Waroma
15 Ingawa hivyo, sisi tulio na nguvu tunapaswa kuchukua udhaifu wa wale wasio na nguvu,+ na tusiwe tukijipendeza wenyewe.+ 2 Kila mmoja wetu na ampendeze jirani yake katika yaliyo mema kwa ajili ya kujengwa kwake.+ 3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe;+ bali kama ilivyoandikwa: “Shutuma za wale waliokuwa wanakushutumu zimeniangukia.”+ 4 Kwa maana mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa+ ili kutufundisha+ sisi, ili kupitia uvumilivu+ wetu na kupitia faraja+ kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.+ 5 Sasa Mungu anayetoa uvumilivu na faraja na awawezeshe ninyi kati yenu wenyewe kuwa na mtazamo uleule wa akili+ ambao Kristo Yesu alikuwa nao, 6 ili kwa umoja+ na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo.
7 Kwa hiyo mkaribishane,+ kama vile Kristo pia alivyotukaribisha sisi,+ kwa kusudi la kumpa Mungu utukufu. 8 Kwa maana nasema kwamba kwa kweli Kristo alikuwa mhudumu+ wa wale waliotahiriwa+ kwa ajili ya ukweli+ wa Mungu, ili kuthibitisha ahadi+ ambazo Yeye aliwapa mababu zao, 9 na kwamba mataifa+ yamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema+ yake. Kama ilivyoandikwa: “Ndiyo sababu nitakukiri wewe waziwazi kati ya mataifa nami nitalipigia jina lako muziki.”+ 10 Naye anasema tena: “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake.”+ 11 Na tena: “Msifuni Yehova, enyi mataifa yote, na vikundi vyote vya watu vimsifu yeye.”+ 12 Na tena Isaya anasema: “Patakuwa na mzizi wa Yese,+ na patakuwa na mmoja ambaye atasimama ili kutawala mataifa;+ na mataifa yatamtumainia yeye.”+ 13 Mungu anayetoa tumaini na awajaze ninyi shangwe yote na amani kwa kuamini kwenu, ili mzidi katika tumaini kwa nguvu za roho takatifu.+
14 Sasa mimi mwenyewe pia ninasadikishwa juu yenu, ndugu zangu, kwamba ninyi wenyewe mmejaa wema pia, kwa kuwa mmejawa na ujuzi+ wote, na kwamba mnaweza pia kuonyana.+ 15 Hata hivyo, ninawaandikia ninyi kwa kusema waziwazi zaidi juu ya mambo fulani, kana kwamba ninawakumbusha+ ninyi tena, kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa nilizopewa kutoka kwa Mungu+ 16 ili niwe mtumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa,+ nikifanya kazi takatifu ya habari njema+ ya Mungu, ili toleo,+ yaani, mataifa haya, likubalike,+ likiwa limetakaswa kwa roho takatifu.+
17 Kwa hiyo nina sababu ya kufurahi katika Kristo Yesu+ kwa habari ya mambo yanayohusiana na Mungu.+ 18 Kwa maana sitathubutu kusema jambo moja ikiwa hilo si kati ya mambo yale ambayo Kristo alifanya kupitia mimi+ ili mataifa yawe yenye utiifu,+ kwa njia ya neno+ na tendo langu, 19 kwa nguvu za ishara na mambo ya ajabu,+ kwa nguvu za roho takatifu; hivi kwamba kutoka Yerusalemu na kuzunguka+ mpaka Ilirikamu nimehubiri kikamili habari njema juu ya Kristo.+ 20 Kwa kweli, katika njia hii, nilikusudia kwamba nisitangaze habari njema mahali ambapo Kristo tayari alikuwa amekwisha kutajwa jina, ili nisiwe nikijenga juu ya msingi wa mtu mwingine;+ 21 bali, kama ilivyoandikwa: “Wale ambao hawajatangaziwa juu yake wataona, na wale ambao hawajasikia wataelewa.”+
22 Kwa hiyo pia nilizuiwa mara nyingi nisiwafikie ninyi.+ 23 Lakini sasa kwa kuwa sina tena eneo lisiloguswa katika maeneo haya, na kwa miaka kadhaa nikiwa nimetamani kuwafikia ninyi+ 24 wakati nitakapokuwa nimeenda Uhispania,+ natumaini, zaidi ya yote, nitakapokuwa safarini kwenda huko, niwaangalie ninyi kidogo nanyi mnisindikize+ kidogo kwenda huko baada ya mimi kutosheka kwa kiasi fulani na ushirika wenu. 25 Lakini sasa nakaribia kusafiri kwenda Yerusalemu ili kuwahudumia watakatifu.+ 26 Kwa maana wale walio katika Makedonia na Akaya+ wamependezwa kushiriki vitu vyao kwa kuwatolea mchango+ fulani walio maskini kati ya watakatifu katika Yerusalemu. 27 Kweli, wamependezwa kufanya hivyo, na bado walikuwa wadeni kwao; kwa maana ikiwa mataifa wameshiriki mambo yao ya kiroho,+ wao pia wana deni la kuwahudumia hadharani kwa vitu ambavyo ni kwa ajili ya mwili.+ 28 Kwa sababu hiyo nikiisha kumaliza hili na kuwafikishia salama tunda+ hili, nitaondoka nikipitia kwenu kwenda Uhispania.+ 29 Zaidi ya hayo, najua kwamba nitakapokuja kwenu nitakuja nikiwa na kipimo kamili cha baraka kutoka kwa Kristo.+
30 Sasa nawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia Bwana wetu Yesu Kristo na kupitia upendo wa roho,+ kwamba mjikaze pamoja nami katika sala kwa Mungu kwa ajili yangu,+ 31 ili nikombolewe+ kutoka kwa wale wasioamini katika Yudea na kwamba huduma yangu ambayo ni kwa ajili ya Yerusalemu+ ikubalike kwa watakatifu,+ 32 ili nitakapofika kwenu nikiwa na shangwe kwa mapenzi ya Mungu niburudishwe+ pamoja nanyi. 33 Mungu anayetoa amani na awe pamoja nanyi nyote.+ Amina.