Hesabu
29 “‘Na katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi huo, mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ Itakuwa siku ya kupiga tarumbeta kwenu.+ 2 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa kuwa harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba, kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 3 na toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta, vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule kondoo-dume,+ 4 na kipimo kimoja cha sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mmoja kati ya wale wana-kondoo saba;+ 5 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu;+ 6 mbali na lile toleo la kuteketezwa+ la kila mwezi na toleo lake la nafaka+ na lile toleo la kuteketezwa la daima+ na toleo lake la nafaka,+ pamoja na matoleo yake ya kinywaji,+ kulingana na utaratibu wa kawaida kwa ajili yake, kuwa harufu ya kutuliza, toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+
7 “‘Na katika siku ya kumi ya mwezi huu mtafanya mkusanyiko mtakatifu,+ nanyi mtazitesa nafsi zenu.+ Hampaswi kufanya kazi yoyote.+ 8 Nanyi mtamtolea Yehova toleo la kuteketezwa, lenye harufu ya kutuliza, ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja.+ Watakuwa wasio na kasoro kwa ajili yenu.+ 9 Na likiwa toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule kondoo-dume mmoja,+ 10 kipimo kimoja cha sehemu ya kumi vivyo hivyo kwa ajili ya kila mmoja wa wale wana-kondoo saba;+ 11 mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi, mbali na lile toleo la dhambi la upatanisho+ na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka, pamoja na matoleo yake ya kinywaji.+
12 “‘Na katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba+ mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote,+ nanyi mtamfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+ 13 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa,+ toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume wachanga kumi na watatu, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Watakuwa wasio na kasoro.+ 14 Na toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya kila ng’ombe-dume kati ya wale ng’ombe-dume kumi na watatu, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya kila kondoo-dume kati ya wale kondo-dume wawili,+ 15 na kipimo kimoja cha sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo kumi na wanne;+ 16 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi, mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima, toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
17 “‘Na katika siku ya pili ng’ombe-dume wachanga kumi na wawili, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 18 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 19 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka, pamoja na matoleo yake ya kinywaji.+
20 “‘Na katika siku ya tatu ng’ombe-dume kumi na mmoja, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 21 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida; 22 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.
23 “‘Na katika siku ya nne ng’ombe-dume kumi, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 24 toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 25 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa+ la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
26 “‘Na katika siku ya tano ng’ombe-dume tisa, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 27 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 28 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
29 “‘Na katika siku ya sita ng’ombe-dume wanane, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 30 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 31 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+
32 “‘Na katika siku ya saba ng’ombe-dume saba, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 33 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 34 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
35 “‘Na katika siku ya nane mtafanya kusanyiko kuu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ 36 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa, toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume mmoja, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 37 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, yule kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 38 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
39 “‘Hayo mtamtolea Yehova kwenye sherehe zenu za majira,+ mbali na matoleo yenu ya nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ yakiwa matoleo yenu ya kuteketezwa+ na matoleo yenu ya nafaka+ na matoleo yenu ya kinywaji+ na dhabihu zenu za ushirika.’”+ 40 Naye Musa akaongea na wana wa Israeli kulingana na kila jambo ambalo Yehova alikuwa amemwamuru Musa.+