2 Timotheo
3 Lakini ujue jambo hili, ya kwamba katika siku za mwisho+ kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.+ 2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi,+ wasio na shukrani, wasio washikamanifu,+ 3 wasio na upendo wa asili,+ wasiotaka makubaliano yoyote,+ wachongezi,+ wasiojizuia, wakali,+ wasiopenda wema,+ 4 wasaliti,+ wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi,+ wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu+ 5 wakiwa na namna ya ujitoaji-kimungu+ lakini wakizikana nguvu zake;+ nawe geukia mbali kutoka kwa hao.+ 6 Kwa maana kutoka kwa watu hao huinuka wale watu wanaojiingiza kwa ujanja katika nyumba+ na kuwachukua mateka wanawake walio dhaifu ambao wamelemewa na mizigo ya dhambi, wanaoongozwa na tamaa za namna mbalimbali,+ 7 wakijifunza sikuzote na bado hawawezi kamwe kufikia ujuzi sahihi juu ya kweli.+
8 Basi katika njia ambayo Yane na Yambre+ walimpinga Musa, vivyo hivyo hawa pia wanaendelea kuipinga kweli,+ watu walioharibika kabisa akilini,+ waliokataliwa kwa habari ya imani.+ 9 Hata hivyo, hawatafanya maendeleo zaidi, kwa maana wazimu wao utakuwa wazi kwa wote, kama vile ulivyokuwa ule wazimu wa watu hao wawili.+ 10 Lakini wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha,+ kusudi langu, imani yangu, ustahimilivu wangu, upendo wangu, uvumilivu wangu, 11 mateso yangu, masumbufu yangu, namna ya mambo yaliyonipata katika Antiokia,+ katika Ikoniamu,+ katika Listra,+ namna ya mateso ambayo nimevumilia; na bado Bwana alinikomboa mimi kutoka katika hayo yote.+ 12 Kwa kweli, wote wanaotamani kuishi kwa ujitoaji-kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watateswa pia.+ 13 Lakini watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.+
14 Hata hivyo, wewe endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini,+ ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo+ 15 na kwamba tangu utoto mchanga+ umeyajua maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu+ kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.+ 16 Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu+ nalo ni lenye faida kwa kufundisha,+ kwa kukaripia,+ kwa kunyoosha mambo,+ kwa kutia nidhamu+ katika uadilifu, 17 ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili,+ akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.+