-
Isaya 53:1-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
53 Ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+
Na mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+
2 Atapanda kama tawi+ mbele yake,* kama mzizi kutoka katika nchi iliyokauka.
Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu.*
Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.+
Lakini tulimwona kama mtu aliyepata mapigo, aliyepigwa na Mungu na kuteswa.
6 Sisi sote tumetangatanga kama kondoo,+
Kila mmoja ameifuata njia yake mwenyewe,
Na Yehova amefanya dhambi yetu sote ikutane naye.+
Aliletwa kama kondoo machinjioni,+
Kama kondoo jike aliye kimya mbele ya wanaomkata manyoya,
Na hakuthubutu kufungua kinywa chake.+
8 Kwa sababu ya kizuizi* na hukumu alichukuliwa;
Na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?*
9 Naye alipewa kaburi* pamoja na waovu,+
Na pamoja na matajiri* katika kifo chake,+
Ingawa hakuwa amefanya kosa*
Na hakukuwa na udanganyifu kinywani mwake.+
10 Lakini yalikuwa mapenzi ya Yehova* kumponda, naye aliruhusu awe mgonjwa.
-