Isaya
6 Katika mwaka ule aliokufa Mfalme Uzia,+ mimi, hata hivyo, nilimwona Yehova,+ akiwa ameketi juu ya kiti cha ufalme+ kilicho juu na kilichoinuliwa, na pindo za nguo yake zilikuwa zimelijaza hekalu.+ 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake.+ Kila mmoja alikuwa na mabawa sita. Aliufunika uso wake kwa mawili,+ na kwa mawili aliifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka huku na huku. 3 Na huyu akamwita yule na kusema: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+ Utukufu wake umejaa katika dunia yote.” 4 Na viegemeo+ vya milango vikaanza kutetemeka kutokana na sauti ya yule aliyekuwa akiita, na mwishowe nyumba ikajaa moshi.+
5 Nami nikasema: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimenyamazishwa, kwa sababu mimi ni mtu asiye na midomo safi,+ nami ninakaa katikati ya watu wasio na midomo safi;+ kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi, mwenyewe!”+
6 Ndipo mmoja wa maserafi akaruka kunijia, na katika mkono wake kulikuwa na kaa+ linalowaka ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka kwenye madhabahu.+ 7 Naye akakigusa kinywa+ changu na kusema: “Tazama! Hili limeigusa midomo yako, na kosa lako limeondoka na dhambi yako imefanyiwa upatanisho.”+
8 Nami nikaanza kuisikia sauti ya Yehova akisema: “Nitamtuma nani, na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?”+ Nami nikasema: “Mimi hapa! Nitume mimi.”+ 9 Naye akaendelea kusema: “Nenda, nawe uwaambie watu hawa, ‘Sikieni tena na tena, lakini msielewe; na mwone tena na tena, lakini msipate ujuzi wowote.’+ 10 Fanya moyo wa watu hawa kuwa mgumu,+ na uyafanye masikio yao kuwa magumu,+ na ushikanishe macho yao pamoja, ili wasione kwa macho yao na kwa masikio yao wasisikie, na ili moyo wao usielewe na ili kwa kweli wasigeuke na kujiponya.”+
11 Ndipo nikasema: “Ni mpaka wakati gani, Ee Yehova?”+ Kisha akasema: “Ni mpaka majiji yabomoke, yawe bila mkaaji, na nyumba ziwe bila mtu wa udongo, na nchi iharibiwe iwe ukiwa;+ 12 na kwa kweli Yehova aondolee mbali watu wa udongo, na hali ya ukiwa ienee sana katikati ya nchi.+ 13 Na bado ndani yake patakuwa na sehemu ya kumi,+ nayo itakuwa tena kitu cha kuteketezwa, kama mti mkubwa na kama mti mnene sana ambapo, inapokatwa,+ kuna kisiki;+ uzao mtakatifu utakuwa kisiki chake.”+