Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 20
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Mataifa jirani yawatisha watu wa Yuda (1-4)

      • Yehoshafati asali apate msaada (5-13)

      • Jibu la Yehova (14-19)

      • Watu wa Yuda waokolewa kimuujiza (20-30)

      • Mwisho wa utawala wa Yehoshafati (31-37)

2 Mambo ya Nyakati 20:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Wameuni.”

Marejeo

  • +Amu 3:14; 2Sa 8:2; Zb 83:2, 6
  • +Mwa 19:36-38

2 Mambo ya Nyakati 20:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana ni Bahari ya Chumvi.

Marejeo

  • +Yos 15:1
  • +Yos 15:20, 62

2 Mambo ya Nyakati 20:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “akauelekeza uso wake.”

Marejeo

  • +2Nya 19:1, 3

2 Mambo ya Nyakati 20:4

Marejeo

  • +Kum 4:29-31

2 Mambo ya Nyakati 20:6

Marejeo

  • +1Fa 8:23; Mt 6:9
  • +1Nya 29:11; Da 4:17
  • +1Nya 29:12; Isa 40:15, 17; Da 4:35

2 Mambo ya Nyakati 20:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu ya.”

Marejeo

  • +Mwa 12:7; Ne 9:7, 8; Isa 41:8; Yak 2:23

2 Mambo ya Nyakati 20:8

Marejeo

  • +2Nya 2:4

2 Mambo ya Nyakati 20:9

Marejeo

  • +2Nya 6:20
  • +1Fa 8:33, 34; 2Nya 6:28-30

2 Mambo ya Nyakati 20:10

Marejeo

  • +Mwa 36:8
  • +Hes 20:17, 18; Kum 2:5, 9, 19

2 Mambo ya Nyakati 20:11

Marejeo

  • +Amu 11:23, 24; Zb 83:2, 4

2 Mambo ya Nyakati 20:12

Marejeo

  • +Amu 11:27, 28; Zb 7:6
  • +2Fa 6:15, 16
  • +2Nya 14:11; Zb 25:15; 62:1

2 Mambo ya Nyakati 20:15

Marejeo

  • +Kum 1:29, 30; Yos 11:4, 6; 2Nya 32:7, 8

2 Mambo ya Nyakati 20:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “korongo.”

2 Mambo ya Nyakati 20:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “muone jinsi Yehova atakavyowaokoa.”

Marejeo

  • +Isa 30:15
  • +Kut 14:13, 14; 15:2; 1Sa 2:1; 1Nya 16:23; Omb 3:26
  • +Kum 31:8; Yos 10:25
  • +Hes 14:9; 2Nya 15:2

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Masomo ya Biblia, kur. 120-121

    The Watchtower,

    12/1/2005, uku. 21

    6/1/2003, kur. 21-22

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 12/1 21; w03 6/1 21-22

2 Mambo ya Nyakati 20:19

Marejeo

  • +1Nya 23:12
  • +1Nya 15:16

2 Mambo ya Nyakati 20:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuvumilia.”

Marejeo

  • +2Nya 11:5, 6
  • +Kut 14:31; 19:9

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    5/1/1998, uku. 20

  • Fahirishi ya Machapisho

    w98 5/1 20

2 Mambo ya Nyakati 20:21

Marejeo

  • +1Nya 15:16
  • +Kut 34:6

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    5/1/1998, kur. 20-21

  • Fahirishi ya Machapisho

    w98 5/1 20

2 Mambo ya Nyakati 20:22

Marejeo

  • +Amu 7:22; 1Sa 14:20

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    5/1/1998, kur. 20-21

  • Fahirishi ya Machapisho

    w98 5/1 20

2 Mambo ya Nyakati 20:23

Marejeo

  • +Kum 2:5
  • +Kut 14:25; Eze 38:21

2 Mambo ya Nyakati 20:24

Marejeo

  • +2Nya 20:16
  • +Kut 14:30; Zb 110:5, 6; Isa 37:36

2 Mambo ya Nyakati 20:25

Marejeo

  • +Kut 12:35; 2Fa 7:15, 16

2 Mambo ya Nyakati 20:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

  • *

    Tnn., “walimbariki.”

  • *

    Maana yake “Baraka.”

