Ezekieli
7 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Na wewe, Ee Mwana wa binadamu, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia nchi ya Israeli, ‘Mwisho, ule mwisho, umekuja juu ya miisho minne ya nchi.+ 3 Sasa mwisho uko juu yako,+ nami nitaipeleka hasira yangu juu yako, nami nitakuhukumu kulingana na njia zako+ na kuleta juu yako machukizo yako yote. 4 Na jicho langu halitakusikitikia, wala sitakuwa na huruma,+ kwa maana juu yako nitazileta njia zako mwenyewe, na katikati yako machukizo yako mwenyewe yatakuja kuwamo;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+
5 “Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Msiba, msiba wa pekee, tazama! unakuja.+ 6 Mwisho wenyewe lazima uje.+ Lazima ule mwisho uje; lazima huo uamke kwa ajili yako. Tazama! Unakuja.+ 7 Lazima shada likujie wewe, Ee mkaaji wa nchi, wakati utakuja, siku ile iko karibu.+ Kuna mvurugo, wala si kupaaza sauti kwa milima.
8 “ ‘Hivi karibuni nitaimwaga ghadhabu yangu juu yako,+ nami nitaitimiza hasira yangu juu yako,+ nami nitakuhukumu kulingana na njia zako+ na kuleta juu yako machukizo yako yote. 9 Jicho langu halitasikitika+ wala sitakuonea huruma.+ Kulingana na njia zako nitaleta juu yako, na machukizo yako mwenyewe yatakuja kuwa katikati yako;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova ninayewapiga.+
10 “ ‘Tazama! Ile siku! Tazama! Inakuja.+ Shada limetoka.+ Fimbo imechanua.+ Kimbelembele kimechipuka.+ 11 Jeuri yenyewe imesimama na kuwa fimbo ya uovu.+ Si kutoka kwao, wala kutoka kwa mali yao; na si kutoka kwao wenyewe, wala hamna ukuu wowote ndani yao. 12 Lazima wakati uje, siku ile lazima ifike. Mnunuzi na ashangilie;+ naye muuzaji asianze kuomboleza, kwa maana kuna hasira juu ya umati wake wote. 13 Kwa maana kwa kile kilichouzwa muuzaji mwenyewe hatakirudia, uhai wao ukiwa bado katikati ya walio hai; kwa maana maono ni ya umati wake wote. Hakuna atakayerudi, na kila mmoja wao hatakuwa na uhai wake mwenyewe kupitia kwa kosa lake mwenyewe.
14 “ ‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mtu ametayarishwa, lakini hakuna anayeenda kwenye pigano, kwa sababu hasira yangu iko juu ya umati wake wote.+ 15 Upanga+ uko nje, na tauni na njaa zimo ndani.+ Yeyote aliye uwanjani, atakufa kwa upanga, na wowote walio jijini, njaa na tauni zitawameza.+ 16 Na watu wao walioponyoka hakika wataponyoka+ na kuwa kama njiwa wa mabondeni juu ya milima,+ ambao wote wanaomboleza, kila mmoja katika kosa lake mwenyewe. 17 Nayo mikono yote, inaendelea kulegea;+ nayo magoti yote yanaendelea kudondoka maji.+ 18 Nao wamejifunga nguo za magunia,+ na kutetemeka kumewafunika;+ na nyuso zote zina aibu+ na vichwa vyao vyote vina upara.+
19 “ ‘Katika barabara watatupa fedha yao wenyewe, na dhahabu yao wenyewe itakuwa chukizo. Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwakomboa katika siku ya ghadhabu ya Yehova.+ Nafsi zao hawatazishibisha, nayo matumbo yao hawatayajaza, kwa maana ni kikwazo kinachosababisha kosa lao.+ 20 Na pambo la mtu—mtu ameliweka kuwa sababu ya kiburi; na sanamu zao zenye kuchukiza,+ machukizo+ yao, wamezifanya kwa hilo. Ndiyo sababu nitalifanya hilo kuwa chukizo kwao.+ 21 Nami nitalitia mkononi mwa wageni walipore na kuwapa waovu wa dunia liwe nyara,+ nao hakika watalitia unajisi.
22 “ ‘Nami nitaugeuzia mbali uso wangu kutoka kwao,+ nao watapatia unajisi mahali pangu palipofichika, na wanyang’anyi wataingia ndani yake kwelikweli na kupatia unajisi.+
23 “ ‘Fanya mnyororo,+ kwa maana nchi yenyewe imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na jiji lenyewe limejaa jeuri.+ 24 Nami nitaingiza yaliyo mabaya kabisa kati ya mataifa,+ nayo hakika yatazimiliki nyumba zao,+ nami nitakikomesha kiburi cha wenye nguvu,+ na patakatifu pao patatiwa unajisi.+ 25 Kutakuwa na maumivu makali, nao hakika watatafuta amani lakini hakutakuwa na yoyote.+ 26 Shida itakuja juu ya shida,+ na kutakuwa na habari juu ya habari, na hakika watu watatafuta maono kutoka kwa nabii,+ na sheria yenyewe itaangamia kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wanaume wazee.+ 27 Mfalme mwenyewe ataomboleza;+ hata mkuu atajivika ukiwa,+ na mikono yenyewe ya watu wa nchi itasumbuka. Kulingana na njia yao nitatenda kuwaelekea wao,+ na kwa hukumu zao nitawahukumu wao;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+