Tito
Kwa Tito
1 Paulo, mtumwa+ wa Mungu na mtume+ wa Yesu Kristo kulingana na imani ya waliochaguliwa+ wa Mungu na ujuzi sahihi+ wa ile kweli+ ambayo inapatana na ujitoaji-kimungu+ 2 juu ya msingi wa tumaini la uzima wa milele+ ambao Mungu, asiyeweza kusema uwongo,+ aliahidi nyakati za zamani za kale,+ 3 lakini katika nyakati zake mwenyewe zinazofaa alifanya neno lake liwe wazi katika kazi ya kuhubiri ambayo nilikabidhiwa,+ chini ya amri ya Mwokozi wetu,+ Mungu; 4 kwa Tito, mtoto wangu+ kwelikweli kulingana na imani inayoshirikiwa kwa pamoja:
Na kuwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba+ na Kristo Yesu Mwokozi wetu.+
5 Kwa sababu hii nilikuacha wewe Krete,+ ili uyarekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro na uweke rasmi+ wanaume wazee katika jiji baada ya jiji, kama nilivyokupa maagizo;+ 6 ikiwa kuna mwanamume yeyote asiye na shtaka,+ mume wa mke mmoja,+ mwenye watoto wanaoamini ambao hawako chini ya shtaka la kuwa wapotovu wala la kuwa watundu.+ 7 Kwa maana mwangalizi lazima awe bila shtaka+ kama msimamizi-nyumba+ wa Mungu, asiwe mshupavu,+ asiwe mwepesi wa ghadhabu,+ asiwe mlevi mwenye fujo,+ asiwe mwenye kupiga watu,+ asiwe mwenye pupa ya pato lisilo la haki,+ 8 bali awe mkaribishaji-wageni,+ mpenda-wema, mwenye utimamu wa akili,+ mwadilifu, mshikamanifu,+ mwenye kujizuia,+ 9 akilishika imara neno la uaminifu kuhusiana na ufundi wake wa kufundisha,+ ili aweze kuhimiza kwa fundisho lenye afya+ na pia kuwakaripia+ wale ambao hulipinga.
10 Kwa maana kuna watu wengi watundu, wanaoongea maneno yasiyo na faida,+ na wanaodanganya akili za watu, hasa watu wale ambao hushikamana na tohara.+ 11 Ni jambo la lazima kuvifunga vinywa vya watu hao, kwa kuwa watu hao wanaendelea kuharibu nyumba nzima-nzima+ kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha, ili kupata pato lisilo la haki.+ 12 Mtu fulani kati yao, nabii wao wenyewe, alisema: “Wakrete ni waongo sikuzote, wanyama-mwitu wenye kudhuru,+ walafi wasiofanya kazi.”
13 Ushahidi huu ni kweli. Kwa sababu hiyo endelea kuwakaripia kwa ukali,+ ili wawe na afya+ katika imani, 14 bila kusikiliza hadithi zisizo za kweli za Kiyahudi+ na amri za watu+ ambao hugeuka na kuiacha kweli.+ 15 Vitu vyote ni safi kwa watu safi.+ Lakini kwa watu waliotiwa unajisi+ na wasio na imani+ hakuna kitu chochote kilicho safi, bali akili zao na pia dhamiri+ zao zimetiwa unajisi. 16 Wao hutangaza hadharani kwamba wanamjua Mungu,+ lakini humkana kwa matendo yao,+ kwa sababu ni wenye kuchukiza na wasiotii nao si wenye kukubalika+ kwa ajili ya kazi njema ya namna yoyote.