Marejeo

  • +Kut 17:14, 15; 1Sa 7:12

2 Mambo ya Nyakati 20:27

Marejeo

  • +1Sa 2:1; Zb 20:5; 30:1

2 Mambo ya Nyakati 20:28

Marejeo

  • +2Sa 6:5; 1Nya 16:5
  • +Hes 10:8; 1Nya 13:8; 2Nya 29:26
  • +Zb 116:19

2 Mambo ya Nyakati 20:29

Marejeo

  • +Kut 15:13, 14; Yos 9:3, 9; 2Nya 17:10

2 Mambo ya Nyakati 20:30

Marejeo

  • +Yos 23:1; 2Sa 7:1; 2Nya 15:15

2 Mambo ya Nyakati 20:31

Marejeo

  • +1Fa 22:41, 42

2 Mambo ya Nyakati 20:32

Marejeo

  • +1Fa 15:11
  • +2Nya 17:3, 4; 19:2, 3

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (Funzo),

    3/2017, uku. 20

2 Mambo ya Nyakati 20:33

Marejeo

  • +1Fa 15:14; 22:43; 2Nya 17:1, 6
  • +1Fa 18:21

2 Mambo ya Nyakati 20:34

Marejeo

  • +1Fa 16:1; 2Nya 19:2
  • +2Nya 16:7

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    3/15/2009, uku. 32

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 3/15 32

2 Mambo ya Nyakati 20:35

Marejeo

  • +2Fa 1:2, 16

2 Mambo ya Nyakati 20:36

Marejeo

  • +1Fa 10:22, 23
  • +Hes 33:1, 35; Kum 2:8; 1Fa 9:26

2 Mambo ya Nyakati 20:37

Marejeo

  • +2Nya 19:2; Zb 127:1
  • +1Fa 22:48

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 20:1Amu 3:14; 2Sa 8:2; Zb 83:2, 6
2 Nya. 20:1Mwa 19:36-38
2 Nya. 20:2Yos 15:1
2 Nya. 20:2Yos 15:20, 62
2 Nya. 20:32Nya 19:1, 3
2 Nya. 20:4Kum 4:29-31
2 Nya. 20:61Fa 8:23; Mt 6:9
2 Nya. 20:61Nya 29:11; Da 4:17
2 Nya. 20:61Nya 29:12; Isa 40:15, 17; Da 4:35
2 Nya. 20:7Mwa 12:7; Ne 9:7, 8; Isa 41:8; Yak 2:23
2 Nya. 20:82Nya 2:4
2 Nya. 20:92Nya 6:20
2 Nya. 20:91Fa 8:33, 34; 2Nya 6:28-30
2 Nya. 20:10Mwa 36:8
2 Nya. 20:10Hes 20:17, 18; Kum 2:5, 9, 19
2 Nya. 20:11Amu 11:23, 24; Zb 83:2, 4
2 Nya. 20:12Amu 11:27, 28; Zb 7:6
2 Nya. 20:122Fa 6:15, 16
2 Nya. 20:122Nya 14:11; Zb 25:15; 62:1
2 Nya. 20:15Kum 1:29, 30; Yos 11:4, 6; 2Nya 32:7, 8
2 Nya. 20:17Isa 30:15
2 Nya. 20:17Kut 14:13, 14; 15:2; 1Sa 2:1; 1Nya 16:23; Omb 3:26
2 Nya. 20:17Kum 31:8; Yos 10:25
2 Nya. 20:17Hes 14:9; 2Nya 15:2
2 Nya. 20:191Nya 23:12
2 Nya. 20:191Nya 15:16
2 Nya. 20:202Nya 11:5, 6
2 Nya. 20:20Kut 14:31; 19:9
2 Nya. 20:211Nya 15:16
2 Nya. 20:21Kut 34:6
2 Nya. 20:22Amu 7:22; 1Sa 14:20
2 Nya. 20:23Kum 2:5
2 Nya. 20:23Kut 14:25; Eze 38:21
2 Nya. 20:242Nya 20:16
2 Nya. 20:24Kut 14:30; Zb 110:5, 6; Isa 37:36
2 Nya. 20:25Kut 12:35; 2Fa 7:15, 16
2 Nya. 20:26Kut 17:14, 15; 1Sa 7:12
2 Nya. 20:271Sa 2:1; Zb 20:5; 30:1
2 Nya. 20:282Sa 6:5; 1Nya 16:5
2 Nya. 20:28Hes 10:8; 1Nya 13:8; 2Nya 29:26
2 Nya. 20:28Zb 116:19
2 Nya. 20:29Kut 15:13, 14; Yos 9:3, 9; 2Nya 17:10
2 Nya. 20:30Yos 23:1; 2Sa 7:1; 2Nya 15:15
2 Nya. 20:311Fa 22:41, 42
2 Nya. 20:321Fa 15:11
2 Nya. 20:322Nya 17:3, 4; 19:2, 3
2 Nya. 20:331Fa 15:14; 22:43; 2Nya 17:1, 6
2 Nya. 20:331Fa 18:21
2 Nya. 20:341Fa 16:1; 2Nya 19:2
2 Nya. 20:342Nya 16:7
2 Nya. 20:352Fa 1:2, 16
2 Nya. 20:361Fa 10:22, 23
2 Nya. 20:36Hes 33:1, 35; Kum 2:8; 1Fa 9:26
2 Nya. 20:372Nya 19:2; Zb 127:1
2 Nya. 20:371Fa 22:48
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 20:1-37

