Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 11
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Wafalme—Yaliyomo

      • Wake za Sulemani waugeuza moyo wake (1-13)

      • Wapinzani wa Sulemani (14-25)

      • Yeroboamu aahidiwa makabila kumi (26-40)

      • Sulemani afa; Rehoboamu awekwa kuwa mfalme (41-43)

1 Wafalme 11:1

Marejeo

  • +1Fa 3:1
  • +Kum 17:15, 17; Ne 13:26
  • +Mwa 19:36, 37
  • +1Fa 14:21
  • +1Fa 16:30, 31
  • +Mwa 26:34, 35

1 Wafalme 11:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Hampaswi kuoana nao.”

Marejeo

  • +Kut 34:16; Kum 7:3; Yos 23:12, 13; 2Ko 6:14

1 Wafalme 11:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wake zake wakawa na uvutano mkubwa kwake.”

1 Wafalme 11:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “waliupotosha.”

  • *

    Au “haukumtumikia kikamili.”

Marejeo

  • +1Fa 11:42
  • +Kum 7:3, 4; Ne 13:26

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    7/1/2005, uku. 29

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 7/1 29

1 Wafalme 11:5

Marejeo

  • +Amu 2:11, 13; 10:6; 1Sa 7:3
  • +Sef 1:5

1 Wafalme 11:6

Marejeo

  • +1Fa 15:5

1 Wafalme 11:7

Marejeo

  • +Law 26:30; Hes 33:52; 2Fa 21:1, 3
  • +Law 18:21; Mdo 7:43
  • +2Fa 23:13

1 Wafalme 11:9

Marejeo

  • +Kum 7:3, 4; Met 4:23
  • +1Fa 3:5; 9:2

1 Wafalme 11:10

Marejeo

  • +2Nya 7:19, 20

1 Wafalme 11:11

Marejeo

  • +2Fa 17:21

1 Wafalme 11:12

Marejeo

  • +2Nya 10:18, 19

1 Wafalme 11:13

Marejeo

  • +2Sa 7:12, 15
  • +1Fa 12:20; 2Nya 11:1
  • +Kum 12:11

1 Wafalme 11:14

Marejeo

  • +2Sa 7:12, 14
  • +Mwa 27:40

1 Wafalme 11:15

Marejeo

  • +2Sa 8:13

1 Wafalme 11:18

Marejeo

  • +Hes 10:12

1 Wafalme 11:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Hakuwa malkia aliyetawala.

1 Wafalme 11:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “alimwachisha kunyonya.”

1 Wafalme 11:21

Marejeo

  • +1Fa 2:10
  • +1Fa 2:34

1 Wafalme 11:23

Marejeo

  • +1Fa 11:14
  • +2Sa 8:3

1 Wafalme 11:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “alipowaua.”

Marejeo

  • +2Sa 10:18
  • +2Sa 8:5; 1Fa 19:15; Isa 7:8

1 Wafalme 11:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuinua mkono wake dhidi ya.”

Marejeo

  • +1Fa 11:31; 12:32; 14:10; 2Nya 11:14; 13:3, 20
  • +1Fa 9:22
  • +2Nya 13:6

1 Wafalme 11:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Milo.” Neno la Kiebrania linalomaanisha “jaza.”

Marejeo

  • +1Fa 9:15, 24
  • +2Sa 5:7

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, kur. 2025-2026

1 Wafalme 11:28

Marejeo

  • +1Fa 5:16

1 Wafalme 11:29

Marejeo

  • +1Fa 12:15; 14:2; 2Nya 9:29

1 Wafalme 11:31

Marejeo

  • +1Fa 12:16

1 Wafalme 11:32

Marejeo

  • +1Fa 12:20; 2Nya 11:1
  • +Mwa 49:10
  • +Kum 12:5, 6; 1Fa 11:13; Zb 132:13

1 Wafalme 11:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu.”

Marejeo

  • +Kum 28:15; 2Nya 15:2

1 Wafalme 11:34

Marejeo

  • +1Fa 9:4, 5; Zb 89:49; 132:17; Isa 9:7

1 Wafalme 11:35

Marejeo

  • +1Fa 12:20; 2Nya 10:16

1 Wafalme 11:36

Marejeo

  • +2Sa 7:29; 1Fa 15:4; 2Fa 8:19

1 Wafalme 11:37

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ambacho nafsi yako inatamani.”

