36 Na ikawa kwamba wakati+ wa kutolewa kwa toleo la nafaka, Eliya nabii akaanza kukaribia na kusema: “Ee Yehova Mungu wa Abrahamu,+ Isaka+ na Israeli,+ leo na ijulikane kwamba wewe ni Mungu katika Israeli+ na mimi ni mtumishi wako na ni kwa neno+ lako nimefanya mambo haya yote.
8 Ndipo Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akalifunga, akapiga maji, nayo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba wote wawili wakavuka juu ya nchi kavu.+
11 Na ikawa kwamba walipokuwa wanatembea, wakizungumza huku wakitembea, tazama! gari+ la vita lenye moto na farasi wenye moto, nao wakawatenganisha hao wawili; na Eliya akaanza kupanda katika ile dhoruba ya upepo kuelekea mbinguni.+
12 Mwishowe maandishi+ yakaja kwake kutoka kwa Eliya+ nabii, na kusema: “Yehova Mungu wa Daudi babu yako, amesema hivi, ‘Kwa sababu hukutembea katika njia za Yehoshafati+ baba yako wala katika njia za Asa+ mfalme wa Yuda,
17 Pia, atakwenda mbele zake kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo+ ya akina baba kwa watoto na wale wasiotii kwenye hekima inayotumika ya waadilifu, ili kuweka tayari kwa ajili ya Yehova+ watu waliotayarishwa.”+