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

20 Baadaye Wamoabu+ na Waamoni,+ pamoja na baadhi ya Waamonimu,* wakaja kupigana vita na Yehoshafati. 2 Basi Yehoshafati akaambiwa hivi: “Umati mkubwa umekuja kukushambulia kutoka katika eneo la bahari,* kutoka Edomu,+ wamefika Hasason-tamari, yaani, En-gedi.”+ 3 Ndipo Yehoshafati akaogopa, akaazimia* kumtafuta Yehova.+ Basi akatangaza watu wote wa Yuda wafunge. 4 Kisha watu wa Yuda wakakusanyika pamoja kutafuta ushauri wa Yehova;+ walikuja kutoka katika majiji yote ya Yuda ili kutafuta ushauri wa Yehova.

5 Ndipo Yehoshafati akasimama katika kutaniko la Yuda na Yerusalemu ndani ya nyumba ya Yehova mbele ya ule ua mpya, 6 akasema:

“Ee Yehova Mungu wa mababu zetu, je, wewe si Mungu mbinguni;+ je, huna mamlaka juu ya falme zote za mataifa?+ Mkononi mwako mna nguvu na uwezo, na hakuna anayeweza kushindana nawe.+ 7 Ee Mungu wetu, je, hukuwafukuza wakaaji wa nchi hii kutoka mbele ya watu wako Waisraeli na kisha kuupa uzao wa* rafiki yako Abrahamu nchi hii iwe miliki yao ya kudumu?+ 8 Nao wakaishi katika nchi hiyo na kukujengea humo mahali patakatifu kwa ajili ya jina lako,+ wakisema, 9 ‘Tukipatwa na msiba, upanga, hukumu kali, au ugonjwa hatari, au njaa, na tusimame mbele ya nyumba hii na mbele zako (kwa maana jina lako limo katika nyumba hii)+ na kukulilia utusaidie katika taabu yetu, nawe usikie na kutuokoa.’+ 10 Sasa tazama, ndio hawa wanaume wa Amoni, Moabu, na eneo lenye milima la Seiri,+ ambao hukuwaruhusu Waisraeli wawavamie walipotoka nchini Misri. Waligeuka na kwenda mbali nao na hawakuwaangamiza.+ 11 Sasa wanatulipa kwa kuja kutufukuza kutoka katika miliki yako uliyotupatia iwe urithi wetu.+ 12 Ee Mungu wetu, je, hutatekeleza hukumu dhidi yao?+ Kwa maana hatuna nguvu mbele ya umati huu mkubwa unaokuja kutushambulia; nasi hatujui tunalopaswa kufanya,+ lakini macho yetu yanakutazama wewe.”+

13 Wakati huo, watu wote wa Yuda walikuwa wamesimama mbele za Yehova, pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, na wana wao.

14 Ndipo katikati ya kutaniko, roho ya Yehova ikamjia Yahazieli mwana wa Zekaria mwana wa Benaya mwana wa Yeieli mwana wa Matania, Mlawi wa wana wa Asafu. 15 Akasema: “Sikilizeni kwa makini, enyi watu wote wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu na Mfalme Yehoshafati! Yehova anawaambia hivi: ‘Msiogope wala msihofu kwa sababu ya umati huu mkubwa, kwa maana vita si vyenu bali ni vya Mungu.+ 16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakuwa wakipanda kupitia njia ya Sisi, nanyi mtawakuta mwishoni mwa bonde* kabla ya nyika ya Yerueli. 17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Simameni mahali penu, simameni tuli,+ muuone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu.*+ Enyi watu wa Yuda na Yerusalemu, msiogope wala msihofu.+ Kesho nendeni mkakabiliane nao, na Yehova atakuwa pamoja nanyi.’”+

