Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 22
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Wafalme—Yaliyomo

      • Yehoshafati aungana na Ahabu (1-12)

      • Mikaya atabiri kwamba watashindwa (13-28)

        • Roho ya udanganyifu itampumbaza Ahabu (21, 22)

      • Ahabu auawa huko Ramothi-gileadi (29-40)

      • Yehoshafati atawala Yuda (41-50)

      • Ahazia mfalme wa Israeli (51-53)

1 Wafalme 22:2

Marejeo

  • +1Fa 15:24
  • +2Nya 18:2, 3

1 Wafalme 22:3

Marejeo

  • +Yos 20:8, 9; 1Fa 4:7, 13

1 Wafalme 22:4

Marejeo

  • +2Fa 3:7; 2Nya 19:2

1 Wafalme 22:5

Marejeo

  • +Hes 27:21
  • +2Nya 18:4, 5

1 Wafalme 22:7

Marejeo

  • +2Fa 3:11; 2Nya 18:6, 7

1 Wafalme 22:8

Marejeo

  • +1Fa 18:4
  • +1Fa 21:20; 2Nya 36:16
  • +Isa 30:9, 10; Yer 38:4

1 Wafalme 22:9

Marejeo

  • +2Nya 18:8-11

1 Wafalme 22:10

Marejeo

  • +Eze 13:2, 3

1 Wafalme 22:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utawasukuma.”

1 Wafalme 22:13

Marejeo

  • +2Nya 18:12-16

1 Wafalme 22:17

Marejeo

  • +Kum 28:15, 25

1 Wafalme 22:18

Marejeo

  • +2Nya 18:17

1 Wafalme 22:19

Marejeo

  • +Isa 6:1; Eze 1:26
  • +2Nya 18:18-22; Ayu 1:6; Da 7:9, 10; Mt 18:10; Ufu 5:11

1 Wafalme 22:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “malaika.”

Marejeo

  • +Zb 104:4; Ebr 1:7, 14

1 Wafalme 22:22

Marejeo

  • +1Fa 22:6

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi, 4/15/1987, uku. 21

1 Wafalme 22:23

Marejeo

  • +Eze 14:9
  • +1Fa 20:42

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi, 4/15/1987, uku. 21

1 Wafalme 22:24

Marejeo

  • +2Nya 18:23-27

1 Wafalme 22:27

Marejeo

  • +Ebr 11:32, 36

1 Wafalme 22:28

Marejeo

  • +Hes 16:28, 29

1 Wafalme 22:29

Marejeo

  • +2Nya 18:28-32

1 Wafalme 22:30

Marejeo

  • +2Nya 35:22

1 Wafalme 22:31

Marejeo

  • +1Fa 20:1

1 Wafalme 22:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kambini.”

Marejeo

  • +2Nya 18:33, 34

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu, uku. 169

1 Wafalme 22:35

Marejeo

  • +1Fa 20:42

1 Wafalme 22:36

Marejeo

  • +1Fa 22:17

1 Wafalme 22:37

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Igeni Imani Yao, makala 1

1 Wafalme 22:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “mbwa waliramba damu yake mahali ambapo makahaba waliogea.”

Marejeo

  • +1Fa 21:18, 19

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Igeni Imani Yao, makala 1

    Mnara wa Mlinzi,

    2/1/2014, uku. 15

1 Wafalme 22:39

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la mfalme alilojenga la.”

Marejeo

  • +1Fa 10:22; Eze 27:15

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    11/1/1990, kur. 16-17

    “Kila Andiko,” uku. 149

1 Wafalme 22:40

Marejeo

  • +1Fa 16:28
  • +2Fa 1:2; 2Nya 20:35

1 Wafalme 22:41

Marejeo

  • +1Nya 3:10; 2Nya 17:1; 20:31; Mt 1:8

1 Wafalme 22:43

Marejeo

  • +1Fa 15:11; 2Nya 14:11; 15:8
  • +2Nya 17:3
  • +Kum 12:14; 1Fa 14:23; 15:14

1 Wafalme 22:44

Marejeo

  • +2Nya 18:1; 19:2

1 Wafalme 22:46

Marejeo

  • +Kum 23:17, 18; 1Fa 14:24
  • +1Fa 15:11, 12

1 Wafalme 22:47

Marejeo

  • +Mwa 36:1, 9
  • +2Sa 8:14; 2Fa 8:20-22; Zb 108:9

1 Wafalme 22:48

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +1Fa 10:22
  • +1Fa 9:26; 2Nya 20:35-37

1 Wafalme 22:50

Marejeo

  • +1Fa 2:10
  • +2Fa 8:16; 2Nya 21:1, 5

1 Wafalme 22:51

Marejeo

  • +2Fa 1:2

1 Wafalme 22:52

Marejeo

  • +1Fa 16:30
  • +1Fa 21:25
  • +1Fa 12:28-30; 13:33

1 Wafalme 22:53

Marejeo

  • +1Fa 16:31, 32; 2Fa 1:2
  • +Kut 20:3; 34:14

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Fal. 22:21Fa 15:24
1 Fal. 22:22Nya 18:2, 3
1 Fal. 22:3Yos 20:8, 9; 1Fa 4:7, 13
1 Fal. 22:42Fa 3:7; 2Nya 19:2
1 Fal. 22:5Hes 27:21
1 Fal. 22:52Nya 18:4, 5
1 Fal. 22:72Fa 3:11; 2Nya 18:6, 7
1 Fal. 22:81Fa 18:4
1 Fal. 22:81Fa 21:20; 2Nya 36:16
1 Fal. 22:8Isa 30:9, 10; Yer 38:4
1 Fal. 22:92Nya 18:8-11
1 Fal. 22:10Eze 13:2, 3
1 Fal. 22:132Nya 18:12-16
1 Fal. 22:17Kum 28:15, 25
1 Fal. 22:182Nya 18:17
1 Fal. 22:19Isa 6:1; Eze 1:26
1 Fal. 22:192Nya 18:18-22; Ayu 1:6; Da 7:9, 10; Mt 18:10; Ufu 5:11
1 Fal. 22:21Zb 104:4; Ebr 1:7, 14
1 Fal. 22:221Fa 22:6
1 Fal. 22:23Eze 14:9
1 Fal. 22:231Fa 20:42
1 Fal. 22:242Nya 18:23-27
1 Fal. 22:27Ebr 11:32, 36
1 Fal. 22:28Hes 16:28, 29
1 Fal. 22:292Nya 18:28-32
1 Fal. 22:302Nya 35:22
1 Fal. 22:311Fa 20:1
1 Fal. 22:342Nya 18:33, 34
1 Fal. 22:351Fa 20:42
1 Fal. 22:361Fa 22:17
1 Fal. 22:381Fa 21:18, 19
1 Fal. 22:391Fa 10:22; Eze 27:15
1 Fal. 22:401Fa 16:28
1 Fal. 22:402Fa 1:2; 2Nya 20:35
1 Fal. 22:411Nya 3:10; 2Nya 17:1; 20:31; Mt 1:8
1 Fal. 22:431Fa 15:11; 2Nya 14:11; 15:8
1 Fal. 22:432Nya 17:3
1 Fal. 22:43Kum 12:14; 1Fa 14:23; 15:14
1 Fal. 22:442Nya 18:1; 19:2
1 Fal. 22:46Kum 23:17, 18; 1Fa 14:24
1 Fal. 22:461Fa 15:11, 12
1 Fal. 22:47Mwa 36:1, 9
1 Fal. 22:472Sa 8:14; 2Fa 8:20-22; Zb 108:9
1 Fal. 22:481Fa 10:22
1 Fal. 22:481Fa 9:26; 2Nya 20:35-37
1 Fal. 22:501Fa 2:10
1 Fal. 22:502Fa 8:16; 2Nya 21:1, 5
1 Fal. 22:512Fa 1:2
1 Fal. 22:521Fa 16:30
1 Fal. 22:521Fa 21:25
1 Fal. 22:521Fa 12:28-30; 13:33
1 Fal. 22:531Fa 16:31, 32; 2Fa 1:2
1 Fal. 22:53Kut 20:3; 34:14
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
  • 46
  • 47
  • 48
  • 49
  • 50
  • 51
  • 52
  • 53
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Wafalme 22:1-53

Kitabu cha Kwanza cha Wafalme

22 Kwa miaka mitatu hakukuwa na vita kati ya Siria na Israeli. 2 Katika mwaka wa tatu, Mfalme Yehoshafati+ wa Yuda akashuka kwenda kwa mfalme wa Israeli.+ 3 Kisha mfalme wa Israeli akawaambia watumishi wake: “Je, mnajua kwamba Ramothi-gileadi+ ni jiji letu? Na bado tunasitasita kulichukua kutoka kwa mfalme wa Siria.” 4 Halafu akamuuliza Yehoshafati: “Je, utaenda pamoja nami kupigana kule Ramothi-gileadi?” Yehoshafati akamjibu hivi mfalme wa Israeli: “Mimi ni kama wewe. Watu wangu ni kama watu wako. Farasi wangu ni kama farasi wako.”+

5 Lakini Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli: “Tafadhali, kwanza tafuta+ neno la Yehova.”+ 6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya pamoja manabii, wanaume wapatao 400, akawauliza: “Je, niende kupigana vita dhidi ya Ramothi-gileadi, au nisiende?” Wakasema: “Panda uende, na Yehova atalitia jiji hilo mikononi mwako.”

7 Kisha Yehoshafati akasema: “Je, hakuna nabii wa Yehova mahali hapa? Acheni tumuulize yeye pia.”+ 8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Bado kuna mtu mmoja ambaye tunaweza kumwomba ushauri kutoka kwa Yehova;+ lakini ninamchukia,+ kwa maana hatabiri kamwe mambo mema kunihusu, ila mabaya tu.+ Anaitwa Mikaya mwana wa Imla.” Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme, usiseme jambo kama hilo.”

9 Basi mfalme wa Israeli akamwita ofisa fulani wa makao ya mfalme na kumwambia: “Mlete haraka Mikaya mwana wa Imla.”+ 10 Sasa mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja wao kwenye kiti chake cha ufalme, akiwa amevaa mavazi ya kifalme, katika uwanja wa kupuria nafaka kwenye lango la kuingia Samaria, na manabii wote walikuwa wakitabiri mbele yao.+ 11 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akajitengenezea pembe za chuma na kusema: “Yehova anasema hivi: ‘Kwa pembe hizi utawapiga* Wasiria mpaka utakapowaangamiza.’” 12 Wale manabii wengine wote walikuwa wakitabiri vivyo hivyo, wakisema: “Panda mpaka Ramothi-gileadi, nawe utafanikiwa; Yehova atalitia jiji hilo mikononi mwako mfalme.”

13 Basi mjumbe aliyeenda kumwita Mikaya akamwambia: “Tazama! Manabii wote kwa pamoja wanasema mema kumhusu mfalme. Tafadhali, acha neno lako liwe kama maneno yao, useme mema.”+ 14 Lakini Mikaya akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, jambo lolote ambalo Yehova ataniambia ndilo nitakalosema.” 15 Kisha akaingia kwa mfalme, naye mfalme akamuuliza: “Mikaya, je, twende kupigana vita dhidi ya Ramothi-gileadi, au tusiende?” Mara moja akajibu: “Panda uende nawe utafanikiwa; Yehova atalitia jiji hilo mikononi mwako.” 16 Ndipo mfalme akamuuliza: “Nitakuapisha mara ngapi kwamba hupaswi kuniambia jambo lingine lolote isipokuwa ukweli katika jina la Yehova?” 17 Basi Mikaya akasema: “Ninawaona Waisraeli wote wakiwa wametawanyika milimani,+ kama kondoo wasio na mchungaji. Yehova akasema: ‘Hawa hawana bwana. Acha kila mmoja wao arudi kwa amani nyumbani kwake.’”

18 Kisha mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Je, sikukwambia, ‘Hatatabiri mambo mema kunihusu, ila mabaya’?”+

19 Ndipo Mikaya akasema: “Basi, sikia neno la Yehova: Nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme+ na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kando yake, upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.+ 20 Halafu Yehova akauliza, ‘Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili apande kwenda na kufia huko Ramothi-gileadi?’ Na malaika mmoja akasema jambo moja na mwingine akasema jambo lingine. 21 Kisha roho*+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova na kusema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Yehova akamuuliza, ‘Utatumia njia gani?’ 22 Akajibu, ‘Nitaenda na kuwa roho ya udanganyifu katika vinywa vya manabii wake wote.’+ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na zaidi ya hilo, utafanikiwa. Nenda ukafanye hivyo.’ 23 Na sasa Yehova ametia roho ya udanganyifu katika vinywa vya hawa manabii wako wote,+ lakini Yehova ametangaza kwamba utapata msiba.”+

24 Sasa Sedekia mwana wa Kenaana akamkaribia Mikaya na kumpiga kwenye shavu na kumuuliza: “Roho ya Yehova iliniacha jinsi gani na kuja kuzungumza nawe?”+ 25 Mikaya akamjibu: “Tazama! Utajua ni jinsi gani utakapoingia katika chumba cha ndani zaidi kujificha.” 26 Ndipo mfalme wa Israeli akasema: “Mchukue Mikaya umpeleke kwa Amoni mkuu wa jiji na kwa Yoashi mwana wa mfalme. 27 Waambie, ‘Mfalme anasema hivi: “Mfungeni mtu huyu gerezani+ na kumlisha kiasi kidogo cha mkate na maji mpaka nitakaporudi kwa amani.”’” 28 Lakini Mikaya akasema: “Ukirudi kwa amani, basi Yehova hajazungumza nami.”+ Kisha akasema: “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote.”

29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakapanda kwenda Ramothi-gileadi.+ 30 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Nitabadili sura yangu na kuingia vitani, lakini wewe vaa mavazi yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akabadili sura yake+ na kuingia vitani. 31 Sasa mfalme wa Siria alikuwa amewaagiza hivi makamanda wake 32 wa magari ya vita:+ “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.” 32 Na mara tu makamanda hao wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakaambiana: “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Basi wakamgeukia ili kupigana naye; na Yehoshafati akaanza kulilia msaada. 33 Makamanda hao wa magari ya vita walipoona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, mara moja wakaacha kumfuatia.

34 Lakini mtu fulani alivuta upinde wake bila kukusudia na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya sehemu ambazo koti lake la vita linaungana. Basi mfalme akamwambia mtu aliyeendesha gari lake: “Geuka uniondoe vitani,* kwa sababu nimejeruhiwa vibaya.”+ 35 Vita vikapamba moto siku hiyo yote, nao wakalazimika kumsimamisha mfalme ndani ya gari akiwaelekea Wasiria. Damu ya jeraha lake ikamwagika ndani ya gari lake la vita, akafa jioni.+ 36 Jua lilipokuwa likitua amri hii ikatangazwa kambini: “Kila mtu aende katika jiji lake! Kila mtu aende katika nchi yake!”+ 37 Basi mfalme akafa, akaletwa Samaria; wakamzika mfalme huko Samaria. 38 Walipolisafisha gari hilo la vita kando ya kidimbwi cha Samaria, mbwa waliramba damu yake na makahaba wakaogea mahali hapo,* kama Yehova alivyokuwa amesema.+

39 Na mambo mengine katika historia ya Ahabu, mambo yote aliyofanya na nyumba aliyojenga ya* pembe za tembo+ na majiji yote aliyojenga, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 40 Kisha Ahabu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ na Ahazia+ mwana wake akawa mfalme baada yake.

41 Yehoshafati+ mwana wa Asa aliwekwa kuwa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Ahabu wa Israeli. 42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka 35 alipowekwa kuwa mfalme, naye alitawala kwa miaka 25 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Azuba binti ya Shilhi. 43 Yehoshafati aliendelea kutembea katika njia yote ya Asa+ baba yake. Hakugeuka na kuiacha njia hiyo, naye alitenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa, na bado watu walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.+ 44 Yehoshafati alidumisha mahusiano ya amani na mfalme wa Israeli.+ 45 Na mambo mengine katika historia ya Yehoshafati, mambo makuu aliyotekeleza na jinsi alivyopigana vita, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 46 Pia aliwaondoa kabisa nchini wanaume wote makahaba wa hekaluni+ waliobaki katika siku za Asa baba yake.+

47 Wakati huo hakukuwa na mfalme katika nchi ya Edomu;+ naibu ndiye aliyetawala kama mfalme.+

48 Yehoshafati pia akatengeneza meli* za Tarshishi za kwenda Ofiri kuleta dhahabu,+ lakini hazikwenda kwa sababu meli hizo zilivunjika huko Esion-geberi.+ 49 Wakati huo ndipo Ahazia mwana wa Ahabu alipomwambia Yehoshafati: “Waruhusu watumishi wangu wasafiri na watumishi wako katika meli hizo,” lakini Yehoshafati hakukubali.

50 Kisha Yehoshafati akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake+ katika Jiji la Daudi babu yake; na Yehoramu+ mwanawe akawa mfalme baada yake.

51 Ahazia+ mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa 17 wa utawala wa Mfalme Yehoshafati wa Yuda, naye alitawala Israeli kwa miaka miwili. 52 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova na kutembea katika njia ya baba yake+ na mama yake+ na katika njia ya Yeroboamu mwana wa Nebati, aliyesababisha Waisraeli watende dhambi.+ 53 Aliendelea kumwabudu Baali+ na kumwinamia, akaendelea kumkasirisha Yehova Mungu wa Israeli,+ kama baba yake alivyokuwa amefanya.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki