Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 22:16-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kwa maana mbwa wananizunguka;+

      Wananizingira kama kundi la watenda maovu,+

      Kama simba, wanaishambulia mikono yangu na miguu yangu.+

      17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+

      Wananitazama na kunikodolea macho.

      18 Wanagawana mavazi yangu,

      Nao wanalipigia kura vazi langu.+

  • Isaya 53:1-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 53 Ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+

      Na mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+

       2 Atapanda kama tawi+ mbele yake,* kama mzizi kutoka katika nchi iliyokauka.

      Hana umbo la kifahari, wala utukufu wowote;+

      Na tunapomwona, sura yake haituvutii.*

       3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+

      Mtu aliyekusudiwa kupata* maumivu na aliyezoea magonjwa.

      Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu.*

      Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.+

       4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyabeba magonjwa yetu,+

      Na kujitwika maumivu yetu.+

      Lakini tulimwona kama mtu aliyepata mapigo, aliyepigwa na Mungu na kuteswa.

       5 Lakini alichomwa*+ kwa sababu ya makosa yetu;+

      Alipondwa kwa sababu ya dhambi zetu.+

      Aliibeba adhabu ili tupate amani,+

      Na kwa sababu ya majeraha yake tuliponywa.+

       6 Sisi sote tumetangatanga kama kondoo,+

      Kila mmoja ameifuata njia yake mwenyewe,

      Na Yehova amefanya dhambi yetu sote ikutane naye.+

       7 Alikandamizwa+ na alikubali kuteswa,+

      Lakini hakuthubutu kufungua kinywa chake.

      Aliletwa kama kondoo machinjioni,+

      Kama kondoo jike aliye kimya mbele ya wanaomkata manyoya,

      Na hakuthubutu kufungua kinywa chake.+

       8 Kwa sababu ya kizuizi* na hukumu alichukuliwa;

      Na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?*

      Kwa maana aliondolewa katika nchi ya walio hai;+

      Alipata pigo* kwa sababu ya makosa ya watu wangu.+

       9 Naye alipewa kaburi* pamoja na waovu,+

      Na pamoja na matajiri* katika kifo chake,+

      Ingawa hakuwa amefanya kosa*

      Na hakukuwa na udanganyifu kinywani mwake.+

      10 Lakini yalikuwa mapenzi ya Yehova* kumponda, naye aliruhusu awe mgonjwa.

      Ukitoa uhai wake* uwe dhabihu ya hatia,+

      Atauona uzao wake,* ataongeza siku zake,+

      Na kupitia kwake mapenzi* ya Yehova yatafanikiwa.+

      11 Kwa sababu ya mateso* yake, ataona na kuridhika.

      Kupitia ujuzi wake, yule mwadilifu, mtumishi wangu,+

      Atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu,+

      Na dhambi zao atazibeba.+

      12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu kati ya wengi,

      Naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,

      Kwa sababu aliumwaga uhai wake* mpaka kifo+

      Naye alihesabiwa miongoni mwa wakosaji;+

      Aliibeba dhambi ya watu wengi,+

      Naye aliwatetea wakosaji.+

  • Danieli 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Na baada ya hayo majuma 62, Masihi atauawa,*+ hatabaki na chochote.+

      “Na watu wa kiongozi anayekuja wataliharibu jiji na mahali patakatifu.+ Na mwisho wake utakuwa kwa mafuriko. Na mpaka ule mwisho kutakuwa na vita; kilichoamuliwa ni ukiwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki