Yeremia
46 Hili ndilo neno la Yehova kwa nabii Yeremia kuhusu mataifa:+ 2 Kuhusu Misri,+ kuhusu jeshi la Farao Neko+ mfalme wa Misri, aliyekuwa kando ya Mto Efrati na aliyeshindwa huko Karkemishi na Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:
4 Wafungeni farasi lijamu na mpande juu yake, enyi wapanda farasi.
Shikeni nafasi zenu na mvae kofia zenu.
Sugueni mikuki na mvae makoti yenu ya vita.
5 ‘Kwa nini ninawaona wameshikwa na hofu?
Wanarudi nyuma, mashujaa wao wamepondwa-pondwa.
Wamekimbia kwa woga, mashujaa wao hawakugeuka.
Kuna hofu kila mahali,’ asema Yehova.
6 ‘Wenye mbio hawawezi kukimbia, na mashujaa hawawezi kuponyoka.
Kule kaskazini, kwenye ukingo wa Mto Efrati,
Wamejikwaa na kuanguka.’+
7 Ni nani huyu anayepanda kama Mto Nile,
Kama mito iliyofurika maji?
8 Misri inakuja kama Mto Nile,+
Kama mito iliyofurika maji,
Nayo inasema, ‘Nitapanda na kuifunika dunia.
Nitaliangamiza jiji na wale wanaokaa humo.’
9 Pandeni, enyi farasi!
Nendeni kiwazimu, enyi magari!
Acheni mashujaa wasonge mbele,
Kushi na Putu, wanaobeba ngao,+
10 “Siku hiyo ni ya Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, siku ya kisasi ya kulipiza kisasi dhidi ya maadui wake. Na upanga utanyafua na kujishibisha na kunywa damu yao mpaka ushibe, kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, ana dhabihu* katika nchi ya kaskazini kando ya Mto Efrati.+
Umezidisha matibabu yako bure tu,
Kwa maana hakuna tiba kwa ajili yako.+
Kwa maana shujaa anajikwaa juu ya shujaa,
Na wote wawili wanaanguka pamoja.”
13 Hili ndilo neno ambalo Yehova alimwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kuishambulia nchi ya Misri:+
14 “Lisemeni katika Misri, litangazeni huko Migdoli.+
Litangazeni huko Nofu* na Tahpanhesi.+
Semeni, ‘Shikeni nafasi zenu na mjitayarishe,
Kwa maana upanga utanyafua pande zote kuwazunguka.
15 Kwa nini watu wako wenye nguvu wamefagiliwa mbali?
Walishindwa kusimama imara,
Kwa maana Yehova amewasukuma na kuwaangusha chini.
16 Wanajikwaa na kuanguka kwa wingi.
Wanaambiana:
“Inukeni! Acheni turudi kwa watu wetu na kwenye nchi yetu
Kwa sababu ya upanga ulio katili.”’
18 ‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi,
‘Ataingia* kama Tabori+ kati ya milima
Na kama Karmeli+ kando ya bahari.
19 Tayarisha mzigo wako kwa ajili ya uhamisho,
Ewe binti unayekaa Misri.
20 Misri ni kama ndama jike anayependeza,
Lakini wadudu wanaouma watamvamia kutoka kaskazini.
21 Hata wanajeshi wake waliokodiwa walio kati yake ni kama ndama waliononeshwa,
Lakini wao pia wamegeuka na kukimbia pamoja.
22 ‘Sauti yake ni kama ya nyoka anayenyiririka,
Kwa maana wanamfuata kwa nguvu, wakiwa na mashoka,
Kama wanaume wanaokata miti.*
23 Wataukata msitu wake,’ asema Yehova, ‘ingawa ulionekana hauwezi kupenywa.
Kwa maana ni wengi sana kuliko nzige, nao hawahesabiki.
24 Hakika binti ya Misri ataaibishwa.
Atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.’+
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Sasa ninamkazia fikira Amoni+ kutoka No,*+ Farao, Misri, miungu yake,+ wafalme wake—naam, Farao na wote wanaomtumaini.’+
26 “‘Nami nitawatia mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua, mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni+ na watumishi wake. Lakini baadaye watu watakaa ndani yake kama zamani,’ asema Yehova.+
Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,
Bila mtu wa kuwaogopesha.+
28 Basi usiogope, mtumishi wangu Yakobo,’ asema Yehova, ‘kwa maana niko pamoja nawe.