Ezekieli
30 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii, nawe useme,+ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Pigeni mayowe, ‘Ole wa siku ile!’+ 3 kwa maana siku iko karibu, naam, siku ya Yehova iko karibu.+ Siku ya mawingu,+ itakuwa wakati uliowekwa wa mataifa.+ 4 Na hakika upanga utaingia Misri,+ na maumivu makali yatatukia Ethiopia wakati ambapo mtu ataanguka akiwa ameuawa katika Misri nao kwa kweli wachukue mali yake nayo misingi yake kwa kweli ibomolewe.+ 5 Ethiopia+ na Putu+na Ludi na jamii yote iliyochangamana+ na Kubu na wana wa nchi ya agano—pamoja nao wataanguka kwa upanga.” ’+
6 “Yehova amesema hivi, ‘Wanaounga mkono Misri lazima waanguke pia, na fahari ya nguvu zake lazima ishuke chini.’+
“ ‘Kutoka Migdoli+ mpaka Sewene+ wataanguka ndani yake kwa upanga,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 7 ‘Lazima pia wafanywe kuwa ukiwa katikati ya nchi zilizofanywa ukiwa, na majiji yake yatakuwa katikati kabisa ya majiji yaliyoharibiwa.+ 8 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowasha moto katika Misri na wasaidizi wake wote kwa kweli wavunjwe.+ 9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele zangu katika meli, ili kuifanya Ethiopia yenye kujitumaini ianze kutetemeka.+ Na maumivu makali yatatukia kati yao katika siku ya Misri, kwa maana, tazama! lazima ije.’+
10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitaufanya pia umati wa Misri ukome kwa mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni.+ 11 Yeye na watu wake pamoja naye, watu wa mataifa wenye kuonea,+ wanaletwa ndani ili kuiharibu nchi. Nao watachomoa panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi kwa waliouawa.+ 12 Nami nitaifanya mifereji ya Nile+ iwe nchi kavu na kuiuza nchi mkononi mwa watu wabaya,+ nami nitaifanya nchi na vyote vinavyoijaza ifanywe ukiwa kwa mkono wa wageni.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’+
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitaangamiza pia sanamu za mavi+ na kufanya miungu isiyo na thamani ikome katika Nofu,+ na hakutakuwa tena na mkuu kutoka katika nchi ya Misri; nami hakika nitatia hofu katika nchi ya Misri.+ 14 Nami nitafanya Pathrosi+ kuwa ukiwa na kuwasha moto katika Soani+ na kufanya matendo ya hukumu katika No.+ 15 Nami nitaimwaga ghadhabu yangu+ juu ya Sini, ngome ya Misri, na kuukatilia mbali umati wa No.+ 16 Nami nitawasha moto katika Misri. Hakika Sini itakuwa katika maumivu makali, na No yenyewe itatekwa kwa kutobolewa matundu; na kwa habari ya Nofu—kutakuwa na wapinzani wakati wa mchana! 17 Nao vijana wa Oni+ na Pibesethi, wataanguka kwa upanga, na majiji yataenda utekwani. 18 Na katika Tehafnehesi+ siku itakuwa na giza, nitakapovunja huko nira za Misri.+ Na katika yeye fahari ya nguvu zake kwa kweli itakomeshwa.+ Na kwa habari yake, mawingu yatamfunika,+ na miji yake mwenyewe ya kandokando itaenda utekwani.+ 19 Nami nitafanya matendo ya hukumu katika Misri;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”
20 Na ikazidi kuwa kwamba katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 21 “Mwana wa binadamu, hakika nitauvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri,+ na, tazama! hautafungwa hata kidogo ili kuufanya upone kwa kutia kitambaa ili kuufunga,+ ili uwe na nguvu za kushika upanga.”
22 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, mimi niko dhidi ya Farao mfalme wa Misri,+ nami nitaivunja mikono yake,+ ule wenye nguvu na ule uliovunjika,+ nami nitaufanya upanga uanguke kutoka mkononi mwake.+ 23 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali.+ 24 Nami nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni+ na kuutia upanga wangu mkononi mwake,+ nami nitaivunja mikono ya Farao, naye ataugua kwelikweli mbele yake kama mwenye majeraha ya kufisha.+ 25 Nami nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni, na mikono yenyewe ya Farao itaanguka; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babiloni naye kwa kweli aunyooshe juu ya nchi ya Misri.+ 26 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa+ na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”