Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,+

      Kwa maana atalipiza kisasi damu ya watumishi wake,+

      Naye atawalipa kisasi adui zake+

      Naye kwa kweli atafanya upatanisho kwa ajili ya nchi ya watu wake.”

  • Waamuzi 9:57
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 57 Na Mungu akaurudisha uovu wote wa watu wa Shekemu juu ya vichwa vyao wenyewe, ili ile laana+ ya Yothamu+ mwana wa Yerubaali+ ije juu yao.+

  • 2 Samweli 1:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Ndipo Daudi akamwambia: “Hatia yako ya damu na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe,+ kwa sababu kinywa chako mwenyewe kimetoa ushuhuda juu yako,+ kusema, ‘Mimi mwenyewe kwa hakika nilimuua mtiwa-mafuta wa Yehova.’”+

  • 1 Wafalme 2:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Na itatukia kwamba siku utakapotoka na kuvuka bonde la mto la Kidroni,+ ujue bila shaka kwamba utakufa hakika.+ Hatia ya damu kwa ajili yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”+

  • Zaburi 7:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Taabu yake itarudi juu ya kichwa chake mwenyewe,+

      Na jeuri yake mwenyewe itashuka juu ya utosi wa kichwa chake.+

  • Zaburi 55:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Lakini wewe mwenyewe, Ee Mungu, utawashusha mpaka kwenye shimo lililo chini kabisa.+

      Nao watu wenye hatia ya damu na wadanganyifu, hawataishi nusu ya siku zao.+

      Lakini mimi, nitakutegemea wewe.+

  • Zaburi 94:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Naye atayageuza madhara yao yarudi juu yao+

      Naye atawanyamazisha kwa msiba wao wenyewe.+

      Yehova Mungu wetu atawanyamazisha.+

  • Methali 5:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Makosa yake mwenyewe yatamkamata mwovu,+ naye atashikwa katika kamba za dhambi yake mwenyewe.+

  • Methali 28:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Mtu aliyelemewa na hatia ya damu ya nafsi atalikimbilia shimo.+ Watu wasimzuie.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki