Amosi
Amosi
1 Maneno ya Amosi, aliyekuwa kati ya wafugaji wa kondoo kutoka Tekoa,+ ambayo aliona katika maono kuhusu Israeli+ katika siku za Uzia+ mfalme wa Yuda na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya lile tetemeko la nchi.+ 2 Naye akasema:
“Yehova—atanguruma kutoka Sayuni,+ naye atatoa sauti yake kutoka Yerusalemu;+ navyo viwanja vya malisho vya wachungaji vitaomboleza, na kilele cha Karmeli kitakauka.”+
3 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya Damasko,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu wamepura Gileadi+ kwa vifaa vya kupuria vya chuma. 4 Nami nitapeleka moto+ juu ya nyumba ya Hazaeli,+ nao utaiteketeza minara ya makao ya Ben-hadadi.+ 5 Nami nitavunja pingo la Damasko+ na kumkatilia mbali mkaaji kutoka Bikath-aveni, na anayeshika fimbo ya enzi kutoka Beth-edeni; na watu wa Siria wataenda Kiri+ wakiwa wahamishwa,” Yehova amesema.’
6 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya Gaza,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu walilipeleka uhamishoni kundi zima la wahamishwa+ ili kuwatia mkononi mwa Edomu.+ 7 Nami nitapeleka moto kwenye ukuta wa Gaza,+ nao utaiteketeza minara ya makao yake. 8 Nami nitakatilia mbali mkaaji kutoka Ashdodi,+ na anayeshika fimbo ya enzi kutoka Ashkeloni;+ nami nitageuza mkono wangu+ juu ya Ekroni,+ na mabaki ya Wafilisti yataangamia,”+ Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’
9 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Tiro,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu ya kulitia mkononi mwa Edomu kundi zima la wahamishwa, na kwa sababu hawakukumbuka agano la ndugu.+ 10 Nami nitapeleka moto kwenye ukuta wa Tiro, nao utaiteketeza minara ya makao yake.’+
11 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Edomu,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake mwenyewe kwa upanga,+ na kwa sababu aliharibu sifa zake mwenyewe za rehema,+ na hasira yake huendelea kurarua milele, na ghadhabu yake—ameishika daima.+ 12 Nami nitapeleka moto katika Temani,+ nao utaiteketeza minara ya makao ya Bosra.’+
13 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya wana wa Amoni,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia,+ kwa sababu waliwapasua wanawake wenye mimba wa Gileadi, kwa kusudi la kupanua eneo lao wenyewe.+ 14 Nami nitawasha moto kwenye ukuta wa Raba,+ nao utaiteketeza minara ya makao yake, pamoja na sauti ya king’ora siku ya pigano, pamoja na tufani siku ya upepo wa dhoruba.+ 15 Na mfalme wao ataenda uhamishoni, yeye pamoja na wakuu wake,”+ Yehova amesema.’