97 Yehova amekuwa mfalme!+ Dunia na ishangilie.+
Na vile visiwa vingi vishangilie.+
2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+
Uadilifu na hukumu ni mahali palipofanywa imara pa kiti chake cha ufalme.+
3 Moto hutoka mbele zake,+
Nao huteketeza adui zake wanaomzunguka pande zote.+
4 Umeme wake ulitia nuru nchi yenye kuzaa;+
Dunia iliona, ikawa na maumivu makali.+
5 Milima ilianza kuyeyuka kama nta kwa sababu ya Yehova,+
Kwa sababu ya Bwana wa dunia nzima.+
6 Mbingu zimeutangaza uadilifu wake,+
Navyo vikundi vyote vya watu vimeuona utukufu wake.+
7 Wote wanaotumikia sanamu yoyote ya kuchongwa na waone aibu,+
Wale wanaojisifia miungu isiyo na thamani.+
Mwinamieni, enyi miungu yote.+
8 Sayuni ilisikia na kuanza kushangilia,+
Na miji ya kandokando ya Yuda ilianza kushangilia+
Kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu, Ee Yehova.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;+
Wewe uko juu sana katika kupanda kwako, juu ya miungu mingine yote.+
10 Enyi mnaompenda Yehova,+ chukieni yaliyo mabaya.+
Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake;+
Huwakomboa kutoka katika mkono wa waovu.+
11 Nuru imemwangazia mwadilifu,+
Na shangwe kwa ajili ya walio wanyoofu moyoni.+
12 Shangilieni katika Yehova, enyi waadilifu,+
Na kutoa shukrani kwa ukumbusho wake mtakatifu.+