Danieli
12 “Na Mikaeli+ atasimama wakati huo, yule mkuu+ anayesimama+ kwa ajili ya wana wa watu wako.+ Na kutakuwa na wakati wa taabu ambayo haijapata kutokea tangu kuwapo kwa taifa lolote mpaka wakati huo.+ Na wakati huo watu wako wataponyoka,+ kila mmoja anayepatikana ameandikwa katika kile kitabu.+ 2 Na kutakuwa na wengi kati ya wale waliolala katika mavumbi ya nchi ambao wataamka,+ hawa kwa ajili ya uzima unaodumu mpaka wakati usio na kipimo+ na wale kwa ajili ya shutuma na chuki zinazodumu mpaka wakati usio na kipimo.+
3 “Na wale walio na ufahamu watang’aa kama mwangaza wa anga;+ na wale wanaoleta wengi kwenye uadilifu,+ watang’aa mpaka wakati usio na kipimo, milele kama nyota.
4 “Na wewe, Ee Danieli, yafanye siri maneno hayo na kukifunga kitabu kwa muhuri,+ mpaka wakati wa mwisho.+ Wengi watakwenda huku na huku, na ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.”+
5 Nami Danieli nikaona, na tazama! watu wengine wawili walikuwa wamesimama,+ mmoja kwenye ukingo huu wa mto na yule mwingine kwenye ukingo ule mwingine wa mto.+ 6 Ndipo mmoja akamwambia yule mtu aliyevaa kitani,+ aliyekuwa juu ya maji ya ule mto: “Itakuwa muda gani kufikia mwisho wa mambo hayo ya ajabu?”+ 7 Nami nikaanza kumsikia yule mtu aliyevaa kitani, ambaye alikuwa juu ya maji ya ule mto, alipoinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbingu na kuapa+ kwa Yule aliye hai kwa wakati usio na kipimo:+ “Itakuwa ni kwa wakati uliowekwa, nyakati zilizowekwa na nusu ya wakati.+ Na mara tu baada ya kuvunjwa vipande-vipande kwa nguvu za watu watakatifu kutakapokwisha,+ mambo hayo yote yatakwisha.”
8 Mimi nami nikasikia, lakini sikuweza kuelewa;+ basi nikauliza: “Ee bwana wangu, mwisho wa mambo hayo utakuwa nini?”+
9 Naye akaniambia tena: “Nenda, Danieli, kwa sababu maneno hayo yamewekwa siri na kufungwa kwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.+ 10 Wengi watajitakasa+ na kujifanya weupe+ na kusafishwa.+ Na waovu watatenda kwa uovu,+ wala hakuna waovu wowote watakaoelewa;+ bali wale walio na ufahamu wataelewa.+
11 “Na kutoka wakati wa kuondolewa+ kwa ile dhabihu ya daima+ na kusimamishwa kwa lile chukizo+ linalosababisha ukiwa, kutakuwa na siku 1,290.
12 “Mwenye furaha+ ni yule anayeendelea kutarajia na anayefika kwenye zile siku 1,335!
13 “Wewe nawe, nenda zako kuelekea ule mwisho;+ nawe utapumzika,+ lakini utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.”+