1 Wafalme 11:38

Marejeo

  • +1Fa 15:5
  • +2Sa 7:11

1 Wafalme 11:39

Marejeo

  • +1Fa 12:16
  • +Mwa 49:10; Isa 11:1; Lu 1:32, 33

1 Wafalme 11:40

Marejeo

  • +1Fa 14:25
  • +2Nya 10:2

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    7/1/2005, uku. 30

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 7/1 30

1 Wafalme 11:41

Marejeo

  • +2Nya 9:29-31

1 Wafalme 11:42

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” kur. 284-285

1 Wafalme 11:43

Marejeo

  • +1Nya 3:10; 2Nya 13:7; Mt 1:7

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    7/15/2005, uku. 31

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 7/15 31

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Fal. 11:11Fa 3:1
1 Fal. 11:1Kum 17:15, 17; Ne 13:26
1 Fal. 11:1Mwa 19:36, 37
1 Fal. 11:11Fa 14:21
1 Fal. 11:11Fa 16:30, 31
1 Fal. 11:1Mwa 26:34, 35
1 Fal. 11:2Kut 34:16; Kum 7:3; Yos 23:12, 13; 2Ko 6:14
1 Fal. 11:41Fa 11:42
1 Fal. 11:4Kum 7:3, 4; Ne 13:26
1 Fal. 11:5Amu 2:11, 13; 10:6; 1Sa 7:3
1 Fal. 11:5Sef 1:5
1 Fal. 11:61Fa 15:5
1 Fal. 11:7Law 26:30; Hes 33:52; 2Fa 21:1, 3
1 Fal. 11:7Law 18:21; Mdo 7:43
1 Fal. 11:72Fa 23:13
1 Fal. 11:9Kum 7:3, 4; Met 4:23
1 Fal. 11:91Fa 3:5; 9:2
1 Fal. 11:102Nya 7:19, 20
1 Fal. 11:112Fa 17:21
1 Fal. 11:122Nya 10:18, 19
1 Fal. 11:132Sa 7:12, 15
1 Fal. 11:131Fa 12:20; 2Nya 11:1
1 Fal. 11:13Kum 12:11
1 Fal. 11:142Sa 7:12, 14
1 Fal. 11:14Mwa 27:40
1 Fal. 11:152Sa 8:13
1 Fal. 11:18Hes 10:12
1 Fal. 11:211Fa 2:10
1 Fal. 11:211Fa 2:34
1 Fal. 11:231Fa 11:14
1 Fal. 11:232Sa 8:3
1 Fal. 11:242Sa 10:18
1 Fal. 11:242Sa 8:5; 1Fa 19:15; Isa 7:8
1 Fal. 11:261Fa 11:31; 12:32; 14:10; 2Nya 11:14; 13:3, 20
1 Fal. 11:261Fa 9:22
1 Fal. 11:262Nya 13:6
1 Fal. 11:271Fa 9:15, 24
1 Fal. 11:272Sa 5:7
1 Fal. 11:281Fa 5:16
1 Fal. 11:291Fa 12:15; 14:2; 2Nya 9:29
1 Fal. 11:311Fa 12:16
1 Fal. 11:321Fa 12:20; 2Nya 11:1
1 Fal. 11:32Mwa 49:10
1 Fal. 11:32Kum 12:5, 6; 1Fa 11:13; Zb 132:13
1 Fal. 11:33Kum 28:15; 2Nya 15:2
1 Fal. 11:341Fa 9:4, 5; Zb 89:49; 132:17; Isa 9:7
1 Fal. 11:351Fa 12:20; 2Nya 10:16
1 Fal. 11:362Sa 7:29; 1Fa 15:4; 2Fa 8:19
1 Fal. 11:381Fa 15:5
1 Fal. 11:382Sa 7:11
1 Fal. 11:391Fa 12:16
1 Fal. 11:39Mwa 49:10; Isa 11:1; Lu 1:32, 33
1 Fal. 11:401Fa 14:25
1 Fal. 11:402Nya 10:2
1 Fal. 11:412Nya 9:29-31
1 Fal. 11:431Nya 3:10; 2Nya 13:7; Mt 1:7
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Wafalme 11:1-43

