Isaya
27 Katika siku ile Yehova,+ akiwa na upanga wake mgumu na wenye nguvu,+ ataelekeza uangalifu wake juu ya Lewiathani,*+ yule nyoka anayenyiririka,+ juu ya Lewiathani, yule nyoka mpotovu, na hakika yeye atamuua huyo mnyama mkubwa wa baharini+ aliye ndani ya bahari.
2 Katika siku ile mwimbieni huyo mwanamke:+ “Shamba la mizabibu+ la divai yenye kutoa povu! 3 Mimi, Yehova, ninamlinda yeye.+ Nitamnywesha maji kila wakati.+ Ili yeyote asielekeze fikira zake kupigana naye, nitamlinda usiku na mchana.+ 4 Mimi sina ghadhabu.+ Ni nani atakayenipa vichaka vya miiba+ na magugu katika pigano? Nitavikanyaga hivyo. Nitaviwasha moto kwa wakati mmoja.+ 5 Kama sivyo na ashike ngome yangu, na afanye amani pamoja nami; na afanye amani pamoja nami.”+
6 Katika siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi, Israeli+ atachanua maua na kwa kweli achipuke; na kwelikweli wao watajaza matunda juu ya uso wa nchi yenye kuzaa.+
7 Je, ni lazima mtu ampige kwa pigo kama la mtu anayempiga? Au, je, ni lazima auawe kwa mauaji kama ya watu wake waliouawa?+ 8 Utashindana naye kwa mlio wa kushtua utakapokuwa ukimfukuza. Lazima yeye atamfukuza huyo kwa mlipuko wake, ulio mkali katika siku ya upepo wa mashariki.+ 9 Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafanyiwa upatanisho,+ na haya ni matunda yote wakati anapoiondoa dhambi yake,+ wakati anapofanya mawe yote ya madhabahu kama mawe ya chokaa ambayo yamepondwa, hivi kwamba miti mitakatifu+ na vinara vya uvumba havitasimama.+ 10 Kwa maana jiji lenye ngome litakuwa peke yake, uwanja wa malisho utaachwa peke yake na kuachwa kama nyika.+ Ndama atalisha hapo, naye atalala hapo; naye kwa kweli atakula matawi yake.+ 11 Vitawi vyake vitakapokuwa vimekauka, wanawake wanaoingia watavivunja, na kuviwasha.+ Kwa maana wao ni kundi la watu lisilo na hamu ya uelewaji.+ Ndiyo sababu Mtengenezaji wake hatalionyesha rehema, na Mfanyizaji wake hatalionyesha kibali.+
12 Na itatukia katika siku ile kwamba Yehova atayapiga matunda,+ kuanzia kijito kinachotiririka cha ule Mto+ mpaka kwenye bonde la mto la Misri,+ na basi ninyi mtaokotwa mmoja baada ya mwingine,+ enyi wana wa Israeli. 13 Na itatukia katika siku ile kwamba baragumu kubwa itapigwa,+ na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru+ na wale waliotawanyika katika nchi ya Misri+ hakika watakuja na kumwinamia+ Yehova kwenye mlima mtakatifu katika Yerusalemu.+