Hesabu
23 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Nijengee mahali hapa madhabahu saba+ na unitayarishie mahali hapa ng’ombe-dume saba na kondoo-dume saba.” 2 Balaki akafanya mara moja kama vile Balaamu alivyokuwa amesema. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 3 Na Balaamu akamwambia Balaki: “Simama kando ya toleo lako la kuteketezwa,+ nami niende. Labda Yehova atawasiliana nami na kukutana nami.+ Ndipo lolote atakalonionyesha, hakika nitakuambia.” Basi akaenda kwenye kilima kilicho wazi.
4 Mungu alipowasiliana na Balaamu,+ Balaamu akamwambia: “Niliweka madhabahu saba katika mistari, nami nikatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.”+ 5 Basi Yehova akatia neno katika kinywa cha Balaamu+ na kusema: “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.”+ 6 Basi akarudi kwake, na, tazama! yeye na wakuu wote wa Moabu walikuwa wamesimama kando ya toleo lake la kuteketezwa. 7 Kisha akaanza neno lake la kimethali+ na kusema:
“Kutoka Aramu+ Balaki mfalme wa Moabu alijaribu kuniongoza,
Kutoka katika milima ya mashariki:
‘Njoo, mlaani Yakobo kwa ajili yangu.
Naam, njoo, washutumu Israeli.’+
8 Ningewezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani?+
Nami ningewezaje kuwashutumu wale ambao Yehova hajawashutumu?+
9 Kwa maana kutoka juu ya miamba nawaona wao,
Na kutoka vilimani nawatazama wao.
Wakiwa kikundi cha watu wanaendelea kukaa wakiwa wamejitenga,+
Nao hawajihesabu katikati ya mataifa.+
10 Ni nani ambaye amehesabu chembe za mavumbi ya Yakobo+
Na ni nani ambaye amehesabu sehemu ya nne ya Israeli?
Nafsi yangu na ife kifo cha wanyoofu,+
Na mwisho wangu na uwe kama ule wao mwishowe.”+
11 Hapo Balaki akamwambia Balaamu: “Umenitendea nini? Nilikuchukua ili uwalaani adui zangu, na, tazama, umewabariki kwelikweli.”+ 12 Naye akajibu na kusema: “Je, lolote ambalo Yehova ametia katika kinywa changu silo ninalopaswa kuwa mwangalifu kulisema?”+
13 Ndipo Balaki akamwambia: “Njoo, tafadhali, pamoja nami mpaka mahali pengine ambapo unaweza kuwaona. Ila utauona mwisho wao tu, nawe hutawaona+ wote. Nawe uwalaani kwa ajili yangu kutoka huko.”+ 14 Basi akampeleka mpaka uwanja wa Sofimu, mpaka juu ya Pisga,+ na kujenga madhabahu saba na kutoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 15 Kisha akamwambia Balaki: “Simama hapa kando ya toleo lako la kuteketezwa, na mimi nami acha niwasiliane naye pale.” 16 Basi Yehova akawasiliana na Balaamu na kutia neno katika kinywa chake na kusema:+ “Rudi kwa Balaki,+ na hili ndilo utakalosema.” 17 Basi akaja kwake, na, tazama! alikuwa amesimama kando ya toleo lake la kuteketezwa, na wakuu wa Moabu pamoja naye. Ndipo Balaki akamwambia: “Yehova amesema nini?” 18 Basi akaanza neno lake la kimethali na kusema:+
“Ondoka, Balaki, usikilize.
Tega sikio kwangu, Ee mwana wa Sipori.+
19 Mungu si mwanadamu kwamba aseme uwongo,+
Wala si mwana wa binadamu kwamba ajute.+
Je, yeye mwenyewe amelisema naye hatalitenda,
Na je, yeye amesema naye hatalitimiza?+
21 Hajatazama nguvu zozote za uchawi+ juu ya Yakobo,
Wala hajaona taabu yoyote juu ya Israeli.
Yehova Mungu wake yuko pamoja naye,+
Na sauti ya mfalme iko katikati yake.
23 Kwa maana hakuna apizo lolote la bahati mbaya juu ya Yakobo,+
Wala uaguzi wowote juu ya Israeli.+
Na wakati huu inaweza kusemwa juu ya Yakobo na Israeli,
‘Mungu ametenda nini!’+
24 Tazama, kikundi cha watu kitasimama kama simba,
Na kama simba kitajiinua.+
Hakitalala chini mpaka kile mawindo,
Na damu ya waliouawa kitakunywa.”+
25 Hapo Balaki akamwambia Balaamu: “Ikiwa, kwa upande mmoja, huwezi kumlaani hata kidogo, basi, kwa upande mwingine, hupaswi kumbariki hata kidogo.” 26 Naye Balaamu akajibu na kumwambia Balaki: “Je, sikusema nawe, na kukuambia, ‘Yote ambayo Yehova atasema ndiyo nitakayotenda’?”+
27 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Njoo, tafadhali. Acha nikupeleke mahali pengine tena. Labda itakuwa sawa machoni pa Mungu wa kweli ili upate kuwalaani kwa ajili yangu kutoka huko.”+ 28 Kwa hiyo Balaki akamchukua Balaamu mpaka juu ya Peori, unaoelekea Yeshimoni.+ 29 Kisha Balaamu+ akamwambia Balaki: “Nijengee mahali hapa madhabahu saba na unitayarishie mahali hapa ng’ombe-dume saba na kondoo-dume saba.”+ 30 Basi Balaki akafanya kama vile Balaamu alivyokuwa amesema, naye akatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja kwenye kila madhabahu.+