Mathayo
3 Katika siku hizo Yohana Mbatizaji+ alikuja akihubiri katika nyika+ ya Yudea, 2 akisema: “Tubuni,+ kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.”+ 3 Huyu, kwa kweli, ndiye anayesemwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Sikilizeni! Mtu fulani anapaaza sauti nyikani, ‘Tayarisheni+ njia ya Yehova! Nyoosheni barabara zake.’ ” 4 Lakini Yohana huyu mavazi yake yalikuwa ya manyoya ya ngamia+ na alikuwa na mshipi wa ngozi+ kiunoni mwake; nacho chakula chake kilikuwa nzige+ na asali ya mwituni.+ 5 Ndipo Yerusalemu na Yudea yote na nchi yote kandokando ya Yordani zikamwendea, 6 naye akawabatiza watu katika Mto Yordani,+ wakiungama waziwazi dhambi zao.
7 Alipoona wengi wa Mafarisayo na Masadukayo+ wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Ninyi uzao wa nyoka-vipiri,+ ni nani ambaye amewaonyesha ninyi kuikimbia ghadhabu+ inayokuja? 8 Kwa hiyo basi zaeni matunda yanayofaa toba;+ 9 na msiseme moyoni mwenu, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu+ watoto kutoka katika mawe haya. 10 Tayari shoka+ limewekwa kwenye mzizi wa miti; basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa+ na kutupwa ndani ya moto.+ 11 Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji+ kwa sababu ya toba+ yenu; lakini yule anayekuja+ nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, ambaye viatu vyake mimi sistahili kuvivua.+ Huyo atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+ 12 Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake, naye atausafisha uwanja wake wa kupuria, na kukusanya ngano yake katika ghala+ lakini makapi atayateketeza kwa moto+ usioweza kuzimwa.”
13 Ndipo Yesu akaja kutoka Galilaya+ mpaka Yordani kwa Yohana, kusudi ambatize.+ 14 Lakini Yohana akajaribu kumzuia, akisema: “Mimi ndiye ninayehitaji kubatizwa na wewe, na je, wewe unakuja kwangu?” 15 Yesu akajibu, akamwambia: “Acha iwe hivyo, wakati huu, kwa maana katika njia hiyo inafaa kwetu kufanya yote yaliyo ya uadilifu.”+ Ndipo akaacha kumzuia. 16 Baada ya kubatizwa Yesu akapanda mara moja kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa,+ naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa,+ ikija juu yake.+ 17 Tazama! Kulikuwa pia na sauti+ kutoka mbinguni iliyosema: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa,+ ambaye nimemkubali.”+