18 Mara moja Yehoshafati akainama chini kifudifudi, na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wakaanguka chini mbele za Yehova ili kumwabudu Yehova. 19 Kisha Walawi waliokuwa wazao wa Wakohathi+ na wazao wa Wakora wakasimama ili kumsifu Yehova Mungu wa Israeli kwa sauti kubwa sana.+

20 Kesho yake, wakaamka asubuhi na mapema na kwenda katika nyika ya Tekoa.+ Walipokuwa wakienda, Yehoshafati akasimama na kusema: “Nisikilizeni, enyi watu wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu! Iweni na imani katika Yehova Mungu wenu ili mweze kusimama imara.* Iweni na imani katika manabii wake,+ nanyi mtafanikiwa.”

21 Baada ya kushauriana na watu, aliwaweka wanaume ili wamwimbie+ Yehova na kumsifu wakiwa wamevaa mavazi matakatifu huku wakiwatangulia wanaume wenye silaha, wakisema: “Mshukuruni Yehova, kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”+

22 Walipoanza kuimba kwa shangwe nyimbo za sifa, Yehova akawaweka watu wawavizie wanaume wa Amoni, Moabu, na eneo lenye milima la Seiri waliokuwa wakivamia Yuda, nao wakaangamizana wenyewe kwa wenyewe.+ 23 Na Waamoni na Wamoabu wakageuka na kuwashambulia wakaaji wa eneo lenye milima la Seiri+ ili wawaue na kuwaangamiza kabisa; na baada ya kuwamaliza wakaaji wa Seiri, wakasaidiana kuangamizana wao kwa wao.+

24 Lakini watu wa Yuda walipofika kwenye mnara wa mlinzi wa nyikani+ na kutazama umati huo, waliona maiti zao zikiwa zimetapakaa ardhini;+ hakuna yeyote aliyeponyoka. 25 Basi Yehoshafati na watu wake wakaja kuchukua nyara kutoka kwao, wakapata vitu vingi sana, mavazi, na vitu vyenye kutamanika, ambavyo waliwavua mpaka waliposhindwa kubeba zaidi.+ Walichukua nyara hizo kwa siku tatu, kwa maana zilikuwa nyingi sana. 26 Siku ya nne walikusanyika pamoja katika Bonde la* Beraka, kwa maana walimsifu* Yehova huko. Ndiyo sababu tangu siku hiyo walipaita mahali hapo Bonde la Beraka.*+

27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakishangilia, kwa maana Yehova alikuwa amewafanya washangilie dhidi ya maadui wao.+ 28 Basi wakaingia Yerusalemu wakiwa na vinanda, vinubi,+ na tarumbeta+ na kwenda katika nyumba ya Yehova.+ 29 Na falme zote za nchi mbalimbali ziliposikia kwamba Yehova alikuwa amepigana na maadui wa Israeli zilishikwa na hofu ya Mungu.+ 30 Kwa hiyo ufalme wa Yehoshafati haukuwa na usumbufu wowote, na Mungu wake akaendelea kumpumzisha pande zote.+

31 Na Yehoshafati akaendelea kutawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka 35 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 25 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Azuba binti ya Shilhi.+ 32 Aliendelea kutembea katika njia ya Asa baba yake.+ Hakugeuka kutoka katika njia hiyo, naye alitenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ 33 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na bado watu hawakuwa wameutayarisha moyo wao kwa ajili ya Mungu wa mababu zao.+

34 Na mambo mengine katika historia ya Yehoshafati, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika maandishi ya Yehu+ mwana wa Hanani,+ yaliyotiwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. 35 Baada ya hayo Mfalme Yehoshafati wa Yuda akaungana na Mfalme Ahazia wa Israeli, aliyetenda uovu.+ 36 Kwa hiyo akashirikiana naye katika kutengeneza meli za kwenda Tarshishi,+ walizitengenezea kule Esion-geberi.+ 37 Hata hivyo, Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha alitoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akisema: “Kwa sababu umeungana na Ahazia, Yehova ataharibu kazi zako.”+ Basi meli hizo zikavunjika,+ kwa hiyo hazikuweza kwenda Tarshishi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki