1 Wathesalonike
5 Sasa kwa habari ya nyakati na majira,+ akina ndugu, hamhitaji kuandikiwa kitu. 2 Kwa maana ninyi wenyewe mnajua vema kabisa kwamba siku ya Yehova+ inakuja sawasawa kabisa kama mwizi usiku.+ 3 Wakati watakapokuwa wakisema:+ “Amani+ na usalama!” ndipo uharibifu+ wa ghafula utakapokuwa juu yao mara moja kama vile maumivu ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba;+ nao hawataponyoka hata kidogo.+ 4 Lakini ninyi, akina ndugu, hamko gizani,+ hivi kwamba siku hiyo iwafikie ninyi kama vile ambavyo ingewafikia wezi,+ 5 kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru+ na wana wa mchana.+ Sisi si wa usiku wala si wa giza.+
6 Kwa hiyo, basi, na tusiendelee kulala usingizi+ kama wengine,+ bali na tukae macho+ na kutunza akili zetu.+ 7 Kwa maana wale wanaolala usingizi+ wana desturi ya kulala usingizi usiku,+ na kwa kawaida wale wanaolewa, hulewa usiku. 8 Lakini kwa habari yetu sisi tulio wa mchana, na tutunze akili zetu na kuvaa bamba la kifuani+ la imani+ na upendo na lile tumaini la wokovu+ kama kofia ya chuma;+ 9 kwa sababu Mungu hakutuweka sisi tupate ghadhabu,+ bali tujipatie wokovu+ kupitia Bwana wetu Yesu Kristo.+ 10 Yeye alikufa kwa ajili yetu,+ ili, kama tunakaa macho au kama tumelala usingizi, tuishi pamoja naye.+ 11 Kwa hiyo endeleeni kufarijiana na kujengana,+ kama vile mnavyofanya.+
12 Sasa tunawaomba ninyi, akina ndugu, mwatilie maanani wale wanaofanya kazi kwa bidii kati yenu na kuwasimamia+ ninyi katika Bwana na kuwaonya ninyi; 13 na kuwafikiria kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.+ Iweni wenye kufanya amani mtu na mwenzake.+ 14 Kwa upande mwingine, tunawahimiza ninyi, akina ndugu, mwaonye wale wasio na utaratibu,+ semeni kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika,+ tegemezeni walio dhaifu, iweni wenye ustahimilivu+ kuelekea wote. 15 Angalieni kwamba mtu asimlipe mwingine yeyote ubaya kwa ubaya,+ bali sikuzote fuatilieni yaliyo mema kuelekea mtu na mwenzake na kwa wengine wote.+
16 Shangilieni sikuzote.+ 17 Salini bila kuacha.+ 18 Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.+ Kwa maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu katika muungano na Kristo Yesu kwa habari yenu. 19 Msiuzime moto wa roho.+ 20 Msiyatendee kwa dharau maneno ya unabii.+ 21 Hakikisheni mambo yote;+ shikeni sana yaliyo mazuri.+ 22 Jiepusheni na kila namna ya uovu.+
23 Yule Mungu wa amani+ na awatakase ninyi kikamilifu.+ Na vikiwa timamu katika kila jambo, roho na nafsi na mwili wenu akina ndugu na vihifadhiwe kwa namna isiyo na lawama wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 24 Yeye anayewaita ninyi ni mwaminifu, naye atafanya hilo pia.
25 Akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu.+
26 Mwasalimu ndugu wote kwa busu takatifu.+
27 Nawaweka ninyi chini ya wajibu mzito kwa Bwana ili barua hii isomewe ndugu wote.+
28 Fadhili zisizostahiliwa+ za Bwana wetu Yesu Kristo na ziwe pamoja nanyi.