      • Toleo la nafaka (1-16)

Mambo ya Walawi 2:1

Marejeo

  • +Law 9:17; Hes 15:2-4
  • +Kut 29:1-3; Law 6:14, 15; Hes 7:13

Mambo ya Walawi 2:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ikiwa sehemu ya ukumbusho (uwakilishi) wake.”

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Hes 5:25, 26

Mambo ya Walawi 2:3

Marejeo

  • +Law 7:9, 10
  • +Law 10:12; Hes 18:9

Mambo ya Walawi 2:4

Marejeo

  • +Law 8:26, 28; Hes 6:13, 19

Mambo ya Walawi 2:5

Marejeo

  • +Law 6:20, 21

Mambo ya Walawi 2:6

Marejeo

  • +Hes 28:9

Mambo ya Walawi 2:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ikiwa sehemu ya ukumbusho (uwakilishi) wake.”

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Law 2:2; 5:11, 12
  • +Kut 29:38-41; Hes 28:4-6

Mambo ya Walawi 2:10

Marejeo

  • +Hes 18:9

Mambo ya Walawi 2:11

Marejeo

  • +Law 6:14, 17

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    5/15/2004, kur. 21-22

  • Fahirishi ya Machapisho

    w04 5/15 21-22

Mambo ya Walawi 2:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayotuliza.”

Marejeo

  • +Kut 23:19; Hes 15:20; 2Nya 31:5; Met 3:9

Mambo ya Walawi 2:13

Marejeo

  • +Eze 43:23, 24

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu, uku. 520

    Mnara wa Mlinzi,

    5/15/2004, uku. 22

    8/15/1999, uku. 32

  • Fahirishi ya Machapisho

    w04 5/15 22; w99 8/15 32

Mambo ya Walawi 2:14

Marejeo

  • +Kut 23:16; 34:22; Hes 28:26

Mambo ya Walawi 2:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ikiwa sehemu ya ukumbusho (uwakilishi) wake.”

Marejeo

  • +Law 5:11, 12; 6:14, 15

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

Law. 2:1Law 9:17; Hes 15:2-4
Law. 2:1Kut 29:1-3; Law 6:14, 15; Hes 7:13
Law. 2:2Hes 5:25, 26
Law. 2:3Law 7:9, 10
Law. 2:3Law 10:12; Hes 18:9
Law. 2:4Law 8:26, 28; Hes 6:13, 19
Law. 2:5Law 6:20, 21
Law. 2:6Hes 28:9
Law. 2:9Law 2:2; 5:11, 12
Law. 2:9Kut 29:38-41; Hes 28:4-6
Law. 2:10Hes 18:9
Law. 2:11Law 6:14, 17
Law. 2:12Kut 23:19; Hes 15:20; 2Nya 31:5; Met 3:9
Law. 2:13Eze 43:23, 24
Law. 2:14Kut 23:16; 34:22; Hes 28:26
Law. 2:16Law 5:11, 12; 6:14, 15
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Mambo ya Walawi 2:1-16

Mambo ya Walawi

2 “‘Sasa ikiwa mtu atamtolea Yehova toleo la nafaka,+ ni lazima toleo lake liwe la unga laini, naye anapaswa kumimina mafuta juu yake na kuweka ubani juu yake.+ 2 Kisha atalipeleka kwa wana wa Haruni, makuhani, naye kuhani atachukua mkono mmoja wa unga huo laini, mafuta, pamoja na ubani wake wote, naye atauteketeza ili ufuke moshi ikiwa dhabihu ya kumbukumbu*+ juu ya madhabahu. Ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova. 3 Chochote kinachobaki cha toleo hilo la nafaka kitakuwa cha Haruni na wanawe,+ kitakuwa kitu kitakatifu kabisa+ kutoka kwa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto.

4 “‘Mkitoa nafaka ambayo imeokwa kwenye jiko, inapaswa kuwa ya unga laini, mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyokandwa kwa mafuta, au mikate myembamba isiyo na chachu ambayo imepakwa mafuta.+

5 “‘Mkitoa toleo la nafaka kutoka katika kiokeo,+ inapaswa kuwa ya unga laini usio na chachu, uliokandwa kwa mafuta. 6 Toleo hilo litavunjwa vipandevipande na mafuta yatamiminwa juu yake.+ Ni toleo la nafaka.

7 “‘Mkitoa toleo la nafaka iliyokaangwa kwenye kikaangio, linapaswa kuwa la unga laini uliokandwa kwa mafuta. 8 Mnapaswa kumletea Yehova toleo la nafaka lililotengenezwa kwa vitu hivyo, nalo litapelekwa kwa kuhani ambaye atalipeleka karibu na madhabahu. 9 Naye kuhani atachukua sehemu ya toleo hilo la nafaka ikiwa dhabihu ya kumbukumbu*+ na kuiteketeza juu ya madhabahu ili ifuke moshi. Ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+ 10 Chochote kinachobaki cha toleo hilo la nafaka kitakuwa cha Haruni na wanawe, kitakuwa kitu kitakatifu kabisa kutoka kwa dhabihu za Yehova zinazoteketezwa.+

11 “‘Toleo lolote la nafaka mnalomtolea Yehova halipaswi kutiwa chachu,+ kwa maana hampaswi kuuteketeza unga wowote uliokandwa ulio na chachu au kuiteketeza asali ili ifuke moshi ikiwa toleo la Yehova linalochomwa kwa moto.

12 “‘Mnaweza kumtolea Yehova vitu hivyo vikiwa mazao ya kwanza,+ lakini hampaswi kuvileta kwenye madhabahu vikiwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayopendeza.*

13 “‘Kila toleo la nafaka mnalotoa linapaswa kukolezwa kwa chumvi; na msiruhusu kamwe chumvi ya agano la Mungu wenu ikosekane katika toleo lenu la nafaka. Kila toleo mtakalotoa, mtalitoa pamoja na chumvi.+

14 “‘Mkimtolea Yehova mavuno ya kwanza ya nafaka iliyokomaa yakiwa toleo la nafaka, mnapaswa kutoa masuke mabichi yaliyokaangwa kwa moto, chengachenga za nafaka mbichi iliyopondwa, kuwa toleo la nafaka la mavuno yenu ya kwanza yaliyokomaa.+ 15 Mnapaswa kutia mafuta na ubani juu yake. Ni toleo la nafaka. 16 Kuhani ataiteketeza ikiwa dhabihu ya kumbukumbu*+ ili ifuke moshi, yaani, baadhi ya chengachenga za nafaka pamoja na mafuta na ubani wake wote. Ni dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki