Ayubu
38 Naye Yehova akaanza kumjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo,+ akasema:
2 “Ni nani huyu anayefunika shauri
Kwa maneno yasiyo na ujuzi?+
5 Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,
Au ni nani aliyenyoosha juu yake kamba ya kupimia?
6 Vikalio+ vyake vimeingizwa ndani ya nini,
Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,
7 Nyota za asubuhi+ zilipopiga vigelegele pamoja kwa shangwe,
Na wana wote wa Mungu+ wakaanza kupaaza sauti kwa kushangilia?
8 Na ni nani aliyeizuia bahari kwa milango,+
Iliyoanza kwenda kama katika wakati ilipotoka katika tumbo la uzazi;
9 Nilipoliweka wingu liwe vazi lake
Na giza zito liwe utepe wake wa kufungia,
10 Nami nikaweka sharti langu juu yake
Na kuweka pingo na milango,+
11 Nami nikasema, ‘Unaweza kufika hapa, na usipite;+
Na hapa mawimbi yako yenye fahari yamewekewa mpaka’?+
12 Je, uliiamuru asubuhi+ tangu siku zako na kuendelea?
Je, uliyajulisha mapambazuko mahali pake,
13 Yapate kushika miisho ya dunia,
Ili waovu wakung’utwe kutoka ndani yake?+
16 Je, umeingia katika chemchemi za bahari,
Au, je, umetembea huku na huku+ ukitafuta kilindi cha maji?+
19 Basi sasa, iko wapi njia inayoenda mahali ambapo nuru hukaa?+
Sasa nalo giza, mahali pake ni wapi,
20 Ili ulipeleke kwenye mpaka wake
Na ili uzielewe barabara zinazoenda katika nyumba yake?
21 Je, umepata kujua kwa sababu wakati huo ulikuwa ukizaliwa,+
Na kwa sababu hesabu ya siku zako ni nyingi?
24 Basi sasa, iko wapi njia ambayo katika hiyo nuru hujigawanya,
Na ambayo upepo wa mashariki+ hutawanyika huku na huku juu ya dunia?
25 Ni nani ameugawanya mfereji kwa ajili ya mafuriko
Na njia kwa ajili ya wingu la dhoruba lenye kunguruma,+
26 Ili kulifanya linyeshe juu ya nchi isiyokuwa na mwanadamu,+
Juu ya nyika isiyokuwa na mtu wa udongo,
27 Ili kushibisha maeneo yenye kupigwa na dhoruba na yenye ukiwa
Na kusababisha majani kuchipuka?+
31 Je, unaweza kufunga vifungo vya kundi-nyota la Kima,
Au, je, unaweza kufungua kamba za kundi-nyota la Kesili?+
32 Je, unaweza kuleta kundi-nyota la Mazarothi katika wakati wake uliowekwa?
Na kwa habari ya kundi-nyota la Ashi, je, unaweza kuliongoza pamoja na wanawe?
35 Je, unaweza kuutuma umeme ili uende
Na kukuambia, ‘Sisi tupo hapa!’?
36 Ni nani aliyetia hekima+ katika tabaka za mawingu,
Au ni nani aliyeyapa uelewaji+ maajabu ya angani?
37 Ni nani anayeweza kuhesabu kwa ukamili mawingu kwa hekima,
Au mitungi ya maji ya mbingu—ni nani anayeweza kuipindua,+
38 Wakati mavumbi yanapomwagika kana kwamba ni fungu lililoyeyushwa,
Na madonge ya udongo kushikamana?