Kitabu cha Kwanza cha Wafalme

11 Lakini mbali na binti ya Farao,+ Mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni:+ wanawake Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu, Wasidoni,+ na Wahiti.+ 2 Walitoka katika mataifa ambayo Yehova alikuwa amewaambia hivi Waisraeli kuyahusu: “Hampaswi kuingia miongoni mwao,* nao hawapaswi kuingia miongoni mwenu; kwa maana kwa hakika wataigeuza mioyo yenu ifuate miungu yao.”+ Lakini Sulemani alishikamana nao na kuwapenda. 3 Naye alikuwa na wake 700 waliokuwa mabinti wa wafalme na masuria 300, na hatua kwa hatua wake zake wakaugeuza moyo wake.* 4 Sulemani alipozeeka,+ wake zake waliugeuza* moyo wake ukaifuata miungu mingine,+ na moyo wake haukuwa kamili kwa* Yehova Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake. 5 Na Sulemani akamfuata Ashtorethi,+ mungu wa kike wa Wasidoni, na Milkomu,+ mungu mwenye kuchukiza wa Waamoni. 6 Na Sulemani akatenda maovu machoni pa Yehova, naye hakumfuata Yehova kikamili kama Daudi baba yake alivyomfuata.+

7 Wakati huo ndipo Sulemani alipojenga mahali pa juu+ kwa ajili ya Kemoshi, mungu mwenye kuchukiza wa Moabu, kwenye mlima uliokuwa mbele ya Yerusalemu, na kwa ajili ya Moleki,+ mungu mwenye kuchukiza wa Waamoni.+ 8 Hivyo ndivyo alivyowafanyia wake zake wote wa kigeni waliokuwa wakifukiza moshi wa dhabihu na kuitolea dhabihu miungu yao.

9 Yehova akamkasirikia vikali Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umegeuka na kumwacha Yehova Mungu wa Israeli,+ aliyekuwa amemtokea mara mbili+ 10 na kumwonya kuhusu jambo hilohilo, kwamba hapaswi kuifuata miungu mingine.+ Lakini hakutii amri ya Yehova. 11 Sasa Yehova akamwambia Sulemani: “Kwa sababu umefanya jambo hili, nawe hukushika agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, kwa hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako, nami nitampa mmoja wa watumishi wako.+ 12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya hivyo maishani mwako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwana wako,+ 13 lakini sitaurarua ufalme wote.+ Kabila moja nitampa mwana wako,+ kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, jiji ambalo nimechagua.”+

14 Ndipo Yehova akatokeza mtu wa kumpinga Sulemani,+ yaani, Hadadi Mwedomu, wa ukoo wa kifalme wa Edomu.+ 15 Daudi aliposhinda Edomu,+ Yoabu mkuu wa jeshi alipanda kwenda kuwazika waliouawa, naye akajaribu kumuua kila mwanamume huko Edomu. 16 (Kwa maana Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita mpaka alipokuwa amemwangamiza kila mwanamume huko Edomu.) 17 Lakini Hadadi alikimbia pamoja na baadhi ya Waedomu waliokuwa watumishi wa baba yake, wakaenda Misri; wakati huo Hadadi alikuwa mvulana mdogo. 18 Basi wakaondoka Midiani na kufika Parani. Walichukua wanaume kutoka Parani+ na kwenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa nyumba, akaamuru awe akipewa chakula, na pia akampa ardhi. 19 Hadadi alipata kibali machoni pa Farao, hivi kwamba akampa dada ya mke wake mwenyewe, dada ya malkia Tapenesi,* ili amwoe. 20 Baada ya muda dada ya Tapenesi akamzalia mwana, Genubathi, na Tapenesi alimlelea* katika nyumba ya Farao; Genubathi aliendelea kukaa katika nyumba ya Farao miongoni mwa wana wa Farao.

21 Hadadi akasikia akiwa Misri kwamba Daudi alikuwa amekufa na kuzikwa pamoja na mababu zake+ na kwamba Yoabu mkuu wa jeshi alikuwa amekufa.+ Basi Hadadi akamwambia Farao: “Niruhusu niende zangu, niende katika ardhi yangu mwenyewe.” 22 Lakini Farao akamuuliza: “Ni nini ulichokosa kwangu hivi kwamba unataka kwenda katika ardhi yako mwenyewe?” Hadadi akamjibu: “Sijakosa chochote, lakini tafadhali niruhusu niende zangu.”

