115 Sisi hatuna chochote, Ee Yehova, sisi hatuna chochote,+
Bali jina lako ulitukuze+
Kulingana na fadhili zako zenye upendo, kulingana na ukweli wako.+
2 Kwa nini mataifa yaseme:+
“Yuko wapi, sasa, Mungu wao?”+
3 Lakini Mungu wetu yuko mbinguni;+
Kila kitu ambacho alipendezwa kufanya, amekifanya.+
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,+
Kazi ya mikono ya mtu wa udongo.+
5 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona;+
6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia.+
Zina pua, lakini haziwezi kunusa.+
7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa.+
Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoi sauti yoyote kwa koo zao.+
8 Wale wanaozifanya watakuwa kama hizo,+
Wale wote wanaozitegemea.+
9 Ee Israeli, mtegemeeni Yehova;+
Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+
10 Ee nyumba ya Haruni, mtegemeeni Yehova;+
Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+
11 Ninyi mnaomwogopa Yehova, mtegemeeni Yehova;+
Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+
12 Yehova mwenyewe ametukumbuka; atatoa baraka,+
Ataibariki nyumba ya Israeli,+
Ataibariki nyumba ya Haruni.+
13 Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,+
Wadogo kwa wakubwa.+
14 Yehova atawapa ninyi ongezeko,+
Ninyi na wana wenu.+
15 Ninyi ndio mliobarikiwa na Yehova,+
Mtengenezaji wa mbingu na dunia.+
16 Mbingu ni mbingu za Yehova,+
Bali dunia amewapa wana wa binadamu.+
17 Wafu wenyewe hawamsifu Yah,+
Wala wowote wanaoingia mahali penye kimya.+
18 Lakini sisi wenyewe tutambariki Yah+
Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+
Msifuni Yah!+