2 Wakorintho
10 Basi mimi mwenyewe, Paulo, nawasihi ninyi kwa upole+ na fadhili+ za Kristo, ingawa kuonekana kwangu+ katikati yenu ni kwa hali ya chini, lakini nisipokuwapo mimi ni jasiri kuwaelekea ninyi.+ 2 Kwa kweli naomba kwamba, nitakapokuwapo, nisitumie ujasiri kwa uhakika ule ambao nategemea kuchukua hatua za kijasiri+ juu ya wengine ambao wanatukadiria sisi kana kwamba tulitembea kulingana na tulivyo katika mwili. 3 Kwa maana ingawa tunatembea katika mwili,+ hatupigi vita kulingana na tulivyo katika mwili.+ 4 Kwa maana silaha za vita vyetu si za kimwili,+ bali ni zenye nguvu kwa Mungu+ kwa ajili ya kupindua ngome zenye nguvu. 5 Kwa maana sisi tunapindua mawazo na kila jambo lililo juu sana ambalo limeinuliwa kinyume cha ujuzi wa Mungu;+ nasi tunaiteka kila fikira ili kuifanya imtii Kristo; 6 nasi tuko tayari kutoa adhabu kwa ajili ya kila kitu kisichotii,+ mara tu utii wenu wenyewe utakapokuwa umeisha kutimizwa kikamilifu.+
7 Mnayatazama mambo kulingana na thamani yake ya juujuu.+ Mtu yeyote akijitegemea mwenyewe kwamba ni wa Kristo, acheni yeye atie akilini tena jambo hili kwa ajili yake mwenyewe, kwamba, kama vile yeye alivyo wa Kristo, ndivyo na sisi pia.+ 8 Kwa maana hata nikijisifu+ mno kidogo juu ya mamlaka ambayo Bwana alitupa sisi ili tuwajenge wala si kuwabomoa ninyi,+ mimi sitaaibishwa, 9 ili nisionekane kuwa nataka kuwatia ninyi hofu kwa barua zangu. 10 Kwa maana, wao husema: “Barua zake ni nzito na zenye nguvu nyingi, lakini kuwapo kwake mwenyewe kimwili ni dhaifu+ na maneno yake ni yenye kudharaulika.”+ 11 Mtu wa namna hiyo na atie jambo hili akilini, kwamba kile tulicho katika neno letu kwa barua wakati hatupo, ndivyo tutakavyokuwa pia katika tendo tutakapokuwapo.+ 12 Kwa maana sisi hatuthubutu kujiweka katika kikundi cha watu fulani au kujilinganisha na watu fulani ambao hujipendekeza wenyewe.+ Hakika wao kwa kujipima wenyewe kwa wenyewe na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, hawana uelewaji.+
13 Kwa upande wetu sisi tutajisifu, si nje ya mipaka yetu tuliyogawiwa,+ bali kulingana na mpaka wa eneo ambalo Mungu alitugawia kwa kipimio, akilifanya lifike hadi kwenu.+ 14 Kwa kweli sisi hatujinyooshi wenyewe kupita kiasi kana kwamba hatukuwafikia ninyi, kwa maana sisi tulikuwa wa kwanza kuja hadi kwenu katika kutangaza habari njema juu ya Kristo.+ 15 Hapana, hatujisifu katika kazi za jasho za mtu mwingine nje ya mipaka yetu tuliyogawiwa,+ bali tunatumainia kwamba, kadiri imani yenu inavyoongezwa,+ ndivyo sisi tutakavyofanywa wakubwa katikati yenu kuhusiana na eneo letu.+ Ndipo tutakapozidi hata zaidi, 16 kutangaza habari njema kwenye nchi zilizo ng’ambo yenu,+ ili tusijisifu katika eneo la mtu mwingine ambapo mambo yamekwisha kutayarishwa. 17 “Bali yeye anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”+ 18 Kwa maana yule anayejipendekeza si ndiye ambaye hukubaliwa,+ bali ni yule mtu ambaye Yehova+ humpendekeza.+