Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 17:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 Basi wakati ule Sauli alipomwona Daudi akienda kukutana na yule Mfilisti, alimwambia Abneri+ mkuu wa jeshi: “Huyu mvulana+ ni mwana wa nani,+ Abneri?” Abneri naye akasema: “Kwa uhai wa nafsi yako, Ee mfalme, sijui kabisa!”

  • 1 Samweli 20:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Lakini Daudi akaapa+ tena na kusema: “Hakika baba yako anajua kwamba nimepata kibali machoni pako,+ na hivyo atasema, ‘Yonathani asijue jambo hili, asije akaumia moyoni.’ Lakini, kwa kweli, kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ kuna kama hatua moja tu kati yangu na kifo!”+

  • 2 Samweli 11:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ndipo Uria akamwambia Daudi: “Lile Sanduku+ na Israeli na Yuda wanakaa katika vibanda, na Yoabu bwana wangu na watumishi wa bwana wangu+ wanapiga kambi juu ya uso wa pori, nami—niende nyumbani kwangu kula na kunywa na kulala na mke wangu?+ Kama unavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi,+ sitafanya jambo hili!”

  • 2 Wafalme 2:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Na Eliya akaanza kumwambia Elisha: “Keti hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma niende mpaka Betheli.” Lakini Elisha akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ mimi sitakuacha.”+ Basi wakashuka kwenda Betheli.+

  • 2 Wafalme 4:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Kwa hiyo mama ya mvulana akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ mimi sitakuacha.”+ Kwa hiyo akaondoka, akaenda pamoja naye.

  • Mhubiri 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa;+ lakini wafu, hawajui lolote kamwe,+ wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki