91 Yeyote anayekaa mahali pa siri+ pa Aliye Juu Zaidi+
Atajipatia makao katika kivuli cha Mweza-Yote.+
2 Nitamwambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+
Mungu wangu, ambaye nitamtegemea.”+
3 Kwa maana yeye mwenyewe atakukomboa kutoka katika mtego wa mwindaji wa ndege,+
Kutoka kwa tauni inayosababisha shida.+
4 Kwa manyoya yake ataweka kizuizi usiweze kufikiwa,+
Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+
Ukweli+ wake utakuwa ngao+ kubwa na boma.
5 Hutaogopa kitu chochote chenye kutia hofu wakati wa usiku,+
Wala mshale+ unaoruka mchana,
6 Wala tauni inayotembea gizani,+
Wala maangamizi yanayopora katikati ya mchana.+
7 Elfu wataanguka upande wako
Na elfu kumi kwenye mkono wako wa kuume;
Haitakukaribia wewe.+
8 Utatazama kwa macho yako tu+
Na kuona malipo ya waovu.+
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”+
Umemfanya Aliye Juu Zaidi awe makao yako;+
10 Hakuna msiba utakaokuangukia,+
Na hata pigo halitakaribia hema lako.+
11 Kwa maana atawaamuru malaika zake kukuhusu wewe,+
Ili kukulinda katika njia zako zote.+
12 Watakuchukua mikononi mwao,+
Ili usiugonge mguu wako juu ya jiwe lolote.+
13 Utamkanyaga mwana-simba na swila;+
Utamkanyagia chini mwana-simba mwenye manyoya shingoni na nyoka mkubwa.+
14 Kwa sababu ameweka upendo wake juu yangu,+
Mimi nitamwokoa pia.+
Nitamlinda kwa sababu amelijua jina langu.+
15 Ataniitia, nami nitamjibu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamwokoa na kumtukuza.+
16 Nitamshibisha kwa wingi wa siku,+
Nami nitamfanya aone wokovu wangu.+