Muziki wa Asafu.+
50 Mwenye Uwezo,+ Mungu, Yehova,+ amesema mwenyewe,+
Naye anaiita dunia,+
Kutoka mashariki mpaka magharibi.+
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu mwenyewe ameangaza.+
3 Mungu wetu atakuja naye hawezi kukaa kimya.+
Mbele zake kuna moto unaoteketeza,+
Na kumzunguka pande zote hali ya hewa imekuwa yenye dhoruba kali sana.+
4 Yeye anaziita mbingu juu na dunia+
Ili atekeleze hukumu juu ya watu wake:+
5 “Wakusanye kwangu washikamanifu wangu,+
Wale wanaofanya agano langu juu ya dhabihu.”+
6 Na mbingu zinasema juu ya uadilifu wake,+
Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ Sela.
7 “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitasema,+
Ee Israeli, nami nitatoa ushahidi dhidi yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Mimi siwakaripii kuhusiana na dhabihu zenu,+
Wala kuhusiana na matoleo yako mazima ya kuteketezwa yaliyo mbele zangu daima.+
9 Sitachukua ng’ombe-dume katika nyumba yako,+
Wala mbuzi-dume katika mazizi yako.
10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+
Wanyama walio juu ya milima elfu moja.+
11 Najua vizuri kila kiumbe chenye mabawa cha milimani,+
Na makundi ya wanyama wa porini yako pamoja nami.+
12 Ningalikuwa na njaa, singalikuambia;
Kwa maana nchi yenye kuzaa+ na vyote vinavyoijaza ni vyangu.+
13 Je, nile nyama ya ng’ombe-dume wenye nguvu,+
Na je, ninywe damu ya mbuzi-dume?+
14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+
Na umtimizie Aliye Juu Zaidi nadhiri zako;+
15 Na uniite katika siku ya taabu.+
Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+
16 Lakini Mungu atamwambia mwovu:+
“Una haki gani ya kuyataja masharti yangu,+
Na kwamba ulichukue agano langu kinywani mwako?+
17 Tazama, wewe—wewe umechukia nidhamu,+
Nawe unaendelea kuyatupa maneno yangu nyuma yako.+
18 Wakati wowote ulipomwona mwizi, naam, ulipendezwa naye;+
Nawe ulishirikiana na wazinzi.+
19 Umefungua kinywa chako kutoa lililo baya,+
Na ulimi wako unaushikamanisha na udanganyifu.+
20 Unaketi na kusema vibaya juu ya ndugu yako mwenyewe,+
Juu ya mwana wa mama yako unafichua kosa.+
21 Umeyafanya mambo hayo, nami nikaendelea kukaa kimya.+
Ulidhani kwamba kwa hakika mimi ningekuwa kama wewe.+
Nitakukaripia,+ nami nitayarekebisha mambo mbele ya macho yako.+
22 Tafadhali, enyi mnaomsahau Mungu eleweni hili,+
Nisije nikawararua vipande-vipande bila ya kuwa na mkombozi.+
23 Yule anayetoa shukrani zikiwa dhabihu yake ndiye anayenitukuza;+
Naye anayedumisha njia iliyowekwa,
Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+