1 Petro
4 Kwa hiyo kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili,+ ninyi pia jivikeni silaha ya mwelekeo uleule wa akili;+ kwa sababu mtu ambaye ameteseka katika mwili ameachana na dhambi,+ 2 kwa kusudi kwamba aishi wakati wake uliobaki katika mwili,+ si kwa ajili ya tamaa za wanadamu tena, bali kwa ajili ya mapenzi ya Mungu.+ 3 Kwa maana wakati+ uliopita uliwatosha kufanya mapenzi ya mataifa+ wakati mlipotembea katika vitendo vya mwenendo mpotovu,+ uchu, divai kupita kiasi,+ karamu za kupindukia, mashindano ya kunywa, na ibada haramu za sanamu.+ 4 Kwa sababu ninyi hamwendelei kukimbia pamoja nao katika mwendo huo kwenda kwenye dimbwi lilelile la chini la upotovu,+ wao wanashangaa na kuendelea kuwatukana ninyi.+ 5 Lakini watu hao watatoa hesabu kwake yeye+ aliye tayari kuhukumu wale walio hai na wale walio wafu.+ 6 Kwa kweli, kwa kusudi hili habari njema ilitangazwa kwa wafu+ pia, ili wahukumiwe kuhusiana na mwili kwa maoni ya wanadamu+ lakini waishi kuhusiana na roho+ kwa maoni ya Mungu.
7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia.+ Kwa hiyo, iweni na utimamu wa akili,+ na kukesha kuhusiana na sala.+ 8 Zaidi ya mambo yote, iweni na upendo mkubwa ninyi kwa ninyi,+ kwa sababu upendo hufunika dhambi nyingi.+ 9 Mkaribishane bila kunung’unika.+ 10 Kwa kadiri ambayo kila mmoja amepokea zawadi, itumieni katika kuhudumiana kama wasimamizi-nyumba wazuri wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu zinazoonyeshwa kwa njia mbalimbali.+ 11 Kama yeyote akisema, na aseme kana kwamba ni maneno matakatifu+ ya Mungu; kama yeyote akihudumu,+ na ahudumu kama anayetegemea nguvu ambazo Mungu hutoa;+ ili katika mambo yote Mungu atukuzwe+ kupitia Yesu Kristo. Utukufu+ na nguvu ni zake milele na milele. Amina.
12 Wapendwa, msishangazwe juu ya moto unaowaka katikati yenu, unaowapata ninyi ili kuwa jaribu,+ kana kwamba jambo geni linawapata. 13 Kinyume chake, endeleeni kushangilia+ kwa maana ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo,+ ili mshangilie na kuwa na shangwe sana pia wakati wa ufunuo+ wa utukufu wake. 14 Ikiwa mnashutumiwa kwa ajili ya jina la Kristo,+ ninyi ni wenye furaha,+ kwa sababu ile roho ya utukufu, yaani roho ya Mungu, inatulia juu yenu.+
15 Hata hivyo, yeyote kati yenu asiteseke+ kwa sababu yeye ni muuaji au mwizi au mtenda-maovu au mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.+ 16 Lakini akiteseka+ kwa sababu yeye ni Mkristo, asione aibu,+ bali na aendelee kumtukuza Mungu katika jina hili. 17 Kwa maana ni wakati uliowekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu.+ Sasa ikiwa inaanza na sisi kwanza,+ basi mwisho wa wale wasioitii habari njema ya Mungu utakuwaje?+ 18 “Na ikiwa mtu mwadilifu anaokolewa kwa shida,+ mtu asiyemwogopa Mungu na mtenda-dhambi wataonekana wapi?”+ 19 Kwa hiyo, basi, acheni wale wanaoteseka kwa kupatana na mapenzi ya Mungu waendelee kuzikabidhi nafsi zao kwa Muumba mwaminifu wanapotenda mema.+