23 Mungu akatokeza pia mtu mwingine wa kumpinga Sulemani,+ yaani, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amemkimbia bwana wake, Hadadezeri+ mfalme wa Soba. 24 Alijikusanyia wanaume akawa kiongozi wa kundi la wavamizi wakati Daudi alipowashinda.*+ Basi wakaenda Damasko,+ wakakaa huko na kuanza kutawala huko Damasko. 25 Naye akawa mpinzani wa Waisraeli siku zote za Sulemani, kuongezea madhara yaliyosababishwa na Hadadi, naye aliwachukia sana Waisraeli alipokuwa akitawala Siria.

26 Pia kulikuwa na Yeroboamu+ mwana wa Nebati, Mwefraimu kutoka Sereda, mtumishi wa Sulemani,+ na mama yake aliyekuwa mjane aliitwa Serua. Yeye pia alianza kumwasi* mfalme.+ 27 Hii ndiyo sababu iliyomfanya amwasi mfalme: Sulemani alikuwa amejenga Kilima*+ na kuziba mwanya katika ukuta wa Jiji la Daudi baba yake.+ 28 Sasa huyu Yeroboamu alikuwa mwanamume mwenye uwezo mkubwa. Sulemani alipoona kwamba kijana huyo alikuwa mfanyakazi mwenye bidii, alimweka kuwa msimamizi+ wa utumishi wote wa lazima wa nyumba ya Yosefu. 29 Wakati huo Yeroboamu alitoka Yerusalemu, na nabii Ahiya,+ Mshilo, akamkuta njiani. Ahiya alikuwa amevaa nguo mpya, na wote wawili walikuwa peke yao shambani. 30 Ahiya akashika nguo mpya aliyokuwa amevaa na kuirarua vipande 12. 31 Kisha akamwambia Yeroboamu:

“Jichukulie vipande kumi, kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mikononi mwa Sulemani, nami nitakupa makabila kumi.+ 32 Lakini atabaki na kabila moja+ kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi+ na kwa ajili ya Yerusalemu, jiji ambalo nimechagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli.+ 33 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha,+ nao wanamwinamia Ashtorethi, mungu wa kike wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu wa Moabu, na Milkomu, mungu wa Waamoni, nao hawajatembea katika njia zangu kwa kufanya yaliyo sawa machoni pangu na kushika maagizo yangu na sheria zangu* kama Daudi baba yake alivyofanya. 34 Lakini sitauchukua ufalme wote kutoka mikononi mwake, nami nitamwacha aendelee kuwa mkuu sikuzote za maisha yake, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu niliyemchagua,+ kwa sababu alitii amri zangu na sheria zangu. 35 Lakini nitauchukua ufalme kutoka mikononi mwa mwana wake na kukupa wewe, yaani, makabila kumi.+ 36 Nitampa mwana wake kabila moja, ili sikuzote Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu Yerusalemu,+ jiji ambalo nimejichagulia liwe mahali pa kuweka jina langu. 37 Nitakuchukua wewe, nawe utatawala kila kitu unachotamani,* nawe utakuwa mfalme wa Israeli. 38 Na ikiwa utatii mambo yote ninayokuamuru na kutembea katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu kwa kutii sheria zangu na amri zangu, kama Daudi mtumishi wangu alivyofanya,+ nitakuwa pia pamoja nawe. Nitakujengea nyumba inayodumu, kama nilivyomjengea Daudi,+ nami nitakupa Israeli. 39 Nami nitauaibisha uzao wa Daudi kwa sababu ya jambo hili,+ lakini sitafanya hivyo sikuzote.’”+

40 Basi Sulemani akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki+ wa Misri,+ akaendelea kukaa Misri mpaka Sulemani alipokufa.

41 Na mambo mengine katika historia ya Sulemani, mambo yote aliyofanya na hekima yake, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya Sulemani?+ 42 Sulemani alitawala nchi yote ya Israeli kwa miaka 40 akiwa Yerusalemu. 43 Kisha Sulemani akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi baba yake; na Rehoboamu+ mwanawe akawa mfalme baada yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki