Nehemia
7 Na ikawa kwamba, mara tu ukuta ulipojengwa upya,+ nikaisimamisha milango+ yake mara moja. Kisha watunza-malango+ na waimbaji+ na Walawi+ wakawekwa rasmi. 2 Nami nikaweka usimamizi wa Yerusalemu chini ya Hanani ndugu yangu na Hanania+ mkuu wa Ngome,+ kwa maana alikuwa mwanamume mwenye kutegemeka+ sana naye alimwogopa+ Mungu wa kweli kuliko wengine wengi. 3 Basi nikawaambia: “Malango+ ya Yerusalemu hayapaswi kufunguliwa mpaka jua liwake kabisa; nao waifunge milango na kuiweka komeo+ wao wakiwa wamesimama kando. Nanyi wekeni walinzi wa wakaaji wa Yerusalemu, kila mmoja katika kituo chake mwenyewe cha ulinzi na kila mmoja mbele ya nyumba yake mwenyewe.”+ 4 Basi jiji lilikuwa pana na kubwa, na kulikuwa na watu wachache ndani yake,+ wala hakukuwa na nyumba zozote zilizojengwa.
5 Lakini Mungu wangu akaweka wazo moyoni+ mwangu kwamba nikusanye watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na watu ili wajiandikishe kiukoo.+ Ndipo nikakipata kitabu cha uandikishaji wa kiukoo+ cha wale waliokuja pale mwanzoni, na ndani nikakuta imeandikwa:
6 Hawa ndio wana wa wilaya ya utawala+ waliokuja kutoka utekwani+ mwa wale waliohamishwa ambao Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni,+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake mwenyewe;+ 7 wale waliokuja pamoja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai,+ Bilshani, Misperethi, Bigvai, Nehumu, Baana.
Hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli: 8 Wana wa Paroshi,+ 2,172; 9 wana wa Shefatia,+ 372; 10 wana wa Ara,+ 652; 11 wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu,+ 2,818; 12 wana wa Elamu,+ 1,254; 13 wana wa Zatu,+ 845; 14 wana wa Zakai,+ 760; 15 wana wa Binui,+ 648; 16 wana wa Bebai,+ 628; 17 wana wa Azgadi,+ 2,322; 18 wana wa Adonikamu,+ 667; 19 wana wa Bigvai,+ 2,067; 20 wana wa Adini,+ 655; 21 wana wa Ateri,+ wa Hezekia, 98; 22 wana wa Hashumu,+ 328; 23 wana wa Besai,+ 324; 24 wana wa Harifu,+ 112; 25 wana wa Gibeoni,+ 95; 26 wanaume wa Bethlehemu+ na Netofa,+ 188; 27 wanaume wa Anathothi,+ 128; 28 wanaume wa Beth-azmavethi,+ 42; 29 wanaume wa Kiriath-yearimu,+ Kefira+ na Beerothi,+ 743; 30 wanaume wa Rama+ na Geba,+ 621; 31 wanaume wa Mikmasi,+ 122; 32 wanaume wa Betheli+ na Ai,+ 123; 33 wanaume wa ile Nebo+ nyingine, 52; 34 wana wa ile Elamu+ nyingine, 1,254; 35 wana wa Harimu,+ 320; 36 wana wa Yeriko,+ 345; 37 wana wa Lodi,+ Hadidi+ na Ono,+ 721; 38 wana wa Senaa,+ 3,930.
39 Makuhani: Wana wa Yedaya+ wa nyumba ya Yeshua, 973; 40 wana wa Imeri,+ 1,052; 41 wana wa Pashuri,+ 1,247; 42 wana wa Harimu,+ 1,017.
43 Walawi: Wana wa Yeshua, wa Kadmieli,+ wa wana wa Hodeva,+ 74; 44 Waimbaji,+ wana wa Asafu,+ 148. 45 Watunza-malango,+ wana wa Shalumu,+ wana wa Ateri, wana wa Talmoni,+ wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai,+ 138.
46 Wanethini:+ Wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi,+ 47 wana wa Kerosi, wana wa Sia, wana wa Padoni,+ 48 wana wa Lebana, wana wa Hagaba,+ wana wa Salmai, 49 wana wa Hanani,+ wana wa Gideli, wana wa Gahari, 50 wana wa Reaya,+ wana wa Resini,+ wana wa Nekoda, 51 wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea, 52 wana wa Besai,+ wana wa Meunimu, wana wa Nefushesimu,+ 53 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri,+ 54 wana wa Baslithi, wana wa Mehida, wana wa Harsha,+ 55 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema,+ 56 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.+
57 Wana wa watumishi wa Sulemani:+ Wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Perida,+ 58 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli,+ 59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Amoni.+ 60 Wanethini+ wote na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.
61 Na hawa ndio waliotoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni na Imeri,+ nao hawakuweza kujua nyumba ya baba zao wala uzao wao, kama walikuwa wa Israeli: 62 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda,+ 642. 63 Na wa makuhani:+ wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai,+ aliyechukua mke kutoka kati ya binti za Barzilai+ Mgileadi naye akaitwa kwa jina lao. 64 Hao ndio wale waliotafuta kitabu chao cha kuandikisha, ili kuthibitisha ukoo wao waziwazi, nacho hakikupatikana,+ basi wakazuiwa wasiwe katika ukuhani kwa kuwa walikuwa najisi.+ 65 Basi huyo Tirshatha+ akawaambia kwamba hawapaswi kula+ vitu vitakatifu zaidi mpaka kuhani mwenye Urimu+ na Thumimu+ asimame.
66 Kutaniko zima likiwa kundi moja lilikuwa watu 42,360,+ 67 zaidi ya hao watumwa+ wao na vijakazi wao, ambao walikuwa 7,337;+ nao walikuwa na waimbaji 245, wa kiume+ na wa kike.+ 68 Farasi zao walikuwa 736, nyumbu zao 245.+ 69 Ngamia walikuwa 435. Punda+ walikuwa 6,720.+
70 Na kulikuwa na sehemu fulani ya vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ waliotoa vitu kwa ajili ya kazi.+ Huyo Tirshatha+ mwenyewe alitoa kwa ajili ya hazina drakma 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, kanzu 530 za makuhani.+ 71 Na palikuwa na sehemu fulani ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba waliotoa kwa ajili ya hazina ya kazi drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,200 za fedha.+ 72 Na watu wale wengine walitoa drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,000 za fedha na kanzu 67 za makuhani.
73 Na makuhani+ na Walawi na watunza-malango na waimbaji+ na wengine kati ya watu na Wanethini+ na Israeli wote wakaanza kukaa katika majiji yao.+ Mwezi wa saba ulipofika,+ tayari wana wa Israeli walikuwa katika majiji yao.+